Kagame: I Fired EAC Minister Due To Incompetence

Kagame: I Fired EAC Minister Due To Incompetence

Huyo waziri wa PK aliyefukuzwa kazi alipewa haki ya msingi ya binadamu ya kujitetea. Ikiwa Mungu alimpatia Adamu, katika bustani Edeni, nafasi ya kujitetea kwa nini alikula matunda ya mti wa mema na mabaya, iweje PK asimpe nafasi ya kujitetea binadamu mwenzake? Ni kweli hatuwezi kuendelea kwa maneno lakini pia hatuwezi kuelewana pasipo kuzungumza maneno. Hakuna maendeleo pasipo maelewano. Maendeleo ni kwa ajili yetu iweje tufarakane kwa ajili ya maendeleo
Kagame ni dictator, na anataka Mawaziri wake wafanye kazi kama anavyotaka yeye.

Hii taarifa ni ya upande mmoja; hatujasikia kutoka kwa waziri aliyefukuzwa. Tusichukulie tu kuwa Waziri alikuwa na makosa kwa sababu Kagame kasema.

Inawezekana Waziri alikuwa sahihi, ila walitofautiana kimtizamo, na Kagame akamtimua kwa kuwa ndiye mwenye uamuzi wa mwisho!
 
kwangu mimi naona kuna haja ya kufikiria zaidi...si utendaji wake bali mabadiliko haya ya waziri wa EAC wa Rwanda tena ya gafla, na hili la vita ya maneno na JK Pia na huu ushirikiano mpya wa kiini maacho ulioitwa wa bandari ya pamoja na UG na KE, labda msimamo wa waziri wake katka hilo ndio limepelekea kutimiliwa kazi,,,,,wapekuzi wa magezet na habari za rwanda plz mfuatilie naisi kuna mambo mengi hapa.....
 
Huyu ndio raisi wetu in a nutshell. Hana mchezo katika kazi. Hana ndugu katika kazi. Yeye anaangalia maslahi ya nchi kwanza. Maandalizi mabovu ya mkutano tu yanamfukuzisha kazi waziri. Uwajibikaji. Hapo tanzania haya yanawezekana kweli?

Angekuwa mkweree hapo angekuwa anachekacheka tu na kwavile ni SHORI/MWANAMKE ndio ingekuwa basi tena hakuna mbungi!!! Nchi haiendeshwi hivyo mwnaume sharti uwe mkali.
 
Dikteta kagame kazini, hiyo sababu ni danganya toto tu lazima kuna kubwa nyuma ya pazia! Atakuwa alipingana nae kuhusu uamuzi wa kijinga wa kutaka kuitenga nchi mwanzilishi wa eac kwa chuki zake binafsi.
 
katika hizo taarifa zote sijaona wala kusikia tusi, wala jina la rais Kikwete! mkuu achana na habari za kikwete kutukanwa na kulalamika! mbona viongozi wetu wameshatutukana sana sisi Watanzania wenzao, mara "mtakula nyasi" mara "mpige mbizi" mara "wazee wanakaribia kufa" mara "wapigwe tu"! sasa yote hayo mnaona sawa ila akisemewa ukweli JK basi tunashinda mitandaoni kumkingia kifua!

huu sio wakati wa "kwanini JK atukanwe"
ni wakati wa kuangalia mbadala wa mapato baada ya Rwanda na Uganda kujitoa TpA;
ni wakati wa kuangalia namna ya kusafisha jina letu na biashara ya unga haramu;
ni wakati wa rais wetu kuacha kueleka chuki kwa raia wenye asili ya Rwanda, eti wahamiaji haramu; hivi miaka yote hakujua kama wapo?

Point yako ya mwisho is very true.

Alichofanya jamaa ni kwamba amejibiwa na mwanaume yeye akaona aende akawaonee wanyonge wenye asili ya Kagame ili na yeye aonyeshe kuwa ni mwanaume.
 
Dikteta kagame kazini, hiyo sababu ni danganya toto tu lazima kuna kubwa nyuma ya pazia! Atakuwa alipingana nae kuhusu uamuzi wa kijinga wa kutaka kuitenga nchi mwanzilishi wa eac kwa chuki zake binafsi.

Day dreaming wewe interahamwe.
 
This slim boy is very serious!!! Napenda uchapakazi wake kama si matusi yake ya juzi kwa Rais wetu bado ningemuona Rais wa mfano wa kuigwa!!

Hahaa huyu wetu anapigwa mitusi kwa sababu ya mawazo yake ya kitoto kwenye vitu serious
 
Am i the only one who is amazed at how TZdians are obsessed with Rwanda? Can i rightly summarize that Tzdians men and women alike are gossipers?
 
Seriously speaking, anybody associating with Kagame should be indicted because this guy is the worst war criminal in office today. Kagame’s crimes rank with those perpetrated by former Iraqi president Saddam Hussein and Sudanese leader Omar al-Bashir (who is wanted by the International Criminal Court on charges of genocide, war crimes, and crimes against humanity). Kagame kills people who he sees as potential whistle blowers to his deadly regime, in fact, he kills anybody who is willing to testify against him simply because he doesn't want the truth revealed. With him and Rwanda in EAC, I DO NOT see future of this organization last any longer as Rwanda is doomed to collapse again. Time will tell.
 
Back
Top Bottom