Kama ni wewe utafanyaje?

ooooopsssssssssssssssssssssss! uswazi nooma men.


To Rouette.picha yako ya ID IKO POA.
 
Hivi mnananmbia as if mi sijawahi kukaa uswahilini? I know mtu anaweza kukaa na dignity yake hata katika hali ya umasikini. Hao wa kuazima wanayao tu!
rafiki uswahilini kunatofautiana...... kama ambavyo huko uzunguni kunavyotofautiana, lol!
kuna sehemu kuna maduka ambayo dawa ya kupiga mswaki wanauza kwa kukuminyia kwenye mswaki wako, yaani watu wa hapo hawana uwezo wa kununua hata kale kadawa kadogo sana...... sukari wanapima kwa kijiko, n.k, nk..... siyo kila sehemu inaitwa uswahilini mambo kama haya yapo
 
Kushare ndoo ya kuogea,tena na kuweka chupi mbichi ndani yake!?hayo maUTI,kaswende na ndugu zao wote watawasalimisha kweli?
 
Story za kufikirika hizi. Hivi huyu mdada abebe ndoo kutoka kote alikotoka kwenda kumrudishia mwanaume halafu asingalie ndani kuna nini? Na huyo mwanaume alipokeaje bila ya kuangalia ndani? Kama hili ni kweli, basi ni dhahiri kwamba huyo dada alikuwa anamtega jamaa. So talaka ni haki yake.
 
Duh hii imekaa kushoto vile, huyu msela ana makosa mawili, kosa lake la kwanza ni kumpa mke wa mtu ndoo ya kuogea na kosa la pili ni kusema ingia uchukue.

Kwenye kosa la pili alitakiwa atoe ndoo yenye chupi nje ili yule mke wa mtu aichukue mwenyewe na kuondoka zake.

Nikirudi kwenye mada husika, huyu mke inabidi atoe maelezo ya kina sana juu huo mkasa, haiwezekani uishie hivyo tu kwa maelezo mafupi tu.
Hainingii akilini kwa mwanamke makini kuazima hadi ndoo ya kuogea, tena kwa msela, hapana,lazima kuna kitu zaidi ama kuna kitu kinatafutwa na hata hiyo chupi itakuwa iliachwa for the purpose.

Hilo ni jaribu kama majaribu mengine, shetani kazini kutafuta na kukusanya wafuasi wengi kadri inavyowezekana.
 
Ntamuuliza kulikoni umesahau chumba!
 
Labda sababu chupi itakua mbichi mume anaweza kuelewa
Lakini ndoo nilisahamnunulia ni kwanini anazipasua na kuzitoboa?
sasa na mimi akaniwekee maji kwenye ndoo hiyo hiyo la sivyo chupi akaitupe jalalani maana jamaa simuamini tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…