Kada wa CCM lawamani kwa kuisaidia CHADEMA

Kada wa CCM lawamani kwa kuisaidia CHADEMA

Joined
Mar 23, 2012
Posts
64
Reaction score
13
NA STEPHANO MANGO, SONGEA

BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Songea mkoani Ruvuma wamekitaka chama hicho ngazi ya Mkoa kumchukulia hatua za kinidhamu Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa Joseph Mhagama kwa kitendo chake cha kujihusisha na kufanikisha harakati za Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wanachama hao walisema kuwa kitendo cha kada huyo kushirikiana na Diwani wa kata ya Kilagano Bathromeo Nkwera ambaye ni kada wa Chadema kinaleta wasiwasi wa imani ya Joseph Mhagama katika chama chake cha CCM na hasa baada ya kutangaza nia ya kutaka kugombea ubunge katika jimbo la Peramiho kupitia CCM.

Wanceraus Komba ambaye ni Kada wa CCM na Mwenyekiti wa Ujenzi wa Zahanati ya Mhepai alisema kuwa hali ya Kisiasa ya Jimbo la Peramiho inavurugwa sana na Joseph Mhagama kwani amekuwa akishawishi baadhi ya viongozi wamuunge mkono katika harakati za ubunge kupitia CCM huku akiwa muda mwingi anautumia kumsaidia diwani wa CHADEMA katika mipango yake.

Komba alisema kuwa hali hiyo inasikitisha sana na kuwafanya viongozi mbalimbali wa Chama katika Jimbo hilo kutoelewa imani yake katika chama na mwenendo mzima wa harakati zake kwani zinatutia shaka sana katika uendelezaji wa majukumu na ilani ya chama ya 2010 na 2015

Alisema kuwa pia inasikitisha sana kuona chama kinamuachia Mhagama kuanza kampeni mapema ya kutaka ubunge kabla ya wakati huku akijua kuwa muda uliobaki ni muhimu kuhakikisha kuwa ilani ya uchaguzi inatekelezwa ili muda wa kampeni ukifika wananchi waelezwe ahadi za chama namna zilivyotekelezwa.

Alieleza kuwa vitendo hivyo vyote vya kumsaidia Diwani wa Chadema na kuanza kampeni mapema vinapaswa vichunguzwe na vichukuliwe hatua kali za kinidhamu ili chama kibaki salama wakati huu ambao tunalekea kwenye uchaguzi mkuu wa Udiwani, ubunge na urais.

Akizungumza na gazeti hili Joseph Mhagama alisema kuwa toka mwaka 2010 amekuwa akisaidia mambo mbalimbali kwenye kata zote za halmashauri ya wilaya ya Songea ambayo ndio Jimbo la Peramiho.

Mhagama alisema kuwa amekuwa akitoa fedha, mipira, jezi na misaada mingine ambayo wanamuomba na wala habagui ila Diwani wa Kata ya Kilagano Nkwera amekuwa akimuomba misaada mara kwa mara na hivyo amekuwa akimpatia.

Kwa Upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Songea Rajabu Uhonde alisema kuwa amesikitishwa sana na mwenendo wa Joseph Mhagama na hasa akiwa ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Ruvuma kwani anaamini kuwa anafahamu fika kuwa lengo la CCM ni kushika dola.

Uhonde alisema kuwa kada huyo anafahamu sheria na kanuni za chama hivyo kwa hayo ambayo anayafanya ana hatarisha uhai wa chama na kutokana na makosa hayo ambayo wanachama wanamlalamikia basi ni vyema chama kikamfuatilia na kumchukulia hatua stahiki kulingana na yale ambayo yatabainika

Alisema kuwa licha ya kupata taarifa za kukiuka kanuni za chama pia Mhagama amekuwa akilalamikiwa kuyagawa makundi ndani ya jumuiya za chama kwa kufanya vikao mbalimbali ambavyo vinaashiria kutengeneza safu yake ya ushindi wa ubunge huku akijua kuwa mbunge aliyopo bado anatekeleza ilani husika.
 
Tatizo tupo ndani tunaona kila kitu bora tuwasaidie hawa jamaa kuliko,mnayotunyia viongozi wetu wa ccm. Halafu kwani dhambi kuandaa na kutangaza nia? Au umetumwa na Jenister au wewe ndie Mhagama Jenny? Huna hati miliki ya Peramiho. Elewa siasa sio ugomvi kumsaidia diwani wa wananchi kuwatumikia wananchi sio tatizo labda ungenambia amemsaidia kuiba ila kama kusaidia kwa nia njema sio point. Mnachowalalamikia chadema kuwa wanabagua watu mnafanya tena hichohicho.
 
ccm haina ubavu wa kufukuza mtu ndani ya chama kwa wakati huu. Mtatafunana mpaka mmalizane
 
Mtakuwepo wengi sana mwaka huu mtaishia kusingizia njama za kuuwawa
 
Mim nilikuwa naipenda sana ccm lakini nilivyoona hela za escrow zinachukuliwa alafu wakawahoj watu kukawa kimyaaa nimeamua kukichkia chama chagu ccm japo siwez kutoka,NAKICHUKIA "LAKINI SIWEZI KUTOKA"
 
Back
Top Bottom