Sdm
Member
- Dec 11, 2017
- 40
- 70
Kuanzia nimlete huyu kijana kuchunga kondoo zangu.. Kijana simuelewi.. Miaka miwili tu akiwa kazini kondoo zangu zinakufa kwa kasi..
Mara nyingine najiuliza kweli ataweza kuchunga hawa kondoo miaka kumi ijayo? Nahisi zizi lote litakuwa limeisha..
Nikiomba ushauri kwa watu wananiambia ni mfugaji mzuri. Lakini mbona hayupo kama wale vijana niliowaajiri miaka ya nyuma?
Nasikitika sana siku moja kondoo wangu alichapwa viboko zaidi ya 30 mguuni.. Nilipomuuliza akajibu ni vijana wasiojulikana ndo wamemchapa.
Siku hizi pia kondoo wangu wengi wapo mitaani.. Alinihaidi angewapeleka marishoni baada ya kutoka kuhasiwa.. Kwani kondoo walihasiwa vizuri sana.. Cha ajabu mpaka leo wapo tu kwenye mazizi na mama zao bado wananyonya.. Huyu kijana hajawapeleka malishoni..
Mlango wa zizi umebana hata mwenyewe kuufungua nashindwa lakini huyu kijana akanambia ninunue grisi nipake.. Kwenda dukani nakuta grisi imepanda bei..
Huyu kijana simuelewi kabisa yani.. Maana naona siku hizi kondoo wamekuwa waoga sana.. Ukipita nje kwa kishindo utasikia kelele humo zizini za kuogopa..
Sielewi anawafanya nini kondoo zangu wakati sipo..nikimuangalia kwa nje anaonekana ni kijana jasiri sana.. Cha ajabu juzi kondoo wamekamatwa kwenye shamba la jirani hata hakuongea kitu mahakamani.
Kila siku kondoo wanapungua lakini napomuuliza anakaa kimya wakati fulani. Nashindwa nimfanye nini kwa sababu ni mtoto wa mdogo wa mke wangu. Naogopa nikimzingua mke wangu atasema nimemuonea..
Juzi alisema hela ya kununua madawa na kuwalipa walimu wanaotufundisha kuhusu mifugo yetu isipate magonjwa alisema imeshatoka kwa wahisani.. Cha ajabu mpaka leo nimemkuta bwana mifugo mmoja kanambia hajalipwa hela.
Watanzania wenzangu naumia sana moyoni mpaka nimeamua kuandika leo.. Mambo mengine yanaudhi sana..
Hao kondoo waliokosa majani baada ya kukaa zizini mpaka saa tisa jioni na wakavunja zizi na kuandamana kwenda malishoni ili wakajitafutie chakula kwa mikono yao.. Alichowafanya yeye na rafiki zake ndo wanajua.. Mpaka kondoo mmoja wa jirani kapoteza maisha kwa kupigwa kiboko kichwani kwa uzembe mkubwa.
Huyu kondoo tena alikuwa jike. Mwenye afya nzuri nilishamuandaa baada ya miaka mitatu alete uzao mzuri nyumbani.. Lakini kapigwa kiboko cha kichwa na kupoteza maisha.. Hakuwa na hatia afu alinawiri sana.. Leo hayupo.
Siyo kwamba namchukia huyu kijana kwanza ni ndugu yangu na mtanzania mwenzangu.. Ila matendo yake kwa mifugo yangu siyo mazuri.. Mifugo inazidi kufa..
Yule kondoo aliyepotea Saanane za mchana mpaka leo sijamuona.. Nikimuuliza anasema alikatika kwenye malisho.. Nikimuuliza mama yake Ben naye anajibu eti Ben kwao hayupo wanasema tangia aondoke haieleweki alienda wapi.
Nawaza sana hawa kondoo zangu na mbuzi zizini walivokonda.. Daladala zangu siku hizi nazo hazifanyi kazi maana sina kipato hata cha kuweza kununua mafuta.. Cha msingi nilichowaza ni kufukuza makonda wote watoke kwani nao hawajaleta hata shillingi na wamekuwa walevi wa Pombe..
Watanzania wenzangu nishaurini nifanye nini kwani nimechoka.. Huyu kijana ananinyapapaa mpaka nakosa hamu ya tendo la ndoa na mke wangu... Mapovu ya sabuni sitaki... FIKRA PEVU.
Mara nyingine najiuliza kweli ataweza kuchunga hawa kondoo miaka kumi ijayo? Nahisi zizi lote litakuwa limeisha..
Nikiomba ushauri kwa watu wananiambia ni mfugaji mzuri. Lakini mbona hayupo kama wale vijana niliowaajiri miaka ya nyuma?
Nasikitika sana siku moja kondoo wangu alichapwa viboko zaidi ya 30 mguuni.. Nilipomuuliza akajibu ni vijana wasiojulikana ndo wamemchapa.
Siku hizi pia kondoo wangu wengi wapo mitaani.. Alinihaidi angewapeleka marishoni baada ya kutoka kuhasiwa.. Kwani kondoo walihasiwa vizuri sana.. Cha ajabu mpaka leo wapo tu kwenye mazizi na mama zao bado wananyonya.. Huyu kijana hajawapeleka malishoni..
Mlango wa zizi umebana hata mwenyewe kuufungua nashindwa lakini huyu kijana akanambia ninunue grisi nipake.. Kwenda dukani nakuta grisi imepanda bei..
Huyu kijana simuelewi kabisa yani.. Maana naona siku hizi kondoo wamekuwa waoga sana.. Ukipita nje kwa kishindo utasikia kelele humo zizini za kuogopa..
Sielewi anawafanya nini kondoo zangu wakati sipo..nikimuangalia kwa nje anaonekana ni kijana jasiri sana.. Cha ajabu juzi kondoo wamekamatwa kwenye shamba la jirani hata hakuongea kitu mahakamani.
Kila siku kondoo wanapungua lakini napomuuliza anakaa kimya wakati fulani. Nashindwa nimfanye nini kwa sababu ni mtoto wa mdogo wa mke wangu. Naogopa nikimzingua mke wangu atasema nimemuonea..
Juzi alisema hela ya kununua madawa na kuwalipa walimu wanaotufundisha kuhusu mifugo yetu isipate magonjwa alisema imeshatoka kwa wahisani.. Cha ajabu mpaka leo nimemkuta bwana mifugo mmoja kanambia hajalipwa hela.
Watanzania wenzangu naumia sana moyoni mpaka nimeamua kuandika leo.. Mambo mengine yanaudhi sana..
Hao kondoo waliokosa majani baada ya kukaa zizini mpaka saa tisa jioni na wakavunja zizi na kuandamana kwenda malishoni ili wakajitafutie chakula kwa mikono yao.. Alichowafanya yeye na rafiki zake ndo wanajua.. Mpaka kondoo mmoja wa jirani kapoteza maisha kwa kupigwa kiboko kichwani kwa uzembe mkubwa.
Huyu kondoo tena alikuwa jike. Mwenye afya nzuri nilishamuandaa baada ya miaka mitatu alete uzao mzuri nyumbani.. Lakini kapigwa kiboko cha kichwa na kupoteza maisha.. Hakuwa na hatia afu alinawiri sana.. Leo hayupo.
Siyo kwamba namchukia huyu kijana kwanza ni ndugu yangu na mtanzania mwenzangu.. Ila matendo yake kwa mifugo yangu siyo mazuri.. Mifugo inazidi kufa..
Yule kondoo aliyepotea Saanane za mchana mpaka leo sijamuona.. Nikimuuliza anasema alikatika kwenye malisho.. Nikimuuliza mama yake Ben naye anajibu eti Ben kwao hayupo wanasema tangia aondoke haieleweki alienda wapi.
Nawaza sana hawa kondoo zangu na mbuzi zizini walivokonda.. Daladala zangu siku hizi nazo hazifanyi kazi maana sina kipato hata cha kuweza kununua mafuta.. Cha msingi nilichowaza ni kufukuza makonda wote watoke kwani nao hawajaleta hata shillingi na wamekuwa walevi wa Pombe..
Watanzania wenzangu nishaurini nifanye nini kwani nimechoka.. Huyu kijana ananinyapapaa mpaka nakosa hamu ya tendo la ndoa na mke wangu... Mapovu ya sabuni sitaki... FIKRA PEVU.