Kama unahitaji chumba na sebule Mwenge DSM vipo

Kama unahitaji chumba na sebule Mwenge DSM vipo

Hivi watu wengine mpo Tanzania ipi au Dar ipi hasa?

Kisa cha kushangaa Kodi ya Pango kwa Chumbakimoja-na-sebule yake kuwa Tshs. laki 2.?

Kwa taarifa yenu tu, Mfano;
Mimi ninavyo sehemu Dar hiihii,
Chumba 1 na Sebule vya hadi $800 na sio kwamba hii ndio bei ya juu zaidi, La hasha, Na-
Ndio,Sijakosea ni Dola za Marekani Mia-nane -
(Yaani zaidi ya Shilingi Milioni moja na Laki tatu ya Tanzania kwa mwezi mmoja)

Na wapo Wateja unaweza ukampeleka kuiona hii kisha akaikataa,
Kwa kuwa haijakidhi kiwango anachotaka na hivyo atafutiwe nyingine bora zaidi.

Yaani hoja kwake si Pesa, Hoja ni Kiwango na Ubora wa Mali.
Pia wapo miongoni mwao Waswahili kama wewe na mimi wanaishi maisha ya level hiyo.

Wakati wewe unatembea kuitafuta mafanikia, Wapo wenzako wameshayapata na wanayaboresha zaidi kwa kasi ubwa sana, Jaribu kustuka sasa na anza kukimbia kuwaiga wao sasa,
Mh!, Wenzako na wataona kukimbia sio dili wataanza kupaa kabisa,

Kifupi nakupa Somo la bure:
Jipange kimaisha, fatuta mafanikio badala ya kupiga bwanya na kuona kuwa kila kitu nikigumu
na hakiwezekani au hakipo.

Habari ndio hiyo.

Kaka hakuna anayeshangaa. Ila Dar bei za nyumba ni kubwa sana bila sababu. Watu wenyewe hata kodi ya ardhi hawalipi. Mimi nilikaa Msasani. Kulikuwa na nyumba yenye chumba na sebule. Kwa sababu ya AC na tiles tu nikaishia kulipa laki 5 kwa mwezi. Lakini nikaja kuona huu ni upuuzi. Siwezi nikawa napoteza pesa nyingi hivi wakati hata mimi naweza nikajenga kwa hizo pesa ninazompa landlord.
Labda tunapigwa kwa sababu wengi wetu twapenda kujikusanya katikati ya mji.
 
Kinachomfanya MTU akamuliwe kodi kubwa ni kupenda majivuno...kujikweza..nyumba inaweza kuwa nzuri pugu asiipende na akataka chumba na sebule huko msasasi..Pride do more harm usipogundua
 
Mimi nna kitu kama hicho pugu..kama utapenda alafu nataka 100 tu
 
Kuna vinavyojitegemaea na pia kuna ambavyo vimefwatana vimne kila sehem luku yake, maji yapo ya kutosha.
 
Bado vyumba vipo karibuni.
 
kisa na mkasa cha kushangaa kodi ya pango kwa chumbakimoja-na-sebule yake
kuwa tshs. Laki 2.?

Kwa taarifa tu, mfano;
mimi ninavyo sehemu dar hiihii,
vyumba 2 na sebule vya $1200, pia si kwamba hii ndio bei ya juu zaidi,
la hasha, na-ndio, sijakosea ni dola za marekani elfu moja na mia mbili -
(yaani zaidi ya shilingi milioni 2 za tanzania kodi ya pango kwa mwezi mmoja)

hapo mtasemaje?

dalali being dalali.......apartment nzuri zipo kuanzia $1200 wewe utuletee habari ya chumba $1200
 
dalali being dalali.......apartment nzuri zipo kuanzia $1200 wewe utuletee habari ya chumba $1200
Soma uzi mkuu kisha uje uzi wangu, uta-realize umekurupuka.
And i am not ready for some unnecessary arguments; sin.jpg
 
dalali being dalali.......apartment nzuri zipo kuanzia $1200 wewe utuletee habari ya chumba $1200

zipo studio appartents (chumba kimoja) za zaidi ya hiyo $1200 kaka, location ndiyo inayouza!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom