The Hunter
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 1,049
- 307
Kaka mkubwa pole kwa pilika zako za kutaka kutuongoza hapo 2015 naheshimu sana maamuzi yako kwakuwa yametambuliwa rasmi na katiba ninayoiamini, ila Mkuu, nikukumbushe tu kuwa Uongozi ni dhamana, isiyotaka hila au ujanja ujanja, kama wewe ni mwenye karama basi wananchi wenzako watakuchagua bila kuzingatia wewe ni wa kabila rangi au dini gani!
Ule uvumi uliosemwa hapa jukwaani kwamba umeamua kubadili dini toka ukristo na kuwa mwislamu,
yaani toka kuwa Bernard kuwa Khalfan umenifanya niamini mkuu umedhamiria kuongoza kwa hali yoyote,
naamini si kwamba unamapenzi ya kweli na uislamu, bali umelisoma game na ukajua ili kuzipata kura za watu wa pwani lazima uwe muislamu,
Yafaa nini kujitaabisha Bw Membe kama utumishi wako umetukuka? unafikiri kuwa mwislamu au Mkristo ndo kuchaguliwa? Toka ulipopata akili hukujua uislamu ni mzuri uende huko mpaka dakika hizi za mwisho kukaribia kuteuliwa mgombea wa ccm 2015 ndo unashtuka!?
Pole mkuu, waislamu hawataki wanafki, hivyo hata wakristo hawataki wanafki!!
Ila kaushauri kadogo; labda ubadili na kabila uwe ****** pia.
Ule uvumi uliosemwa hapa jukwaani kwamba umeamua kubadili dini toka ukristo na kuwa mwislamu,
yaani toka kuwa Bernard kuwa Khalfan umenifanya niamini mkuu umedhamiria kuongoza kwa hali yoyote,
naamini si kwamba unamapenzi ya kweli na uislamu, bali umelisoma game na ukajua ili kuzipata kura za watu wa pwani lazima uwe muislamu,
Yafaa nini kujitaabisha Bw Membe kama utumishi wako umetukuka? unafikiri kuwa mwislamu au Mkristo ndo kuchaguliwa? Toka ulipopata akili hukujua uislamu ni mzuri uende huko mpaka dakika hizi za mwisho kukaribia kuteuliwa mgombea wa ccm 2015 ndo unashtuka!?
Pole mkuu, waislamu hawataki wanafki, hivyo hata wakristo hawataki wanafki!!
Ila kaushauri kadogo; labda ubadili na kabila uwe ****** pia.