Dr hyperkid
JF-Expert Member
- Jun 7, 2019
- 13,738
- 27,103
Mola ampe tahafifu mapema makurudi kuijenga nchi
Huyo jamaa alipona?Yaani hawa jamaa hawana tofauti na mafisi yaonapo kundi LA kondooView attachment 1202907
Una roho mbayaWange Mmawazo 2 Nayeye
We ni kichaa haiwezekani mtu mwenye akili timamu kuandika ushuzi huuKada kacharangwa. Hayo mengine hayanihusu.Nimelalia hapo kwenye ukada ili furaha yangu ikamilike
Kama ni mccm powa tu
Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) aliyekuwa mgombea ubunge wa Vunjo kupitia chama hicho mwaka 2015, Innocent Melleck amenusurika kifo baada ya kucharangwa mapanga na watu wasiojulikana jijini Dar es Salaam.
Melleck ambaye katika uchaguzi huo mwaka 2015 alichuana vikali na mbunge wa sasa wa jimbo hilo, James Mbatia (NCCR-Mageuzi) amecharangwa mapanga maeneo ya mwili eneo la kichwani, mabegani, mgongoni na kwenye mguu wa kushoto.
Akizungumza kwa taabu na Mwananchi leo Jumatatu Septemba 9,2019 amesema tukio hilo lilitokea usiku saa 5, Alhamisi iliyopita ya Septemba 5, 2019 akiwa jirani na nyumbani kwake Goba nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
"Vijana wawili wakiwa na pikipiki walikuwa jirani na nyumbani kwangu, walionekana kama kuhitaji msaada, mmoja akasogea kwenye gari yangu akagonga," anasimulia.
Anasema alishusha kioo ili kumsikiliza, lakini kabla ya kuzungumza naye chochote alimfunika usoni na kitambaa na akapoteza fahamu.
"Sikujua kilichoendelea hadi nilipozinduka nikiwa hospitali ya Kairuki ambapo niliambiwa nilitupwa njia panda ya Kawe, nilisaidiwa na madereva bodaboda ambao walitoa taarifa Polisi Kawe," anasema
Anasema waliomvamia walichukua fedha Sh11 milioni ambazo alikuwa nazo kwenye gari, flash mbili, laptop na simu mbili za mkononi.
"Nafikiri walikuwa na nia ya kuniua, kwani walinicharanga mapanga kichwani nikiwa nimepoteza fahamu, kwenye gari kulikuwa na vitu vingine vya thamani lakini hawakuchukua zaidi ya flash mbili, laptop, simu mbili za mkononi na fedha," anasema
Anasema tukio hilo limepeleka kuogopa kurejea nyumbani hata baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali ambako amefanyiwa upasuaji mkubwa uliochukua saa nane.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Mussa Taibu alipoulizwa amesema wakati tukio linatokea alikuwa Shinyanga kikazi.
"Anayepaswa kunipa taarifa ni OCD ambaye nimejaribu kuwasiliana naye bahati mbaya yuko katika shughuli za mitihani," amesema Kamanda Taibu.
Mkuu wa Upelelezi Kawe, Alfred Lugamara amesema tukio hilo limeripotiwa polisi Kawe na upelelezi bado unaendelea.
"Mtu mmoja anaitwa Innocent Shirima (Melleck), kesi yake bado inachunguzwa, sababu mwenyewe hakuweza kutoa maelezo yoyote kutokana na hali yake kiafya, alichukuliwa Goba akatelekezwa njia panda ya kawe akiwa amejeruhiwa," alisema Alfred.
-Mwananchi-
Ila waliomcharanga hadi kumtoa roho Alphonse Mawazo ni malaika. Hilo kwa vile ni liccm wangelitoa roho tu dadeqUna roho mbaya
Duuuuu hawa Chadema waneanza tenaWrite your reply...Chadema wameanza ujambazi
Una roho ya kishetani kabisa.Ila waliomcharanga hadi kumtoa roho Alphonse Mawazo ni malaika. Hilo kwa vile ni liccm wangelitoa roho tu dadeq
Kujiamini kwingi halafu watu hawajui sio wote walioko karibu yao ni watu wazuri naamini hii ni inside job!Mil 11 anatembea nazo kwenye gari, saa 5 usiku, alafu unagongewa dirisha la gari unafungua. Jamani, security alerts ndogo ndogo mjue zitawasaidia sana maishani..!!
Wangemtoa roho kabisa kama walivyomtoa roho Mawazo.Una roho ya kishetani kabisa.
Hivi Israili anakosea wapi siku hizi?Inatuhusu nini sissi kwanini hakufa
Mkuu walisema wanaimarisha ulinzi kipindi cha mkutano,kwasababu umeisha nadhani shughuli za wahuni zemerejea.Hilo ni jiji la kifutu imekuaje tena wakati ni juzi tu hapa anamwagiwa misifa kua jiji liko shwari kabisa!
Hata mimi nimewaza sana hili jambo..Mil 11 anatembea nazo kwenye gari, saa 5 usiku, alafu unagongewa dirisha la gari unafungua. Jamani, security alerts ndogo ndogo mjue zitawasaidia sana maishani..!!