Kakobe apinga waraka wa wakatoliki

kwanza kakobe ni darasa la ngapi mpaka akosoe waraka ulioandaliwa na wataalam waliobobea?

Nakumbuka wakati anauza kanda za nyimbo pale temeke, sijui kama alienda shule zaidi.


Ha ha ha..kwenye post ya 44 hapa, jamaa ananukuliwa akisema kuwa jamaa alikuwa anaiba nyimbo za watu anazidurufu na kujipatia rizq.. hii ndio bongo zaidi ya uijuayo.

Kaaaz kwerkwer
 
Nyaraka za dini haziwezi kuwagawa wa Tanzania ila Ufisadi Utawagawanya.

Why?

Katika mijadala hii Wakristo hawajakaa kama kundi moja kupinga Kundi lingine lisilo la Wakristo... na wala haieelekei kuwa hivyo.

The same Kwa waislam na wasio na dini.

Nyaraka hazijajadiliwa kwa mtindo wa Kushabikia dini na wala sioni ikiwa hivyo.

Wajadili Nyaraka Wanaijadilili kama Wa Tanzania....

Na Hakuna cha kuogopa hapa.
 
Ni kweli kabisaa, kakobe kaongea point. Namuunga mkono. Kuna watu waoga sana kukemea jambo hili waziwazi.
 
Kakobe nae ameamua tuu kujilipua nae aonekana yupo Tz,otherwise ata aingecomment tungemtambua tuu!
 
alipokosa dili la kuuza kanda za ASSMBLESS OF GOD KARIAKOO ndio akaamua kujitoa na kuanzisha DHEHEBU lake linalokataliwa na Viongozi wengine wa dini

Tangu siku nyingi nilifahamu kuwa huyu jamaa ni KIBAKA.

Nilishamuona kwenye TV akiombea akina mama eti maziwa yatoke. Na mshe*** huyu bila aibu akawa akiwashika akina mama matiti na kuyakamua na kuonyesha eti maziwa yanatoke. Angelikuwa mke wangu, ningelimshataki kwa kusoa hilo. Utashikaje HOTELI ya watoto wangu?
 
ahhahahhahahhaha!! duh!! makubwa1
 
Sidhani kama Pengo ana sababu ya kujibizana na Kakobe aliyejipachika uaskofu. Kwanza hana upeo wowote wa kuelewa mambo. Ni kichaa tu anayeweza kusimama na kuupinga ule waraka murua wa Kanisa Katoliki. Vichaa wengine walishajitokeza mwanzo, na sasa wanazidi kujitokeza.
 
Ni kweli kabisaa, kakobe kaongea point. Namuunga mkono. Kuna watu waoga sana kukemea jambo hili waziwazi.

wewe uliyoona point ni ipi mbali ya yeye kubwabwaja tu. Si ajabu wewe ni miongoni mwa wanaoenda pale kuabudu na mnaambiwa kuwa na dhahabu ni dhambi, mnampatia yeye anauza anasomesha watoto wake nje ya afrika. poleni sana waathirika
 
Huyu ni kiongozi wa dini ambaye kipindi fulani alidai mgombea mmoja wa urais alikuwa ni chaguo la mungu lakini Mungu wa ukweli alimuumbua kwa kufanya ndivyo sivyo.

Maraka hauna tatizo na hata wanaoukosoa hawakosei ni kama kudhani kwa mawingu kufurika basi jua halipo
 
alipokosa dili la kuuza kanda za ASSMBLESS OF GOD KARIAKOO ndio akaamua kujitoa na kuanzisha DHEHEBU lake linalokataliwa na Viongozi wengine wa dini

Alikuwa anauza kanda za nyimbo za miziki ya kidunia - Casba recordings... "edition mulenga"....
alibadili upepo wa biashara maana tusisahau kuwa dini nayo imo katika makundi ya biashara siku hizi.... ukiachilia mbali dini/madhehebu kongwe.
 
Mi nadhani Kakobe ameshindwa kuelewa kwamba si kazi ya serikali kuhubiri injili. Hiki ndicho kile alichokuwa akikisema Pengo. Halafu Waislamu nawashangaa sana wanaposema wanaonewa, Rais ni Mwislamu, Makamu wake ni Mwislamu, Rais wa Zanzibar ni Mwislamu hata Katibu na mwenyekiti wa CCM ni waislamu, sasa wanaonewa vipi? Sielewi. Kwa heshima zote, waislamu mnisaidie maana nauliza kwa uzuri tu, sina ubaya na nyinyi, naomba msaada wenu na si kashfa!
 
Huyu kikobe hana adabu tu hivi hajawasikia wakatoliki hivi majuzi walipo iambia serekali kuwa hakuna mwenye uwezo wa kuwakataza wakatoliki wasiandike waraka, sasa kikobe jeuri yake kaitowa wapi ?
 

nimekupata mkuu. waraka unaelimisha tu jinsi ya kupata viongozi bora. hauwezi kuwagawa watu, hizo ni mbinu tu za kuficha ukweli na kuendelea kuwabeba mafisadi

huenda KAKOBE kanunuliwa, anapenda sana hela yule
 
nimekupata mkuu. waraka unaelimisha tu jinsi ya kupata viongozi bora. hauwezi kuwagawa watu, hizo ni mbinu tu za kuficha ukweli na kuendelea kuwabeba mafisadi

huenda KAKOBE kanunuliwa, anapenda sana hela yule

Siku hizi mtu yeyote akiwa na position tofauti na yako basi "kanunuliwa" au "fisadi"

Before getting on Kingunge's dyck hapo juu, Kakobe alikuwa ana echo sentiments nilizokwishawahi kuzitoa humu ndani.
 
.

Naomba sana umtake radhi Askofu Kakobe. Kwani Pengo kapewa ukadinari na nani miongoni mwa watanzania anaoshiriki nao kila siku?
 
Kuna nyeti kuwa huyu bwana Kakobe ni msilamu, na jina lake ni Zahoro. Hivyo sistushwi saaana na sarakasi zake. Tutegemee kuona mengi kabla ya 2010.


Pili, kakobe anajulikana, wala watu wenye akili zao hawawezi kupoteza muda kumsikiliza. Ndo maana anamsifia Kingunge. Ni opportunist tu hana lolote, anatafuta attention

alipokosa dili la kuuza kanda za ASSMBLESS OF GOD KARIAKOO ndio akaamua kujitoa na kuanzisha DHEHEBU lake linalokataliwa na Viongozi wengine wa dini


Sasa ndio naamini WAKATOLIKI NI MABINGWA WA MATUSI.

WAKATOLIKI: sasa KKKT wanakuja na waraka wao na vile vile Anglican wanakuja na wakwao. Kakobe, Mama Rwekatare na Wasabato wanajipanga kuja na waraka zao.

Sasa wananchi wa tanzania atakuwaje. hebu acheni kutoa kashfa kwani kila mtu ana haki ya kuujadili na kuupinga au kuukubali waraka huo wa wakatoliki. Kwani hayo sio maneno toka kwa Mungu. Hayo ni Maneno ya Pengo na kabineti yake kwa kuridhiwa na Papa kwa waumini wao na wala si kila mtanzania.

Wakatoliki mlilelea vibaya na kudekezwa na JK Nyerere sasa mnakiona cha moto.
Lazima mjue ninyi ni chini ya 20% ya wananchi wote wa Tanzania, sasa hamuwezi kuwaburuza 80% ambao ni majority ingawa bungeni mpo zaidi ya 70% ya wabunge wote.

Agenda zenu za siri zimebaininika , mngoje sasa kupungua kwa idadi yenu bungeni.
 
.

Barubaru.Tatizo naona ni kwasababu Waraka wametoa Wakatoliki.Hata Kakobe anajua kuwa Waraka wake hauwezi leta tofauti. WaTZ na hata Mafisadi wasingejali/wasingeshughulika. Malumbano yanavyoendelea inakula upande wa Ufisadi na chama tawala.ngoja tuone muda utasema.
 
hana jipya,awaombe radhi watz kwa kuwadanganya kuwa mrema alikuwa chaguo wa mungu wakati alikuja kubwagwa vibaya.Inawezekana kweli wanaosema kakobe hahubiri kuhusu mungu wa kweli bali kuna mungu wake ambae ndie alimuahidi kuwa mrema ni chaguo lake mungu.
''Nao watakuja kwa jina langu wakiamuru hata moto kushuka toka juu na watafanya maajabu kwa jina langu lakini msiwaamini''
Yu wapi mungu wa kakobe?
 
askofu kakaobe fisadi mkubwa anawakwangua waaamini wake sadaka kama nini hana lolote huyu mnafiki na kigeu geu si amewahi kumpigia kampeni mrema huyu sasa yeye hakuchanganya siasa na dini kipindi hicho? mwehu tu
 
askofu kakaobe fisadi mkubwa anawakwangua waaamini wake sadaka kama nini hana lolote huyu mnafiki na kigeu geu si amewahi kumpigia kampeni mrema huyu sasa yeye hakuchanganya siasa na dini kipindi hicho? mwehu tu

Mie Binafsi nawapenda sana mch Mtikila, Dr Slaa na Askofu kakobe na Mama Rwekatare.

Mtikila, Mama Rwekatare na Dr Slaa hao ni viongozi wakubwa a kidini lakini wapo wazi sana na wanaingia wenyewe kwenye siasa na ni wana siasa.

Nampenda sana Kakobe kwa kujitowa waziwazi na kumpigia mgombea kampeni na kutumia nafasi yake kikatiba.

Najiuliza Hivi Pengo na kamati yake kama kweli ao wanawajua viongozi safi. Kwanini wasiige mfano wa Kakobe kusema wazi fulani ni kiongozi safi na kuamrisha waumini wao wamchague badala ya kuandika nyaraka.

Mimi naona hao wanaotumia njia ya kutoa maelekezo wakati wenyewe wamejificha nyuma ya pazia ni wanafiki tena Sana na hawafai katika jamii.

Tunapenda viongozi wawazi yaani wale wanaobainisha kuwa fulani mbaya na fulani mzuri kama Mola anavyobainisha katika vitabu vyake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…