Kafulila anajiamini nini?

Kafulila anajiamini nini?

ABC ZA 2025

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2018
Posts
1,349
Reaction score
851


Ndg zangu nimekutana na taarifa hii muhimu ya Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila kwakweli nimeshtuka kidogo na kujiuliza huyu bwana anajiamini nini kukubali kukabiliana na hawa wasomi?

Kwa wale wachache wanayo ifahamu vizuri historia ya Taifa hili ni Viongozi wakuu wawili tu Hayati Mwl Jk Nyerere na Hayati Edward Moringe Sokoine ndio viongozi pekee kwa kumbukumbu zangu kama sijakosea waliomudu kufanya mijadala ya wazi tena na kada hili la wasomi wa ngazi ya vyuo vikuu kikiwemo hiki cha Dar es salaam,

Watendaji wetu wengi wa Serikali kwa muda sasa wamekuwa si marafiki wa mijadala ya aina hii baadhi yao hawapendi kabisa kuhojiwa au kuulizwa maswali magumu magumu na yenye kukera kutoka kwa Watu wenye Mrengo tofauti na wao wakiwemo ma-activis wa mambo mbalimbali huko mavyuoni ambao wengi wao ni Wanafunzi wenye Mrengo na hulka za kipinzani hivyo Utulivu na uvumilivu umekuwa ukiwashinda Viongozi wengi hasa Viongozi wa Kiafrika ndio maana namwona Kafulila kama mtu mwenye kujiamini.

Kafulila lazima ajue shughuli hii ya kukutana na ma-activist haitakuwa ya polepole lazima ajipange sawa sawa lakini jambo moja zuri kutoka kwa Mkurugenzi huyu ni huku kujiamini kwake na kukubali kufanya mjadala wa wazi tena "Live" kwa manufaa ya Taifa lake hapa apongezwe hata kabla ya Mjadala.

Pamoja ya kwamba taarifa hii haijasema hiyo Jumanne tarehe 27.05.2025 ni vituo gani vya TV & Redio vitarusha tukio hili la kihistoria ila binafsi naahidi kufuatilia mjadala huu kwa karibu mwanzo mwisho tuone namna watu watakavyohenyeshana kwa hoja mbele ya Prof. Rwekaza Mukandara

===

IMG-20250526-WA0000.jpg

The Public-Private Partnership Centre (PPPC) and a University of Dar es Salaam (UDSM) think tank have joined forces to hold a workshop that will explore the role of public-private partnerships in the reallsation of the Tanzania National Development Vision 2050.

The PPPC will conduct the one-day workshop at UDSM's library complex on May 27 in collaboration with the Research and Education for Democracy in Tanzania (REDET).

"Public private partnerships have a key role to play in the realisation of Vision 2050 by their ability to help build resilience against external shocks and constrained public finances," said David Kafulila, Executive Director of the PPPC.

"The government has set out a bold and ambitious challenge to deliver significant development to the country over the coming years with Vision 2050. PPPs are an integral part of this national development blueprint."

Kafulila said the role of the private sector as the main driver of economic growth is underpinned in Tanzania's National Development Vision 2050.

He underscored the importance of Tanzania pursuing economic self-reliance by diversifying funding sources amid a global shift in development financing.

The workshop is expected to take a deep dive into a number of issues, including international capital markets, mobilization of financing, opportunities, and challenges.

Chief executive officers (CEOs), business leaders, and other private sector actors are also expected to be in attendance.

Tanzania had about 80 PPP projects by last month at different stages of implementation, according to the Ministry of Finance.

The government has implemented various legal and regulatory reforms intended to make it easier for the private sector to engage in partnerships with the public sector.

📷 David Kafulila, Executive Director of the PPPC, will make a presentation on the PPP model and its role in Vision 2050, while REDET Chairman Prof. Rwekaza Mukandala will moderate the workshop.
 
Hawa waliondamana kwa kumuunga sa100 ndo bado unawaita thinktenker?
 
Nadhani ni mjadala mzuri. Hasa ukizingatia kwamba elimu yetu na uendeshaji wetu wa uchumi misingi yake mikuu bado ni ya kiujamaa. Bado hatujajikira sana kwenye uchumi wa masoko huria ambamo sekta binafsi ndio msingi wa uendeshaji wa uchumi. Ni vizuri kutoa elimu kwa kutumia mijadala kama hii.
 
Katibu mkuu wa CCM mtarajiwa lazima ajiamini.
You can take this statement to the bank.
 
Back
Top Bottom