Kama TISS wataamua kuwa wauaji, watekaji na watesaji, kuna kiongozi wa upinzani atasalimika?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuna Waziri na Msemaji wa Wizara. Pia kila taasisi ndani ya wizara hiyo iwe Jeshi la Magereza, Zimamoto, Uhamiaji na Polisi wana msemaji wao ambaye ndiye hutoa ufafanuzi pindi hoja inapoibuka inayohitaji ufafanuzi.

Hiyo haipo kwa TISS. Wanafanya kazi kubwa sana katika kulinda amani ya nchi hii na kuzuia matukio kabla hayajatokea. Ni kutokana na kazi zao ndio maana Tanzania inakuwa nchi ya mfano Barani Afrika kwa kuwa na amani na utulivu. Ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Hawa jamaa hawalali na kila mahala wapo. Wanawajibika usiku na mchana kuhakikisha kila mtu analindwa na anatendewa haki.

Kwa sasa imekuwa ni kama fasheni kila mtu anaibuka na hoja na kujifanya anaijua sana TISS na kuihusisha na kila jambo baya linalotokea katika nchi hii. Waandishi wa Habari, wanasiasa na hata wasanii ambao hawajui hata nini maana ya TISS ndio hujifanya wanaijua sana Taasisi hiyo ambayo nina hakika hata viongozi wakuu wa nchi hawaijui na hawatakuja kuijua kwa vile na wao ni sehemu ya watuhumiwa wa taasisi hiyo.

Kila mtu ana uhuru wa kuongea. Ila uhuru usio na mipaka ni vurugu. Kutokana na TISS kuwa na muundo ambao haulazimishi kazi zao kutangazwa kwenye public, kumetoa mwanya kwa ngumbaru wa taasisi hiyo kujitokeza na kujifanya kuwa wasemaji. Hawana Waziri mwenye dhamana ya moja kwa moja na Taasisi yao. Hawana Msemaji wa Taasisi. Hawana Bajeti inayoonekana. Hawana specific goals ambayo public inaweza kuwajudge. Kwa ujumla TISS ndio kila kitu katika nchi hii.

Kwa upande wangu siamini kama TISS ni wauaji, watesaji na wanyanyasaji kama wengine wanavyosema. Siamini kama TISS inajihusisha na utekaji kama wengine wanavyodai. Ninachojua TISS kote ulimwenguni huwashughulikia wavurugaji wa amani na hufanya hivyo kabla wahusika hawajafanya tukio. Tena wanakushughulikia hadharani na hata ukipiga kelele hakuna atakayekutetea.

Wale wote mnaolalamikia kuwa TISS inaua na kutesa watu, mna uhakika na hayo msemayo? Hivi kama TISS inamshughulikia kila mtu, mbona Mgombea wa CHADEMA, 2015, Edward Lowasa na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye wanalindwa na maafisa Usalama wa Taifa? Kama lengo ni kuua wapinzani, si hao walinzi wangewatumia kuwafyatulia risasi ama kuwapa sumu ili wakufilie mbali?

Kuna wakati Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe aliwahi kutekwa na nusura auawe. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliomuokoa na Mbowe anajua hayo.

Kuna wakati Zitto Kabwe aliwahi kuwekewa sumu kwenye Maji ya kunywa pale Lunch Time Hotel na aliyehusika kuweka sumu hiyo ni Ben Saanane. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliofichua mkakati huo na Zitto analijua hilo. Ipo mifano mingi sana na laiti kama hawa Maafisa watatoa ushuhuda wa jinsi walivyoliokoa taifa hili basi leo hii wanasiasa wangekuwa wa kwanza kuitetea na kuipa nguvu TISS na si sasa ambapo kila mmoja anajifanya ni mkosoaji na anaijua sana taasisi hiyo.

Najiuliza sana. Hivi ikitokea TISS wakaamua sasa kutekeleza matakwa wanayovikwa na wanasiasa wa upinzani ya kuua, kuteka na kutesa watu, kuna mwanasiasa wa upinzani atasalimika?
 
TISS kama idara huenda haifanyi huo utesaji, lakini kuna watu ndani ya Idara kwa kutumia udhaifu wa Boss mkuu wanafanya utesaji huo na utekaji huo.

Kama Bashite ndiye right-hand man wa BigBoss na akapewa "vijana" chini yake toka idarani unafikiri atashindwa kutesa na kufanya hayo.

Nape katolewa bastola na mtu aliyekuwa amepanda gari yenye namba za Ofisi kubwa ya magogoni, Clouds inavamiwa na watu waliovaa sare za kutoka pale Kijitonyama idarani, tuseme yote hayo yametokea kimakosa??

Kila anayetekwa na kuteswa anazitaja safe-house za idara kuwa zilitumika kutesa, kwa nini tusijenge picha kwamba kuna mkono wa idara hii nyeti??

Rais Mwinyi aliwahi kutenguliwa uwaziri wa mambo ya ndani kwa sababu hii hii ya TISS kuvurunda kwa kutesa na sheria ikapelekwa bungeni ya kuinyang'anya idara mamlaka ya kukamata, ikabaki na mamlaka iliyo nayo leo baada ya kuanza kuota makucha kwa sababu sheria iliwapa favor kidogo.

Kwa historia ya nyuma yaliyotokea wakati wa Nyerere ni dhahiri hwa jamaa huwa inafika wakati wanakengeuka hasa wanapopata Boss mfanya maamuzi ambaye aidha ni mpole sana kama alivyokuwa Mwinyi wakati ni Waziri wa mambo ya ndani au Boss mwenye ajenda kama hizi za kurundika watu wasio competent kama kina Bashite.

Kuna mambo mkuu inabidi achague, aidha kurudi kwenye misingi na kutowatumia hawa akina Bashite kwenye mambo nyeti ya kitaifa ili kuficha aibu inayoikumba sasa idara, au afanye witch-hunt ya kutafuta vimeo wote ndani ya idara wanaoichafua kwa kuteka na kutesa watu.

Suala la viongozi wa upinzani kutotekwa ni suala la muda tu, kama Mbowe alipigwa bomu Arusha mkutanoni, na Dokta Slaa aliwekewa mpaka kamera kwenye chumba chake cha kulala hotelini, kwa nini washindwe kuwateka na kuwatesa??

Ni suala la muda tu.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuna Waziri na Msemaji wa Wizara. Pia kila taasisi ndani ya wizara hiyo iwe Jeshi la Magereza, Zimamoto, Uhamiaji na Polisi wana msemaji wao ambaye ndiye hutoa ufafanuzi pindi hoja inapoibuka inayohitaji ufafanuzi.

Hiyo haipo kwa TISS. Wanafanya kazi kubwa sana katika kulinda amani ya nchi hii na kuzuia matukio kabla hayajatokea. Ni kutokana na kazi zao ndio maana Tanzania inakuwa nchi ya mfano Barani Afrika kwa kuwa na amani na utulivu. Ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Hawa jamaa hawalali na kila mahala wapo. Wanawajibika usiku na mchana kuhakikisha kila mtu analindwa na anatendewa haki.

Kwa sasa imekuwa ni kama fasheni kila mtu anaibuka na hoja na kujifanya anaijua sana TISS na kuihusisha na kila jambo baya linalotokea katika nchi hii. Waandishi wa Habari, wanasiasa na hata wasanii ambao hawajui hata nini maana ya TISS ndio hujifanya wanaijua sana Taasisi hiyo ambayo nina hakika hata viongozi wakuu wa nchi hawaijui na hawatakuja kuijua kwa vile na wao ni sehemu ya watuhumiwa wa taasisi hiyo.

Kila mtu ana uhuru wa kuongea. Ila uhuru usio na mipaka ni vurugu. Kutokana na TISS kuwa na muundo ambao haulazimishi kazi zao kutangazwa kwenye public, kumetoa mwanya kwa ngumbaru wa taasisi hiyo kujitokeza na kujifanya kuwa wasemaji. Hawana Waziri mwenye dhamana ya moja kwa moja na Taasisi yao. Hawana Msemaji wa Taasisi. Hawana Bajeti inayoonekana. Hawana specific goals ambayo public inaweza kuwajudge. Kwa ujumla TISS ndio kila kitu katika nchi hii.

Kwa upande wangu siamini kama TISS ni wauaji, watesaji na wanyanyasaji kama wengine wanavyosema. Siamini kama TISS inajihusisha na utekaji kama wengine wanavyodai. Ninachojua TISS kote ulimwenguni huwashughulikia wavurugaji wa amani na hufanya hivyo kabla wahusika hawajafanya tukio. Tena wanakushughulikia hadharani na hata ukipiga kelele hakuna atakayekutetea.

Wale wote mnaolalamikia kuwa TISS inaua na kutesa watu, mna uhakika na hayo msemayo? Hivi kama TISS inamshughulikia kila mtu, mbona Mgombea wa CHADEMA, 2015, Edward Lowasa na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye wanalindwa na maafisa Usalama wa Taifa? Kama lengo ni kuua wapinzani, si hao walinzi wangewatumia kuwafyatulia risasi ama kuwapa sumu ili wakufilie mbali?

Kuna wakati Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe aliwahi kutekwa na nusura auawe. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliomuokoa na Mbowe anajua hayo.

Kuna wakati Zitto Kabwe aliwahi kuwekewa sumu kwenye Maji ya kunywa pale Lunch Time Hotel na aliyehusika kuweka sumu hiyo ni Ben Saanane. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliofichua mkakati huo na Zitto analijua hilo. Ipo mifano mingi sana na laiti kama hawa Maafisa watatoa ushuhuda wa jinsi walivyoliokoa taifa hili basi leo hii wanasiasa wangekuwa wa kwanza kuitetea na kuipa nguvu TISS na si sasa ambapo kila mmoja anajifanya ni mkosoaji na anaijua sana taasisi hiyo.

Najiuliza sana. Hivi ikitokea TISS wakaamua sasa kutekeleza matakwa wanayovikwa na wanasiasa wa upinzani ya kuua, kuteka na kutesa watu, kuna mwanasiasa wa upinzani atasalimika?

Jaribu tena.
 
Na ww unauhakika gn unavyowatetea wakti mambo yao ni yasiri na hatakama wakitenda unadhan watakyja kukiri au unadhan tiss wao hawana upandee na waosio binadam na kama hawahusiki mbn matykio mengi sn ya ajabu yanayohusishwa na siasa mengi hatupati muafaka wao VIP suala LA ulmbok?VP suala LA been saaanane ?VP suala LA alphonc mawazo ?


Homework kwako lizibon mbn we kila jambo LA serkali unaungaty mkono inaman serkali haikoseii au MTU ukishapewa mamlaka ubinadamu unapotea mana we kila kitu unatetea ty chemsha brain yko kk daaaaaaaaaaa? Vijana tumeonywa kuwa mabwana ndioo mzee kwa kila kitu duuuuuuuuu badilika brooo
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuna Waziri na Msemaji wa Wizara. Pia kila taasisi ndani ya wizara hiyo iwe Jeshi la Magereza, Zimamoto, Uhamiaji na Polisi wana msemaji wao ambaye ndiye hutoa ufafanuzi pindi hoja inapoibuka inayohitaji ufafanuzi.

Hiyo haipo kwa TISS. Wanafanya kazi kubwa sana katika kulinda amani ya nchi hii na kuzuia matukio kabla hayajatokea. Ni kutokana na kazi zao ndio maana Tanzania inakuwa nchi ya mfano Barani Afrika kwa kuwa na amani na utulivu. Ukiona vyaelea ujue vimeundwa. Hawa jamaa hawalali na kila mahala wapo. Wanawajibika usiku na mchana kuhakikisha kila mtu analindwa na anatendewa haki.

Kwa sasa imekuwa ni kama fasheni kila mtu anaibuka na hoja na kujifanya anaijua sana TISS na kuihusisha na kila jambo baya linalotokea katika nchi hii. Waandishi wa Habari, wanasiasa na hata wasanii ambao hawajui hata nini maana ya TISS ndio hujifanya wanaijua sana Taasisi hiyo ambayo nina hakika hata viongozi wakuu wa nchi hawaijui na hawatakuja kuijua kwa vile na wao ni sehemu ya watuhumiwa wa taasisi hiyo.

Kila mtu ana uhuru wa kuongea. Ila uhuru usio na mipaka ni vurugu. Kutokana na TISS kuwa na muundo ambao haulazimishi kazi zao kutangazwa kwenye public, kumetoa mwanya kwa ngumbaru wa taasisi hiyo kujitokeza na kujifanya kuwa wasemaji. Hawana Waziri mwenye dhamana ya moja kwa moja na Taasisi yao. Hawana Msemaji wa Taasisi. Hawana Bajeti inayoonekana. Hawana specific goals ambayo public inaweza kuwajudge. Kwa ujumla TISS ndio kila kitu katika nchi hii.

Kwa upande wangu siamini kama TISS ni wauaji, watesaji na wanyanyasaji kama wengine wanavyosema. Siamini kama TISS inajihusisha na utekaji kama wengine wanavyodai. Ninachojua TISS kote ulimwenguni huwashughulikia wavurugaji wa amani na hufanya hivyo kabla wahusika hawajafanya tukio. Tena wanakushughulikia hadharani na hata ukipiga kelele hakuna atakayekutetea.

Wale wote mnaolalamikia kuwa TISS inaua na kutesa watu, mna uhakika na hayo msemayo? Hivi kama TISS inamshughulikia kila mtu, mbona Mgombea wa CHADEMA, 2015, Edward Lowasa na Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye wanalindwa na maafisa Usalama wa Taifa? Kama lengo ni kuua wapinzani, si hao walinzi wangewatumia kuwafyatulia risasi ama kuwapa sumu ili wakufilie mbali?

Kuna wakati Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe aliwahi kutekwa na nusura auawe. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliomuokoa na Mbowe anajua hayo.

Kuna wakati Zitto Kabwe aliwahi kuwekewa sumu kwenye Maji ya kunywa pale Lunch Time Hotel na aliyehusika kuweka sumu hiyo ni Ben Saanane. Ni Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ndio waliofichua mkakati huo na Zitto analijua hilo. Ipo mifano mingi sana na laiti kama hawa Maafisa watatoa ushuhuda wa jinsi walivyoliokoa taifa hili basi leo hii wanasiasa wangekuwa wa kwanza kuitetea na kuipa nguvu TISS na si sasa ambapo kila mmoja anajifanya ni mkosoaji na anaijua sana taasisi hiyo.

Najiuliza sana. Hivi ikitokea TISS wakaamua sasa kutekeleza matakwa wanayovikwa na wanasiasa wa upinzani ya kuua, kuteka na kutesa watu, kuna mwanasiasa wa upinzani atasalimika?
Ulichoandika hakieleweki ndio maana huna "like" hata Moja!
 
kwani umepostia chooni mkuu?

itabidi utupe experience
Nazungumzia alichokiongea hakuna tofauti na takataka ya chooni tu. Ni nani asiyeyajua matendo ya hao jamaa? Ninapata shida sana ni kwa nini wateke watu? Wanachoogopa ni nini? Kama hao wanaowalinda ni wasafi ni kwa nini wateke na kutesa walipakodi ambao ndio waliowaajiri?
 
Pamoja na pumba ambazo umeziandika kamuulize Hussein Bashe TISS walimfanyaje huu uonevu tulikuwa tunausikia wa upinzani sasa umerudi kwa wabunge wa CCM wakitoka hapo watakuwa kwako
 
Watanzania tunaoneka tumevimbiwa na ushwari.TISS wakilala siku moja tu,nchi hii haitakalika.
Ni mafisadi,wapiga dili na wauza unga na mawakala wao ndio wanapiga kelele TISS ivunjwe
 
Wangekuwa kwa ajili ya chama cha siasa leo hii chadema wangefutika tanzania
Sasa heading ya hii thread sijaielewa. Imeandikwa TISS wangekuwa wanateka watu, basi viongozi wa upinzani wangesinge pona, hoja yangu ni kuwa hao wapinzani ni maadui wa TISS au? Pili labda wapinzani sio watanzania au? Nadhani hii yote inatokana na katiba mbovu tuliyonayo, hakika bila kupata katiba mpya haya mambo hayataisha. Mungu atupe ujasiri
 
Back
Top Bottom