eti watu wa kagera walitegemea hoja za namna ya kuboresha maisha yao (kutoka kwa maandamano ya CDM), badala yake wakaambulia matusi na kejeli tu. <br />
Humu kumegeuka kijiwe cha wambea,hapa issue ya kujadili haipo na wewe na wenzio muache uvumi wa kunyanyua kila hoja ili mradi imepita ktk tv tu.Sasa ni wakati wa kazi na msifanye kijiwe hiki kama sehemu ya wauza kahawa ambapo kila habari inapatikana.Sio kila kitu ni issue,kwa thread hii unatafuta umbea tu toka kwa wenzio.Kuna haja ya kutafakari upya humu maake kinaonekana kama kakichaka flani ambako kamejificha eti great thinkers kumbe wafuasi waoga wa CDM(ambao ni invisible na maneno yao ni ya vilabu vya gongo).Lugha chafu kwa kuwa wanahisi hawawezi tambulika ni kujidanganya tuwe wastarabu pasije pakafungwa hapa sisi waficha sura na majina feki tukakosa pa kupumulia.