KALI LINUX the best OS ever seen

Mimi napendekeza iwepo Official Thread ya Linux ili mtu atakayetaka kujua kitu chochote kuhusu Linux anakwenda huko. Watu wengi wanasema OS za Linux ni ngumu, hii inatokana na ufahamu mdogo kuhusu Linux.

Mkuu wazo zuri sana hilo,mm nimeshatumia linux mint,ubuntu,backtrack na kali linux nimeidownload juzi ila bado sijaitumia
 
Mkuu wazo zuri sana hilo,mm nimeshatumia linux mint,ubuntu,backtrack na kali linux nimeidownload juzi ila bado sijaitumia

Uko wapi mkuu, mim naitaji iyo image yake hii yangu ni bad image so ninaitumia ku boot from flash (live CD). Nataka ni install permanent

Niko Dar
 

Apo mkuu naomba unielekeze kati ya hii KDE na Gnome? Na ipi nzuri?
 
Mkuu wazo zuri sana hilo,mm nimeshatumia linux mint,ubuntu,backtrack na kali linux nimeidownload juzi ila bado sijaitumia

Leo nimeipata Mint lakini zaidi naitaka SUSE, nimejaribu kudownload lakini sikufanikiwa maana image yake ni kubwa, speed ya internet ilikuwa ndogo.
 
Hivi SUSE ni nzuri KULIKO Mint au, leo nimefownload SUSE? Hebu nijuzeni
 

Tatizo kubwa ni wewe unaitumia kwa kazi gani. Kuna mazingira hayakuruhusu kutumia os nyingine zaidi ya windows os kutokana software unazotumia katika kazi yako. Mimi binafsi nimeshindwa kuhama windows kutokana na application za kazi yangu zote ni windows only.
 

Ni kweli Mkuu, ila ninachokiona ni kuwa Linux wamelenga kuwasaidia watu kwa kuwa hizi program za kununua kama za Microsoft ni ghali sana. Fikiria Windows 7 Professional ni usd 375, na Office ni usd 200, ni Wabongo wangapi wanaweza kumudu hizo gharama? Na ndiyo maana watu wengi wanatumia program za Kudurufu kuanzia OS, Office na nyinginezo. Kwa mfano Linux OS naipata bure pia package ya office inakuwa imeambatanishwa japo siyo kama ile ya Microsoft lakini vitu muhimu vyote vipo, sasa kwa nini nisitumie Linux kama shughuli zangu ni za kawaida?
 
Leo nimeipata Mint lakini zaidi naitaka SUSE, nimejaribu kudownload lakini sikufanikiwa maana image yake ni kubwa, speed ya internet ilikuwa ndogo.

kweli kabisa kaka microsoft ni ghali sana. Kama sio mambo ya piracy wengi tusingeimudu. Mimi huwa nina deal na cash registers na efd kwa ujumla. Sasa software zote zinazotumika katika maintenance ya hizi devices ni windows based. Yaani kama leo nitaweka linux basi kesho sitafanya chochote kazini zaidi ya ku browse.



 
Mkuu mfano ni kazi gani huwezi kufanya kwenye OS nyingine
 
Mkuu mfano ni kazi gani huwezi kufanya kwenye OS nyingine

Kiufupi sio kazi ila ni program tunazotumia kutoka kwa vendor wa printers na devices zingine zote ni za windows only. Applications zote kama vile printer flasher, loader na programing utilities zingine ni windows based
 

Kama inakulazimu basi huna namna ya kufanya.
 
Kiufupi sio kazi ila ni program tunazotumia kutoka kwa vendor wa printers na devices zingine zote ni za windows only. Applications zote kama vile printer flasher, loader na programing utilities zingine ni windows based

Nakubaliana na wew mkuu, bilashaka kwa organisation za hapa Tz kutumia linux Os bado sana mana ving wanafnya kwa sharing n wengi wa wafanyakazi hawako educated sana na linux, itawasumbua
 
Duh, waswahili kwa kujisifu!! Mambo gani ya ajabu ajabu unayofanyia? hebu yaeleze hayo mambo tushangae.
 
Apo mkuu naomba unielekeze kati ya hii KDE na Gnome? Na ipi nzuri?








hapo inategemea na wewe mwenyewe kama unapenda windows like na more customization chagua kde ila kama unataka different appearance na simpicity gnome iko poa

Sent from my Nokia Lumia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…