Kama mnaweza malezi zaeni, vinginevyo acheni………….!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398
Leo ningependa kuwaambia wanawake ambao wanafanya kazi, ambao wameajiriwa katika kazi zinazowaondoa nyumbani asubuhi hadi usiku, huku waume zao nao wakiwa makazini kwa muda kama huo au zaidi. Katika familia hizi, wazazi ni watumishi wa majumbani ambao wengine wanalingana na watoto wa matajiri zao. Unapomuuliza mwanamke huyu kwamba inakuwaje wanazaa watoto na kuwaachia majukumu watumishi majukumu ya kuwalea watoto wao, atakupa majibu ya ajabu sana.

Atakuambia, ‘maisha'. Yaani ni lazima afanye kazi ili aweze kukabiliana na ugumu wa maisha. Mwingine atakwambia anatamani kuacha kazi, lakini akiacha kazi, mumewe anaweza kumbadilikia na kuanza kumnyanyasa. Hayo yote ni majibu yenye makengeza. Ukweli ni kwamba hakuna maisha bora kama kulea mtoto wako mwenyewe ambaye baadae anakuja kuwa mfano wa kuigwa kesho, na kama mume anaweza kumdhalilisha mkewe kwa kuwa hana kazi, basi huyo siyo mume wa kukaa naye hata kama mke huyo ana kazi.

Huenda nikaonekana nawavunja nguvu wanawake wanaofanya kazi lakini huo ndio ukweli. Imebainika kwamba watoto ambao wazazi wao wote wanafanya kazi zinazowafanya kukosekana nyumbani muda mwingi, huwa na nidhamu mbovu sana. Watoto hao huwa na matatizo mengi ya kisakolojia pia kwa sababu ya kukosa mapenzi ya wazazi, kwa sababu ya wazazi kushindwa kujua matatizo yao na kuweza kuwasaidia na kwa sababu ya watoto hao kukosa mifano ya kuiga, hivyo kuiga ya watumishi wa nyumbani na watu wa mitaani . tukumbuke kwamba kila mtoto ana ‘shujaa' wake anayetaka kumuiga na ‘shujaa' wa awali ni mama na baba yake.

Kama mwanamke anaamini kwamba hawezi kuwalea watoto wake mwenyewe, hana muda wa saa nne au tano za kukaa na wanaye kila siku, ya nini azae? Watoto wanahitaji mzazi au wazazi katika muda mwingi wa makuzi yao, labda tu pale ambapo hilo haliwezekani kutokana na sababu zisizoepukika.
 
1st to post, yay!

i have a working mom and i turned fine. get a good housemaid, ask how school was in the evening and be around on weekends

edit:
you can't afford not to work as a woman these days, and malezi is the responsibility of both parents. times have changed and the old gender roles are no longer mutually exclusive
 
Mkuu Mtambuzi, lazima tukubali mfumo wa maisha unapobadilika hata watu waliomo ndani yake hubadilika pia. Kimsingi watu ndio hubadilisha utaratibu wa kuishi kulingana na mahitaji.
 
mtambuzi sio kweli,mimi baba angu aliingia mitini kabisa,na mama yangu,alitulea as a single mum,na tulikuwa 4.akiondoka asubuhi kwenda kazini mpaka usiku,nikienda shule nikirudi ni house girl,namshukuru mungu,sina tabia kama hizo ulizoelezea,nimekua vizuri na namshukuru sana mama kwa uwezo wake mdogo,ila alitulea japo kwa shida,na nimejifunza mengi katika maisha
 
na wanawake wengine,hawa chagui kuishi hayo maisha ya kuwaachia ma house girl,huachwa na waume zao,au waume hufariki,na hata kama mume na mke wakiishi pamoja na kuweka house girl,maisha ya sasa ni magumu,wote mkifanya kazi,mna saidiana katika maisha.mimi sioni vibaya ila wapo wazazi wengine mwanamme akitoka kazini moja kwa moja bar,na mwanamke na yeye akitoka kazini,atakwambia anaenda kwenye maombi,watoto wao waliowazaa wanawasahau kwa kutegemea house girl amalize kila kitu,ukiangalia hapo ni makosa.kuwe na muda wa kukaa na watoto,au wazazi wengine mtoto miaka 5 anapelekwa boarding,nahisi ni kama kukwepa majukumu yako na mtoto wako
 
mtambuzi sio kweli,mimi baba angu aliingia mitini kabisa,na mama yangu,alitulea as a single mum,na tulikuwa 4.akiondoka asubuhi kwenda kazini mpaka usiku,nikienda shule nikirudi ni house girl,namshukuru mungu,sina tabia kama hizo ulizoelezea,nimekua vizuri na namshukuru sana mama kwa uwezo wake mdogo,ila alitulea japo kwa shida,na nimejifunza mengi katika maisha
Kama mwanamke anaamini kwamba hawezi kuwalea watoto wake mwenyewe, hana muda wa saa nne au tano za kukaa na wanaye kila siku, ya nini azae? Watoto wanahitaji mzazi au wazazi katika muda mwingi wa makuzi yao, labda tu pale ambapo hilo haliwezekani kutokana na sababu zisizoepukika.
Soma hapo kwenye RED, nimebainisha kuhusu sababu zisizoweza kuepukika, mama yako alilazimika kuwalea kama alivyowalea kutokana na sababu zisizoweza kuepukika......................
 
mtambuzi nimeamini kweli we babu! yaani kabisa sasa hivi uniweke nyumbani eti nalea! mimi huyuhuyu, na wanaume wenyewe hawahawa! acha bwana liende tu, siachi kazi yangu NG'O!
 
mtambuzi sio kweli,mimi baba angu aliingia mitini kabisa,na mama yangu,alitulea as a single mum,na tulikuwa 4.akiondoka asubuhi kwenda kazini mpaka usiku,nikienda shule nikirudi ni house girl,namshukuru mungu,sina tabia kama hizo ulizoelezea,nimekua vizuri na namshukuru sana mama kwa uwezo wake mdogo,ila alitulea japo kwa shida,na nimejifunza mengi katika maisha

Nimependa kifua chako dear.
 
mtambuzi nimeamini kweli we babu! yaani kabisa sasa hivi uniweke nyumbani eti nalea! mimi huyuhuyu, na wanaume wenyewe hawahawa! acha bwana liende tu, siachi kazi yangu NG'O!
Atakuambia, ‘maisha'. Yaani ni lazima afanye kazi ili aweze kukabiliana na ugumu wa maisha. Mwingine atakwambia anatamani kuacha kazi, lakini akiacha kazi, mumewe anaweza kumbadilikia na kuanza kumnyanyasa. Hayo yote ni majibu yenye makengeza. Ukweli ni kwamba hakuna maisha bora kama kulea mtoto wako mwenyewe ambaye baadae anakuja kuwa mfano wa kuigwa kesho, na kama mume anaweza kumdhalilisha mkewe kwa kuwa hana kazi, basi huyo siyo mume wa kukaa naye hata kama mke huyo ana kazi.

Kwenye RED, nadhani ujumbe umefika..........................!
 
Mtambuzi umenifurahisha,mi naona ungewapigia makofi wapemba maana wao wanajua umuhimu wa mke lol......tuache utani umeongea kitu kizuri lakini kutokana na sababu zisizoweza epukika inabidi tu na wakinamama tuingie makazini kutafuta mkate wa watoto. Hata mm nisingependa mtoto wangu alelewe na house girl sema mazingira hayaruhusu. Inauma sana pale unapomuacha mtoto wa miezi mitatu na dada ni ngumu sana nashukuru sijawahi kuipitia hiyo laaah


bin
 
Last edited by a moderator:
kazi siachi.........
mama yangu alitulea huku akiwa anafanya kazi(ingawa mahousegirl wa enzi zile walikuwa na adabu)
mimi nafanya kazi na kulea watoto...

labda ungewaambia wazazi wahakikishe kila siku wanatenga muda wa kuwa na watoto..
kuwasaidia homework...
kuzungumza nao , kucheza nao na kubond....
nashukuru jumamosi kwangu ni free..
hivyo najitahidi niwe nao kuanzia saa nane mchana hadi jumapili.....

mtoto akuheshimu kama mzazi na akuone kama rafiki wa kukufunulia yote na kukuuliza chochote...

 
Back
Top Bottom