Kadinali Pengo ni mkweli au naye ni MSANII TU!?

Huyu kadinal Pengo anajifanya Mchicha Mwiba ,lakini ipo siku atanaswa ndani ya mtego Mbovu
 
Hii hisije kuwa ni hasira ya kuondolewa ulaji wa kusamehewa kodi.

HabariLeo | Viongozi wa dini waomba msamaha wa kodi upitiwe
Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Methodius Kilaini ameishauri serikali kupitia upya uamuzi wa kuyafutia msamaha mashirika ya dini na asasi za kiraia. Akizungumza jana na gazeti dada la Daily News, alisema taasisi hizo hazitengenezi faida na badala yake, zipo kwa ajili ya kuwainua watu wa kawaida ambao ni masikini. Alitoa mfano wa huduma za afya zinazotolewa hususan maeneo ya vijijini, ambazo nyingi hutolewa na taasisi za dini.

“Serikali ilipaswa kukaa na wadau kwa ajili kupata ushauri juu ya hasara na faida ya kuondoa msamaha huo kabla ya kutangaza bajeti yake,” alisema Kilaini. Wakati huo huo, Naibu Katibu Mkuu (masuala ya dini) wa Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA), Mohamed Khamis alisema uamuzi huo unakwamisha sera ya Taifa ya kuwapa maisha bora wananchi.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-na-mashehe-wanafiki-mmevuna-mlichopanda.html
 

X-PASTER, ahsante sana kwa wazo hili labda hili la kuondolewa msamaha limemkera mno Pengo hadi kutoa kauli aliyotoa. Alikuwa wapi miaka yote hii katika mapambano dhidi ya ufisadi? Kwa nini hakutoa kauli kama hii miaka miwili au mitatu iliyopita na kusubiri hadi sasa? Ni kitu gani kimemsukuma hadi kutoa kauli hii wakati huu? Una point kubwa sana Mkuu hapo, bahati mbaya hawa wakuu wa dini huwa ni wagumu sana kukaa na waandishi wa habari ili wawekwe kiti moto na kujibu maswali ambayo majbu yake Watanzania wengi tungepata kuyafahamu.
 
He needs to walk the talk kama mwenzake wa Zimbabwe alivyofanya. Kamkemea nani kwa jina katika hii martyrdom anayoitafuta? Na wengine wanaotuhumiwa si kondoo wake?

Amandla............

UW,


Unaweza ukawa na pointi ila kwa jinsi ulivyoweka hoja yako unakuwa kama umeweka conclusion badala ya hoja. Hebu jaribu ku-respond maswali ya hapo chini ndg yetu BAK naona ameyakimbia:

Ok, lets say Pengo hana nia blah blah blah na ni msanii.

Now lets talk sense and straight..ulitaka afanye kitu gani ili wewe roho yako iridhike kuwa si msanii? Je alikuahidi nini ambacho hajakitekeleza? Ni wajibu upi ambao ninyi msio waumini mlimpa mpaka mumdai kuwa hajafanya a,b,c na hivyo kustahili kuitwa msanii?

Naomba majibu mujarabu
 
Mhashamu Cardinal Pengo, nashukuru sana kwa yeye kuamua kuwa shahidi wa watanzania na kuamua kumwaga damu yake kwa ajili yetu, good move.
sasa haya ndiyo anatakiwa ayakabili, aseme wazi Mkapa alitumia madaraka yake vibaya na amelisababishia taifa hasara kubwa hivyo anatakiwa apandishwe kizimbani.

Pili Msiminary Chenge kalitia aibu kanisa kwani wizi anaoufanya hauendani na mafundisho ya kanisa anatakiwa apandishwe kizimbani bila ya kuonewa huruma.

tatu atengue kauli yake kwamba Kikwete ni chagua la mungu na aweke wazi kuporomaka kwa maadili ya uongozi wizi na rushwa iliyokithiri ni matokeo ya uongozi mmbovu wa rais J. Kikwete kwani wanaoharibu ni watu aliowachagua.

Tatu aitishe kikao na viongozi wengine wa dini mbali mali na wazungumzia mustakabali wa nchi na kila mmoja kwa uwazi ajadili na kuweka mikakakti ya kuwaeleza waumini wao nini wanatakiwa kufanya.

Atuambie nini wakikutana na Kikwete huwa wanamwambia na atuambie ni kitu gani kilimsukuma kwenda kufungua kitabu cha fisadi Lowassa akitumia jina la mkewe.

Unafiki ndio unatumaliza tanzania.
 
anatuzuga, nguvu aliyonayo ni kubwa sana, akiwapa modality mapadri, CCM inang'oka..


Tatizo letu humu JF wengi wetu ni kutoatu lawama zisizo na kichwa wala miguu. Huku tunataka viongozi wa dini wasiguse mambo ya 2010 kuhusu kuwahamasisha wananchi wajiandikishe na kupiga kura kwa makini, at the same time tunawalalamikia eti ni ufisadi umeshamiri.

Sasa wewe unasema akiwapa modality ya kuing'oa CCM, huoni huku ndio kuchanganya siasa na dini?
 
Mhashamu Cardinal Pengo, nashukuru sana kwa yeye kuamua kuwa shahidi wa watanzania na kuamua kumwaga damu yake kwa ajili yetu, good move.
sasa haya ndiyo anatakiwa ayakabili, aseme wazi Mkapa alitumia madaraka yake vibaya na amelisababishia taifa hasara kubwa hivyo anatakiwa apandishwe kizimbani.

Pili Msiminary Chenge kalitia aibu kanisa kwani wizi anaoufanya haundani na mafundisho ya kanisa anatakiwa apandishwe kizimbani bila ya kuonewa huruma.

tatu atengue kauli yake kwamba Kikwete ni chagua la mungu na aweke wazi kuporomaka kwa maadili ya uongozi wizi na rushwa iliyokithiri ni matokeo ya uongozi mmbovu wa rais J. Kikwete kwani wanaoharibu ni watu aliowachagua.

Tatu aitishe kikao na viongozi wengine wa dini mbali mali na wazungumzia mustakabali wa nchi na kila mmoja kwa uwazi ajadili na kuweka mikakakti ya kuwaeleza waumini wao nini wanatakiwa kufanya.

Atuambie nini wakikutana na Kikwete huwa wanamwambia na atuambie ni kitu gani kilimsukuma kwenda kufungua kitabu cha fisadi Lowassa akitumia jina la mkewe.
Unafiki ndio unatumaliza tanzania.

Kinepix2, Ahsante sana kwa maswali yako mazuri sana. Swali lako linaonyesha unafiki wa hawa viongozi wetu wa dini mbali mbali. Huyu Pengo miezi michache iliyopita alihudhuria ufunguzi wa kitabu hicho huku akijua fika kwamba Lowassa alihusika moja kwa moja na ufisadi uliofanywa na kampuni ya Richmond halafu leo hii anatwambia kwamba yuko tayari kufa katika mapambano dhidi ya ufisadi na wakati huo huo akialikwa na mafisadi anatoka mbio kuhudhuria mwaliko aliopewa bila hata kutafakari athari ya yeye kuhudhuria mwaliko aliopewa.
 
Tatizo letu humu JF wengi wetu ni kutoatu lawama zisizo na kichwa wala miguu. Huku tunataka viongozi wa dini wasiguse mambo ya 2010 kuhusu kuwahamasisha wananchi wajiandikishe na kupiga kura kwa makini, at the same time tunawalalamikia eti ni ufisadi umeshamiri.

Sasa wewe unasema akiwapa modality ya kuing'oa CCM, huoni huku ndio kuchanganya siasa na dini?

Abdulhalim, wengi tunawaunga mkono hawa viongozi wa dini katika jitihada zao za kuwaelimisha wapiga kura wa Kitanzania ili kuhakikisha katika uchaguzi unaokuja wa 2010 tupate viongozi bora ambao wataweka mbele maslahi ya Tanzania na Watanzania kuliko ilivyo sasa ambapo maslahi yamewekwa kwa mafisadi na makampuni ya kigeni, lakini wakati huo huo haituzuii kama Watanzania kuhoji mienendo yao mbali mbali ambayo inaonyesha hawapo makini katika vita dhidi ya mafisadi. Labda maswali yetu kwao yanaweza yakawafanya wawe makini katika mienendo yao na hivyo kutoonekana wanafiki wa kutoa kauli ambazo hakuna ufuatiliaji wowote na wakati mwingine kufanya matendo au kutoa kauli ambazo zinaonekana zimejaa unafiki.
 
Back
Top Bottom