Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Tumemsikia kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum wa Dar, Lazaro Mambosasa akielezea kuwa kutokana na taarifa walizozipata kutoka vyombo vyao vya usalama, wamebaini kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula, alipatikana na sumu mwilini mwake, iliyosababisha aangukuke ghafla kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM na kusababisha akimbizwe hositalini Muhimbili na akaahidi kuwa Jeshi hilo litawasaka kwa nguvu zote, watu wote waliohusika na Uhalifu huo
Tunalipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua ya haraka mno, ya kuwasaka hao watu ambao wanadaiwa walitenda kosa hilo la jinai.
Hata hivyo ninavyofahamu mimi ni kuwa wajibu namba moja wa Jeshi la Polisi nchini, ni kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Ninacholiomba Jeshi hilo la Polisi ni kuwa juhudi hizo wanazozifanya katika kuwasaka watu waliofanya jaribio la kutaka kutoa uhai wa makamu Mwenyekiti wa CCM, Mzee Mangula, juhudi hizo hizo wazifanye kwa waliotaka kutoa uhai wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu, waliofanya jaribio la kutaka kumwua, kwa kumminia risasi 16 kwenye gari lake, ambazo zilimwingia mwilini na hivyo kulazimika kukimbizwa nje ya nchi, ambako anaendelea na matibabu, zaidi ya miaka miwili hivi sasa
Vilevile, ningewaomba Polisi hao wafanye juhudi hizo hizo kwa kuwasaka waliomuua, Mwenyekiti wa Chadema, wa mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo, zaidi ya miaka mitatu hivi sasa.
Jeshi la Polisi halipaswi lifanye ubaguzi katika matukio ya uhalifu nchini, kwa kuangalia ni nani amefanyiwa, kama ni kiongozi wa CCM juhudi kubwa zinafanyika, lakini kama ni kiongozi wa Chadema, haufanyiki uchunguzi wowote!
Tunajua kuwa Jeshi hilo linagharimiwa na walipa kodi wa nchi hii, bila kujali itikadi zao za kisiasa, hasa tukitilia maanani kauli ya mara kwa mara inayotolewa na Rais Magufuli kuwa maendeleo hayana chama.
Tunalipongeza Jeshi la Polisi kwa hatua ya haraka mno, ya kuwasaka hao watu ambao wanadaiwa walitenda kosa hilo la jinai.
Hata hivyo ninavyofahamu mimi ni kuwa wajibu namba moja wa Jeshi la Polisi nchini, ni kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, bila kujali itikadi zao za kisiasa.
Ninacholiomba Jeshi hilo la Polisi ni kuwa juhudi hizo wanazozifanya katika kuwasaka watu waliofanya jaribio la kutaka kutoa uhai wa makamu Mwenyekiti wa CCM, Mzee Mangula, juhudi hizo hizo wazifanye kwa waliotaka kutoa uhai wa aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki, Tundu Lissu, waliofanya jaribio la kutaka kumwua, kwa kumminia risasi 16 kwenye gari lake, ambazo zilimwingia mwilini na hivyo kulazimika kukimbizwa nje ya nchi, ambako anaendelea na matibabu, zaidi ya miaka miwili hivi sasa
Vilevile, ningewaomba Polisi hao wafanye juhudi hizo hizo kwa kuwasaka waliomuua, Mwenyekiti wa Chadema, wa mkoa wa Geita, Alphonce Mawazo, zaidi ya miaka mitatu hivi sasa.
Jeshi la Polisi halipaswi lifanye ubaguzi katika matukio ya uhalifu nchini, kwa kuangalia ni nani amefanyiwa, kama ni kiongozi wa CCM juhudi kubwa zinafanyika, lakini kama ni kiongozi wa Chadema, haufanyiki uchunguzi wowote!
Tunajua kuwa Jeshi hilo linagharimiwa na walipa kodi wa nchi hii, bila kujali itikadi zao za kisiasa, hasa tukitilia maanani kauli ya mara kwa mara inayotolewa na Rais Magufuli kuwa maendeleo hayana chama.