Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.Ila Pasco Mungu hatukubalii kukaa tu tuombe bila ya kuitafuta haki yako, Hata kama mtu unamdai unaambiwa umwambie na umkumbushe Mara kadhaa deni lako.
Maombi yawepo na haki itafutwe kama ukiamini umedhulumiwa, zipo njia nyingi zenye kheri za kutafuta haki na uziepuke zenye shari
Mungu ndio msemaji wa mwisho ...tutafunga kwa maombi na sadaka tutatoa Mungu akapate kujidhihirisha
Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.
Pasco
Hivi inaingia akilini mtu awe anahutubia mikutano ya kampeni kwa dakika 4 halafu aseme ameibiwa kura! is it logic kweli, tufikie mahali tuwe wakweli tu
Mkuu KipimaPembe, kwanza asante kwa objectivity kwenye bandiko lako hili. Nimependa zaidi mstari huu,Hapa ndo udhaifu wa mwafrika ulipo. Hatukubali matokeo. Tunatafuta kila sababu ili tu tuonekane tumeonewa ili tuwaridhishe washabiki wetu.
Washabiki wote wa Lowasa lazima wawe wakweli na mmwambie ukweli Edward Lowasa kuwa Kura hazijatosha. Hizo kura million 10 anazosema amepata wekeni tu mfano wa majimbo matano ya kuonesha tofauti ya kura zilizohesabiwa na kusainiwa majimboni na zile zilizosomwa na tume ya Uchaguzi.
Wakati matokeo ya Ubunge majimboni yakisomwa hakuna hata mmoja aliyekuja na mfano hata mmoja. Zimekuwa zikitengenezwa tofauti za kuumba (Tunduma na Bumbuli) ambazo zote zimekuwa debunked na rekodi sahihi za tume na majimboni.
Kama EDO anajua kuna wizi na anajua ulivyofanyika; aje na mifano ya rekodi, siyo sweeping statements kwamba alipata kura million 10. Kampeni za mijini tu kwenye wapiga kura 30% na kununua media (TV na Magazeti) haitoshi. Unahitaji wapiganaji on the ground. Hakuna vita ambayo imeshawahi kushindwa kwa kutumia air power na pyschological warfare peke yake. You need ground solders. Hao maeneo mengi ya nchi hawakuwepo; ukiachana na mikoa miwili ya Arusha na Kilimanjaro pekee.
Edo is dangerously polarizing na hilo ni mojawapo ya matatizo yake makubwa. Wakati ana win hardcore supporters, methods zake vile vile zinafanya apate hardcore opponents. Si mkusanyaji, ni mtawanyaji. Challenge ya kwanza kuunganisha Upinzani alishindwa and he nearly killed Ukawa.
Magufuli hakuhitaji wizi wa kura kushinda huu uchaguzi, wala CCM haikuhitaji wizi wa kura kushinda majimbo mengi. Walichohitaji ni Ukawa iliyokosa mwelekeo. Hakuna mtu hata mmoja aliyeweza kusimamia hoja ya katiba ya warioba na kuielezea vizuri. Hiyo inaonesha kwamba, kampeni ya Edo ilijaa wadandiaji, si watu original waliokuwa wakijua Ukawa inasimamia nini. Matokeo yake walipoteza mwelekeo wakafanya kampeni ya kutoa ahadi; kampeni ambayo haikuwatofautisha na CCM. Wananchi wengi wanajua kuwa hizo ahadi ni uongo na nyingi hazitekelezeki.
Wananchi walitaka kusikia alternative thinking. Edo alitegemea Mbowe, Sumaye na Kingunge kuwa ndo wasemaji wakuu. Ni vigumu sana kuwashawishi watanzania wengi kuwa Sumaye na Kingunge ni watu tofauti na wale waliokuwa CCM. Mbowe watanzania walishamkataa mwaka 2005.
Tulitarajia Lowassa aongozane na Kina Lissu, Mnyika, Mwalim, Lema, Mdee ili kuwaonesha wanachadema wa siku zote kuwa Lowasa ni Chadema. Hilo halikutokea. Watu hao wote walijichimbia majimboni kwao kupigania uhai wao Bungeni.
Kwa kufanya uchambuzi makini usio na chembe ya unafiki, ni wazi hizo kura million 10 anazodai kuzipata Edo ni za kupikwa na washabiki wake wanaotaka kuendelea kufaidi mfuko wake.
Ataheshimika sana hata akikaa kimya tu. Kura milioni kumi akiulizwa ushahidi uko wapi itakuwa kichekesho!
na hapa ndipo mahali pekee, kama kuna wizi ulifanyika, ndipo karma ita strike!.Magufuli hakuhitaji wizi wa kura kushinda huu uchaguzi, wala CCM haikuhitaji wizi wa kura kushinda majimbo mengi.
Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.
Pasco
Mkuu The Boss, you have the powers, usijiogope bali jitumie!. Hili la majina nawaachia watu wa numerology, tena sio majina tuu hara vibrations za rhymes, John Pombe, Joseph Magufuli yenye herufi zinazojirudia mara mbili mbili, angalia jina hili John Pombe, Joseph Magufuli, lina herufi hizi JJ, EE, HH, MM, PP, OO na UU na jina la Samia Suluhu Hassan lenye SSSS, AAAA, UUU, sio bure!.Pasco nimeanza kujiogopa aisee
nilisema lazima Pasco atazungumzia karma....nikawa naingia JF nitazame thread gani utaanzisha
halafu nakuta kweli umeanzisha thread kuhusu Karma....nimejiogopa mkuu..
Kwa kuongeza mkuu Pasco.....nimejiuliza ni bahati mbaya makamu mteule anaitwa Suluhu?
tazama hilo jina.....vowels zinajirudia kama Nyerere Kawawa Makamba Jakaya...nafikiri umeelewa kitu hapo..
Yaani adi natamani ningekuwa kwenye kitutuli nikiona unaweka tiki kwa rangi ya majani nakutia bonge la kofi kuanzia wew adi kitutuli mnaenda chini alafu nawaambia walio kwenye msitari mwingine aje afanye upumbavu aone .... Maana watu wengi wana kufa kisa hakuna huduma bora za afya alaf wew unayeweka tiki una ndugu na jamaa zako kibao wako mtaani hawana ajira na ata ada ni shiiida alafu ulikuwa mmoja wa watu uliye lalamika kuhusu Escro, Epa na mengi neyo then leo unafanya upumbavu na ulofa nakwambia ilo kofi lingekupa akili na ulofa na upumbavu wako ungekutoka... Embu ninyamaze nisije kulia bure
Huo wizi umefanyika wap wakat kila jimbo palkuwa na wakala na amesain matokeo ndo yakatumwa NeC? Hahah Fisad papa waTanzaniia tumemkata tena, akagombee uraisi Zanzbar au Fifa anaweza shinda
anatangazwa mshind siku hyo hyo anaadhimisha siku yake ya Kuzaliwa hajaona tu kuw huyu ndiye chaguo la Mungu
Ndio maana ombi la Lowassa kwa tume siku zote limekuwa kuhesabu kura kwa kutumia karatasi za kura zilizosainiwa na mawakala vituoni. Kura zilizotangazwa na NEC zimetoka kwa vijana wa CCM pale Kempinski hotel na hazifanani na kura halisi.