mjunguonline
Member
- Mar 10, 2011
- 73
- 5
MBUNGE wa Kigoma Kusini (NCCR Mageuzi), David Kafulila jana jioni alichafua hali ya hewa bungeni baada ya kuwataja wabunge wawili wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) kwa kuomba rushwa katika halmashauri ambayo hakuitaja.
Akichangia Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano, Kafulila aliwataja Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi na Mbunge wa Bahi, Omary Badwel wote wa CCM akidai kwamba aliwakamata wakiomba rushwa kwa viongozi wa halmashauri.
Wakati akitaja majina hayo, Kafulila nusra aingie katika mgogoro na Mwenyekiti wa Bunge, George Simbachawene ambaye alikuwa akimwamuru kukaa chini kutokana na muda wake wa kuchangia kumalizika.
Kafulila alikuwa akiendelea kuzungumza bila kujali kengele ya pili iliyopigwa kuashiria kwamba muda wake wa kuzungumza ulikuwa umekwisha.
"Mheshimiwa Mwenyekiti kwa wakati wa sasa ni vigumu kusimamia matumizi kwani mfumo wetu wa uongozi unaruhusu ufisadi, wapo viongozi, mawaziri, wabunge wanaomba rushwa...." alisema Kafulila na kuamsha zogo ambalo liliambatana na sauti zisizo rasmi katika ukumbi wa Bunge zikiuliza ".....wapo humu humu?" Kafulila alijibu "Ndiyo..." Sauti moja ilisema wataje, hapo ndipo aliposema ".... Wapo kina Zambi, Badwel,Â* nimewakamata na nimechukua hatua, hatuwezi kuendelea namna hii," kisha akaketi.
Akichangia Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano, Kafulila aliwataja Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi na Mbunge wa Bahi, Omary Badwel wote wa CCM akidai kwamba aliwakamata wakiomba rushwa kwa viongozi wa halmashauri.
Wakati akitaja majina hayo, Kafulila nusra aingie katika mgogoro na Mwenyekiti wa Bunge, George Simbachawene ambaye alikuwa akimwamuru kukaa chini kutokana na muda wake wa kuchangia kumalizika.
Kafulila alikuwa akiendelea kuzungumza bila kujali kengele ya pili iliyopigwa kuashiria kwamba muda wake wa kuzungumza ulikuwa umekwisha.
"Mheshimiwa Mwenyekiti kwa wakati wa sasa ni vigumu kusimamia matumizi kwani mfumo wetu wa uongozi unaruhusu ufisadi, wapo viongozi, mawaziri, wabunge wanaomba rushwa...." alisema Kafulila na kuamsha zogo ambalo liliambatana na sauti zisizo rasmi katika ukumbi wa Bunge zikiuliza ".....wapo humu humu?" Kafulila alijibu "Ndiyo..." Sauti moja ilisema wataje, hapo ndipo aliposema ".... Wapo kina Zambi, Badwel,Â* nimewakamata na nimechukua hatua, hatuwezi kuendelea namna hii," kisha akaketi.