nimie
JF-Expert Member
- Sep 9, 2011
- 525
- 104
Nikiwa safarini hivi majuzi nimesikia kupitia BBC kuwa mkenya mmoja aishiye London Uingereza amehukumiwa kwa kumbaka mkewe. Kisa, alifanya naye mapenzi bila ridhaa ya huyo mkewe. Nikawambia wenzangu ktk hali ya kulijadili suala hili. Ndipo mmoja akasema kama mambo yenyewe ndio hivyo, basi wabongo wengi wanandoa huwa wanawabaka wake zao mara kibao!