Elections 2015 Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali Yetu ni Serikali Dhalimu?, Haramu?. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!

Edward Lowassa ni nani?

Wewe Pasco nnakusihi kaa kimya na ukubali matokeo.

Amini.

Unajua bwana watu tuliomba makanisani na misikitini,na tunaamini kiongozi yeyote anatoka kwa MUNGU na kwa makusudi mazima kwa watu wake.hvyo basi mimi binafsi naamini kua MAGUFULI ni chaguo la MUNGU na waliompigia kura hawajakosea,by the way ni watu tu kujaribu kupotezea lakini wanajua MAGUFULI ni mtu gani,tukiachana na madhaifu ya kibinadamu lakini ndo wazili pekee ambae tumekua tunaona hajawah kufeli ktk kazi,na huyu wa upande wa pili ndiye mtu ambae alihubiliwa na hawa hawa walokua wanamnadi kua alikua fisadi na hafai kua kiongozi,leo wamekuja nae kusema anatufaa sana,tunamheshimu sana huyo mzee lakini kuna mambo juu yake na walokua wakimnadi ambayo hayahitaji degree kupambanua mambo! MUNGU IBARIKI TANZANIA YANGU.
 
Last edited by a moderator:
Ila Pasco Mungu hatukubalii kukaa tu tuombe bila ya kuitafuta haki yako, Hata kama mtu unamdai unaambiwa umwambie na umkumbushe Mara kadhaa deni lako.

Maombi yawepo na haki itafutwe kama ukiamini umedhulumiwa, zipo njia nyingi zenye kheri za kutafuta haki na uziepuke zenye shari
Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.

Pasco


 
Mungu ndio msemaji wa mwisho ...tutafunga kwa maombi na sadaka tutatoa Mungu akapate kujidhihirisha

Nani unayemfungia na kumwombea huyo kwenye picha? Mzee wa michanganyo? Usipoteze muda kale ulale

LOWASA.jpg
 
Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.

Pasco



Sasa nikukumbushe kitendo alichokifanya huyu kiongozi cha kuiacha Ccm kwa Mara ya Kwanza katika historia ya siasa za Tanzania alikua ni yeye, je huoni pia kama kwa Mara ya kwanza tena akaweza pia kuyafanya hayo unayoyasema hayawezekani yena kubadilishwa? Kitendo kile kila mmoja kilimshangaza sana na mimi sikuwahi kuzitegemea siasa zetu kuwa zingelifikia kiwango kile.

Ni kwambie tu kwa Mungu tunaona,na tutaona maajabu mengi sana ya kawaida na yasio ya kawaida.. Kwa kupitia jitihada zake yeye kama Mungu yuko nae anaweza akaleta mabadiliko makubwa na akaiandikia tena historia nyingine nchi hii.

Mimi nionavo ni mapema sana kumwambia akachunge ngombe kwanza Tumuache atafakari cha kufanya na sisi tumejifunza mengi kupitia kwake na pengine tutazidi kujifunza kuliko tukimuacha akenda akafuga ngombe.

Ahsante
 
Hivi inaingia akilini mtu awe anahutubia mikutano ya kampeni kwa dakika 4 halafu aseme ameibiwa kura! is it logic kweli, tufikie mahali tuwe wakweli tu

ni sheria ipi inayosema mgombea urais lazima ahutubie kwa masaa matatu?!
mbona wote mnaoitetea ccm humu jf mna akili fupi sana?!
 
Hapa ndo udhaifu wa mwafrika ulipo. Hatukubali matokeo. Tunatafuta kila sababu ili tu tuonekane tumeonewa ili tuwaridhishe washabiki wetu.

Washabiki wote wa Lowasa lazima wawe wakweli na mmwambie ukweli Edward Lowasa kuwa Kura hazijatosha. Hizo kura million 10 anazosema amepata wekeni tu mfano wa majimbo matano ya kuonesha tofauti ya kura zilizohesabiwa na kusainiwa majimboni na zile zilizosomwa na tume ya Uchaguzi.

Wakati matokeo ya Ubunge majimboni yakisomwa hakuna hata mmoja aliyekuja na mfano hata mmoja. Zimekuwa zikitengenezwa tofauti za kuumba (Tunduma na Bumbuli) ambazo zote zimekuwa debunked na rekodi sahihi za tume na majimboni.

Kama EDO anajua kuna wizi na anajua ulivyofanyika; aje na mifano ya rekodi, siyo sweeping statements kwamba alipata kura million 10. Kampeni za mijini tu kwenye wapiga kura 30% na kununua media (TV na Magazeti) haitoshi. Unahitaji wapiganaji on the ground. Hakuna vita ambayo imeshawahi kushindwa kwa kutumia air power na pyschological warfare peke yake. You need ground solders. Hao maeneo mengi ya nchi hawakuwepo; ukiachana na mikoa miwili ya Arusha na Kilimanjaro pekee.

Edo is dangerously polarizing na hilo ni mojawapo ya matatizo yake makubwa. Wakati ana win hardcore supporters, methods zake vile vile zinafanya apate hardcore opponents. Si mkusanyaji, ni mtawanyaji. Challenge ya kwanza kuunganisha Upinzani alishindwa and he nearly killed Ukawa.

Magufuli hakuhitaji wizi wa kura kushinda huu uchaguzi, wala CCM haikuhitaji wizi wa kura kushinda majimbo mengi. Walichohitaji ni Ukawa iliyokosa mwelekeo. Hakuna mtu hata mmoja aliyeweza kusimamia hoja ya katiba ya warioba na kuielezea vizuri. Hiyo inaonesha kwamba, kampeni ya Edo ilijaa wadandiaji, si watu original waliokuwa wakijua Ukawa inasimamia nini. Matokeo yake walipoteza mwelekeo wakafanya kampeni ya kutoa ahadi; kampeni ambayo haikuwatofautisha na CCM. Wananchi wengi wanajua kuwa hizo ahadi ni uongo na nyingi hazitekelezeki.

Wananchi walitaka kusikia alternative thinking. Edo alitegemea Mbowe, Sumaye na Kingunge kuwa ndo wasemaji wakuu. Ni vigumu sana kuwashawishi watanzania wengi kuwa Sumaye na Kingunge ni watu tofauti na wale waliokuwa CCM. Mbowe watanzania walishamkataa mwaka 2005.

Tulitarajia Lowassa aongozane na Kina Lissu, Mnyika, Mwalim, Lema, Mdee ili kuwaonesha wanachadema wa siku zote kuwa Lowasa ni Chadema. Hilo halikutokea. Watu hao wote walijichimbia majimboni kwao kupigania uhai wao Bungeni.

Kwa kufanya uchambuzi makini usio na chembe ya unafiki, ni wazi hizo kura million 10 anazodai kuzipata Edo ni za kupikwa na washabiki wake wanaotaka kuendelea kufaidi mfuko wake.

Ataheshimika sana hata akikaa kimya tu. Kura milioni kumi akiulizwa ushahidi uko wapi itakuwa kichekesho!
Mkuu KipimaPembe, kwanza asante kwa objectivity kwenye bandiko lako hili. Nimependa zaidi mstari huu,
Magufuli hakuhitaji wizi wa kura kushinda huu uchaguzi, wala CCM haikuhitaji wizi wa kura kushinda majimbo mengi.
na hapa ndipo mahali pekee, kama kuna wizi ulifanyika, ndipo karma ita strike!.

Naungana na wewe sio tuu kuwa Magufuli hakuhitaji kuiba kura kumshinda Lowassa, kwa sababu in reality Magufuli ni mzuri kushinda Lowassa na hili nililisema kabla hata Magufuli hajateuliwa na CCM, nilieleza humu kuna 'sababu fulani' lazima awe Magufuli, nilizieleza humu!
[h=3]Mgombea wa Urais Kwa tiketi ya CCM, 2015 "Could Be" John [/h] ile day 1 tuu Magufuli amepitishwa pia nikatoa ushauri huu kwa Lowassa
[h=3]Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, [/h]Hivyo hakuhitaji kuiba kura kushinda, ila ilifika mahali CCM wakatambua kuwa Lowassa ana mvuto wa ajabu wa kupendwa na watu [h=3]Hii 'Vox Populi' ni 'Vox Dei' Kuhusu 'Jiwe Walilolikataa Waashi .
[/h]for a reason or no apparent reasons at all ila anapendwa na ana mvuto!, hivyo wangejiachia tuu kuiacha nature itoe ushindi, kulikuwa na hatari ya kushindwa na ndipo wakapanga mambo yao!. Haiwezekani kabisa, kama kila kituo kila mpiga kura alipiga kura tatu, haiwezekani jumla ya matokeo ya udiwani, ubunge na urais yatofautiane kwa sababu every vote was casted and caunted!. Jazia jazia kubwa imefanyika kwenye kura za ubunge na rais!. Kule wapinzani walikotangazwa washindi, ujue the gap was too wide to bridge!. Ila mimi jiliwashauri sana hawa jamaa zangu to ivest on numbers because numbers dont lie!.
[h=3]Kuelekea 2015: CHADEMA, Don't Miss the Target,
[/h]they missed the target!.

Pasco


 
Pasco,
Does it mean kwamba kila jimbo CCM waliiba? Kila kata CCM waliiba? zile ambazo hawakuiba basi upinzani ulishinda? I doubt kama wengi tunaoleta hayo madai ya wizi tulikuwa na contact zozote on the ground.

Nina ndugu yangu aligombea udiwani kupitia Chadema alishindwa na anakiri alishindwa kihalali! Lazima tujue kuwa huku kupendwa kwa Edo hakukuwa perfect jamani. Tuwe wakweli. Kama kupendwa kama kampeni yake mlivyokuwa mnamchora ni kweli alikuwa anapendwa; lakini kwamba alikuwa anapendwa perfectly na kila mtu?? That's delussional!
 
Mkuu Mgeni wa Mungu, sisi Watanzania tuna tatizo kubwa sana la upungufu wa elimu ya uraia na elimu ya haki zetu za msingi!. Kwa mujibu wa katiba hii iliyopo, matokeo ya urais yakiishatangazwa na NEC, ndio the end of the world!. Hakuna mamlaka yoyote duniani au mbinguni inaweza kubadilisha kitu!, ndio maana nimemshauri Lowassa ajirudie zake tuu kijini kwake akajichungie ngombe wake kama alivyoahidi, there is nothing more one can do!.

Pasco



Uko sawa kabisa na "AKIKAIDI"......Halafu hawa kina Mbowe akili ndogo sana yaani wanaleta vijana wa IT kutoka sijui Korea halafu wanaona kama watafanikiwa lengo lao kabisaa.Tanzania siyo Somalia
 
Pasco nimeanza kujiogopa aisee
nilisema lazima Pasco atazungumzia karma....nikawa naingia JF nitazame thread gani utaanzisha
halafu nakuta kweli umeanzisha thread kuhusu Karma....nimejiogopa mkuu..

Kwa kuongeza mkuu Pasco.....nimejiuliza ni bahati mbaya makamu mteule anaitwa Suluhu?
tazama hilo jina.....vowels zinajirudia kama Nyerere Kawawa Makamba Jakaya...nafikiri umeelewa kitu hapo..
Mkuu The Boss, you have the powers, usijiogope bali jitumie!. Hili la majina nawaachia watu wa numerology, tena sio majina tuu hara vibrations za rhymes, John Pombe, Joseph Magufuli yenye herufi zinazojirudia mara mbili mbili, angalia jina hili John Pombe, Joseph Magufuli, lina herufi hizi JJ, EE, HH, MM, PP, OO na UU na jina la Samia Suluhu Hassan lenye SSSS, AAAA, UUU, sio bure!.

Hata ile kushinda tuu siku yake ya kuzaliwa it is not nothing!, kwenye mambo haya hakuna coincidence, kila jambo ni pre meditated move!, hivyo hawakuhitaji kabisa kuiba kura!.

Pasco

 
Yaani adi natamani ningekuwa kwenye kitutuli nikiona unaweka tiki kwa rangi ya majani nakutia bonge la kofi kuanzia wew adi kitutuli mnaenda chini alafu nawaambia walio kwenye msitari mwingine aje afanye upumbavu aone .... Maana watu wengi wana kufa kisa hakuna huduma bora za afya alaf wew unayeweka tiki una ndugu na jamaa zako kibao wako mtaani hawana ajira na ata ada ni shiiida alafu ulikuwa mmoja wa watu uliye lalamika kuhusu Escro, Epa na mengi neyo then leo unafanya upumbavu na ulofa nakwambia ilo kofi lingekupa akili na ulofa na upumbavu wako ungekutoka... Embu ninyamaze nisije kulia bure

Ndugu inaonekana hujui maana ya democrasia. Km unadhani mawazo yako ni bora kuliko ya watanzania walio baki basi una tatizo.
Waache na wengine watumie uhuru wao km EL alivyotumia Uhuru wake kuja CDM kutuchafulia chaka chetu
 
Huo wizi umefanyika wap wakat kila jimbo palkuwa na wakala na amesain matokeo ndo yakatumwa NeC? Hahah Fisad papa waTanzaniia tumemkata tena, akagombee uraisi Zanzbar au Fifa anaweza shinda

Ndio maana ombi la Lowassa kwa tume siku zote limekuwa kuhesabu kura kwa kutumia karatasi za kura zilizosainiwa na mawakala vituoni. Kura zilizotangazwa na NEC zimetoka kwa vijana wa CCM pale Kempinski hotel na hazifanani na kura halisi.
 
Watanzania tumeikataa UKAWA KUANZIA madiwani,wabunge na Rais.pia tumefahamu wazi wazi kwamba UKAWA ilikuwa na mamluki KUTOKA nje kuwasaidia kampeni..kwa hali UKAWA isahau kuongoza tz
 
anatangazwa mshind siku hyo hyo anaadhimisha siku yake ya Kuzaliwa hajaona tu kuw huyu ndiye chaguo la Mungu


That was planned not Coincidence. Kama ni chaguo la Mungu its a matter of time kama Mungu atasimamia utawala wake tutajua. Sitaki kuzungumzia habari za Mfalme Belshaza lakini naziona dalili kuwa Magufuli is destined to be Belshaza of our time.
 
Ndio maana ombi la Lowassa kwa tume siku zote limekuwa kuhesabu kura kwa kutumia karatasi za kura zilizosainiwa na mawakala vituoni. Kura zilizotangazwa na NEC zimetoka kwa vijana wa CCM pale Kempinski hotel na hazifanani na kura halisi.

Unaweza kutoa uthibitisho hadharani?
 
Nahisi wale mamluki walishauri hivi@
1) kamata vyombo habari na NGOs mapema
2)ponda media na NGOs zisizokukubali
3)waahidi wenye changamoto kila kitu duniani-bodaboda, mama ntilie
3)usijibu hoja nzito.jidai unaonewa
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom