Hivi watu wengine mpo Tanzania ipi au Dar ipi hasa?
Kisa cha kushangaa Kodi ya Pango kwa Chumbakimoja-na-sebule yake kuwa Tshs. laki 2.?
Kwa taarifa yenu tu, Mfano;
Mimi ninavyo sehemu Dar hiihii,
Chumba 1 na Sebule vya hadi $800 na sio kwamba hii ndio bei ya juu zaidi, La hasha, Na-
Ndio,Sijakosea ni Dola za Marekani Mia-nane -
(Yaani zaidi ya Shilingi Milioni moja na Laki tatu ya Tanzania kwa mwezi mmoja)
Na wapo Wateja unaweza ukampeleka kuiona hii kisha akaikataa,
Kwa kuwa haijakidhi kiwango anachotaka na hivyo atafutiwe nyingine bora zaidi.
Yaani hoja kwake si Pesa, Hoja ni Kiwango na Ubora wa Mali.
Pia wapo miongoni mwao Waswahili kama wewe na mimi wanaishi maisha ya level hiyo.
Wakati wewe unatembea kuitafuta mafanikia, Wapo wenzako wameshayapata na wanayaboresha zaidi kwa kasi ubwa sana, Jaribu kustuka sasa na anza kukimbia kuwaiga wao sasa,
Mh!, Wenzako na wataona kukimbia sio dili wataanza kupaa kabisa,
Kifupi nakupa Somo la bure:
Jipange kimaisha, fatuta mafanikio badala ya kupiga bwanya na kuona kuwa kila kitu nikigumu
na hakiwezekani au hakipo.
Habari ndio hiyo.