Kama taifa, tusipoona faida ya mawazo mbadala, kamwe tusitegemee kulipeleka taifa hili popote

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Nimewaza sana!

Na acha ninakiri mbele zenu kuwa kwa minyukano hii inayovuka mipaka ya kidemokrasia, sisi kama taifa; tusipoona faida ya mawazo mbadala, kamwe, narudia tena kamwe, tusitegemee kulipeleka taifa hili popote.

Juzi niliwasikia washabiki wa Yanga wakiwaambai wenzao wa Simba kuwa; wako tayari kuwalipia deni yote ile waliloamriwa na fifa kwa madai kuwa watani wao hao wakishushwa daraja; ligi haitakuwa na changamoto.

Sikia watu wa mpira wanavyojua maana ya ushindani.

Ndugu zangu watanzania chonde msiendelee kudanganywa na kudanganyika!
Ni kwamba nchi haiendelei, wala haitatokea iendelea; si kwa sababu ya nyingine yeyote ile, isipokuwa kwa ile ya kuukataa mwendo wa demokrasia unaoanzia kwenye msuguano wa fikra.

Viongozi wetu waliotangulia walikuwa si wabaya kivile lakini hata hivyo nao walikwama kwa sababu ya kukataa kitu kilekile kimoja kiitwacho mwendo wa demokrasia ya msuguano!

Ndugu zangu mara nyingi maendeleo hayaji katika jamii inayowahofu viongozi wao isipokuwa katika viongozi wanaozihofu jamii yao!
Iwapo wananchi watakuwa na mbadala wa chama tawala na kweli wakawa na uwezo wa kufanya mabadiriko ni hakika chama chochote kile kitakachokuwa madarakani kitawahudumia kwa hofu ya kuondolewa kisipofanya hivyo.

Ndiyo maana mimi huwa nasema heri kuwa na bunge la chama kimoja kikatiba kuliko kuwa na bunge la vyama vingi lenye wabunge wachache wa mawazo mbadala na hao wachache wakawa wamedhibitiwa vilivyo!
Najiuliza tena na tena tunalifanya hili na kulishabikia kwa faida ya nani?

Iwapo ccm hawatagundua kuwa wanatakiwa kubaki madarakani kwa utendaji wao na si vinginevyo, basi tusitegemee lolote la maana kutoka kwa wenzetu hawa.

Kwa kulitakia mema taifa hili na si kuwatakia mema wapinzani; kama wengi wao wanavyodhani!
Ni wao wanawajibika kuuandaa na kuuimalisha upinzani nchini ili wao watakapochokwa na wanachi wakae pembeni kama mawazo mbadala.

Na kuwa watakapo kuja katika kambi ya mawazo mbadala watanikuta nawasubiri maana mimi nilishaamua kuwa wa kudumu katika upande huu NASA pale nilipogundua kuwa wote hatuwezi kuwa na mawazo ya upande mmoja.

Tukipevuka na kufikia kiwango hicho, basi ni lazima maendeleo yatapatikana tu!

Maana tutakuwa tumetambua kuwa sisi sote ni ndugu ndani ya boma moja!

Nawasilisha.
 
Nimewaza sana!

Na acha ninakiri mbele zenu kuwa kwa minyukano hii inayovuka mipaka ya kidemokrasia, sisi kama taifa; tusipoona faida ya mawazo mbadala, kamwe, narudia tena kamwe, tusitegemee kulipeleka taifa hili popote.

Juzi niliwasikia washabiki wa Yanga wakiwaambai wenzao wa Simba kuwa; wako tayari kuwalipia deni yote ile waliloamriwa na fifa kwa madai kuwa watani wao hao wakishushwa daraja; ligi haitakuwa na changamoto.

Sikia watu wa mpira wanavyojua maana ya ushindani.

Ndugu zangu watanzania chonde msiendelee kudanganywa na kudanganyika!
Ni kwamba nchi haiendelei, wala haitatokea iendelea; si kwa sababu ya nyingine yeyote ile, isipokuwa kwa ile ya kuukataa mwendo wa demokrasia unaoanzia kwenye msuguano wa fikra.

Viongozi wetu waliotangulia walikuwa si wabaya kivile lakini hata hivyo nao walikwama kwa sababu ya kukataa kitu kilekile kimoja kiitwacho mwendo wa demokrasia ya msuguano!

Ndugu zangu mara nyingi maendeleo hayaji katika jamii inayowahofu viongozi wao isipokuwa katika viongozi wanaozihofu jamii yao!
Iwapo wananchi watakuwa na mbadala wa chama tawala na kweli wakawa na uwezo wa kufanya mabadiriko ni hakika chama chochote kile kitakachokuwa madarakani kitawahudumia kwa hofu ya kuondolewa kisipofanya hivyo.

Ndiyo maana mimi huwa nasema heri kuwa na bunge la chama kimoja kikatiba kuliko kuwa na bunge la vyama vingi lenye wabunge wachache wa mawazo mbadala na hao wachache wakawa wamedhibitiwa vilivyo!
Najiuliza tena na tena tunalifanya hili na kulishabikia kwa faida ya nani?

Iwapo ccm hawatagundua kuwa wanatakiwa kubaki madarakani kwa utendaji wao na si vinginevyo, basi tusitegemee lolote la maana kutoka kwa wenzetu hawa.

Kwa kulitakia mema taifa hili na si kuwatakia mema wapinzani; kama wengi wao wanavyodhani!
Ni wao wanawajibika kuuandaa na kuuimalisha upinzani nchini ili wao watakapochokwa na wanachi wakae pembeni kama mawazo mbadala.

Na kuwa watakapo kuja katika kambi ya mawazo mbadala watanikuta nawasubiri maana mimi nilishaamua kuwa wa kudumu katika upande huu NASA pale nilipogundua kuwa wote hatuwezi kuwa na mawazo ya upande mmoja.

Tukipevuka na kufikia kiwango hicho, basi ni lazima maendeleo yatapatikana tu!

Maana tutakuwa tumetambua kuwa sisi sote ni ndugu ndani ya boma moja!

Nawasilisha.

mh... kweli uliyoandika china wanademocrasia gani , democrisia ni unafiki tu na gharama kwa walipa kodi
hata waasis wa hiyo demo-crasee , wameshindwa kuitekeleza
 
Ndiyo maana nikasema ni bora ya kuwa na demokrasia ya kweli au mfumo wa chama kimoja; kwa maana ya kuujenga upinzani wa ndani wenye mawazo mbadala.
Tatizo letu ni huo upopo wetu mnaousifia!
 
Mleta uzi heshima kwako. Sina haja ya kuujua mrengo unaouumini ila naamini unaitetea demokrasia ya kweli yenye kuruhusu fair play kwa kila team. Kuna watu wapo hapo ccm ni waoga mno wa mabadiliko. Sijui wanayaanzia katika stage gani katika zile tano kwanapoyatafakari. Wapunguze hofu na wapende kuupata mrejeo.
 
demokrasia bila sheria ni vurugu, ndo maana waziri mkuu msitafu alitamka, ukikatazwa jambo ukafanya utapigwa tu, sheria lazima ifuatwe, huwepo wa democrasia sio tija ya kutofuata sheria na taratibu
 
Njia ya kunusuru Demokrasia hapa Tanzania napendekeza Katiba afanyiwe marekebisho ili:-
1. Private candidate akubaliwe
2. Mbunge akishachaguliwa awe ni mbunge wa jimbo husika si wa chama husika. Hii itasaidia kuondoa ati Wabunge wa Upinzani etc
3. Kiongozi yeyote akishachaguliwa hata akiondolewa uanachama abaki na ubunge wake
4. Waziri asiwe mbunge

Hili likifanyika unafiki utaondoka na tutakuwa na demokrasia ya kweli
 
demokrasia bila sheria ni vurugu, ndo maana waziri mkuu msitafu alitamka, ukikatazwa jambo ukafanya utapigwa tu, sheria lazima ifuatwe, huwepo wa democrasia sio tija ya kutofuata sheria na taratibu

Hujui unaloongea wewe, unakuta wale walioko madarakani wanataka wanyenyekewe, na wakiambiwa wazo mbadala wanalitafsiri kisiasa. Matokeo yake hayo mawazo yao wanayolazimishia yakikwama tunakuwa tumekwama kama taifa na hatuna la kuwafanya. Acheni kujificha kwenye misemo ya kizee eti demokraisa bila sheria ni vurugu. Ni demokrasia gani mnayotuambia wakati mnaingia mikataba ya kinyonyaji yenye 10% mkiulizwa mnasema siri, watu wakiamua kuhoji baada ya kuchoka mnaleta misemo ya demokrasia bila sheria. Acheni utoto na ubinafsi nyie kwenye nchi yetu.
 
Tukifika mahali tukauponda mfumo tuliouchagua wenyewe, hili litakuwa ni zaidi ya tatizo lenyewe!
Na ndipo watu wengi weupe wanapopata sababu ya kuwadharau utu wetu sisi weusi.
 
Hawatakuelewa, hivi kwa nini hatujiulizi inakuwaje tuna maumbo na sura tofauti. Mola angependa basi wote tungekuwa identical. Yaani kama ni wajinga kwenye issue wote hamchekani. Kwa nini ametuumba tofauti? Kama ametuumba tofauti kwa nini wewe utake wote tuone kitu kwa mtizamo mmoja. Hata huko China ndani ya Communist Party kuna mitifuano hutokea kwa vipindi tofauti. Walituambia elimu bure ni uongo mbona sasa wameelekea huko. Mawazo mbadala ndio msingi wa maendeleo. Hata Mwalimu aliwahi kusema lichama lake likiachwa peke yake litalewa na kusinzia kama poono.

Leo nimemuona mmbunge wa Korogwe vijijini akishauri wapinzani wana role bungeni kwa hiyo mazungumzo yafanywe ili warudi bungeni cha ajabu msomi wao mmoja anataka wapinzani hata mshahara wasipate.
 
Back
Top Bottom