Kaburi la Bibi Titi Mohamed

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,788
30,086
KABURI LA BI. TITI MOHAMED, KISUTU

Siku tatu hizi zimekuwa ngumu sana kwangu na naamini na kwa wenzangu wengi tuliokulia Dar es Salaam kwa kuondokewa na wapenzi wetu.

Juzi nikiwa nimesimama pembeni mwa kaburi tukimzika mmoja wa wapendwa wetu jicho langu lilivutiwa na kaburi lililokuwa pembeni kwa jinsi majani ya kijani yalivyokuwa yameota kama vile kuna mtu ananyeshea majani yale maji kila siku na kupalilia.

Kaburi hili ni kaburi la Bi. Titi Mohamed mmoja wa wapigania uhuru wa Tanganyika.

Bi. Titi alipata kuniambia nyumbani kwake nilipokwenda kutaka kufanya mahojianonae ya historia ya maisha yake wakati nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes.

Alinambia, ''Bwana Mohamed una lipi wewe la kuandika kuhusu mimi ambalo bado halijaandikwa?''

Hakika sikuwa na jipya ambalo halikuwa limeandikwa kuhusu Bi. Titi lakini pia nilikuwa na mengine ambayo yeye hakuyasema kuhusu maisha yake na wengi hawayajui lakini wale waliokuwapo wakati wa kupigania uhuru walinieleza.

Abbas Sykes na Tewa Said Tewa walipata kunieleza mengi kuhusu Bi. Titi na uwezo wake katika kuhamasisha umma wakati wa kupambana na Waingereza.

Nitalieleza moja.

Abbas Sykes anasema, ''Tuko chini ya jukwaa tunasubiri kuanza mkutano Mnazi Mmoja.

Nyerere anataka kupanda jukwaani lakini anatuambia kuwa nachoka na hana jipya la kusema.

Nyerere hakika amechoka basi atamwendea Bi. Titi, ''Titi hebu anza wewe kuzungumza,'' Mwalimu atamwambia Bi. Titi.''

Bi. Titi atapanda jukwaani akisindikizwa na nyimbo mashuhuri ya TANU iliyokuwa ikiimbwa na Bi. Hawa Maftah na kundi lake la akina mama:''Muheshimiwa nakupenda sana wallah sina mwinginewe, In Shaa Allah Mungu yuko Tanganyika tutajitawala.''

Bi. Titi atakapoanza kuzungumza uwanja utalipuka kwa vimondo ambavyo Bi. Titi anavirusha.

Bi. Titi anawauliza Waingereza, '' Hivi nyie hamna kwenu? Kwa nini mnatung'ng'ania hivi ondokeni nendeni kwenu. Nyie watu gani msiojua kukataliwa?''

Vifijo vinazizima uwanja mzima.

Mwalimu Abbas Sykes akanambia kuwa kutokana na hotuba ile ya Bi. Titi Nyerere atakuwa kapata ''cue'' na atakapopanda jukwaani Nyerere atapita mle mle alimopita Bi. Titi lakini kwa namna nyingine ya kuhutubia.

Allah mrehemu mama yetu na lifanye kaburi lake kuwa moja ya mabustani ya peponi.

KABURI LA BI. TITI.jpg
BI. TITI STREET.jpg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wa pwani hasa Dar es salaam wana mchango mkubwa sana katika kuzaliwa kwa taifa hili (Tanzania), na inasemekana Nyerere alipewa msaada mkubwa Sana na wenyeji wake wa Dar kipindi Cha harakati za ukombozi. Ila Cha ajabu hv Sasa watu wa pwani wamekuwa wakibezwa sana Kama si lolote.

Hivi ukiachia ile barabara iliyopewa jina lake, huyu Malkia ana kumbukumbu gani nyingine hapa nchini?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wa pwani hasa Dar es salaam wana mchango mkubwa sana katika kuzaliwa kwa taifa hili (Tanzania), na inasemekana Nyerere alipewa msaada mkubwa Sana na wenyeji wake wa Dar kipindi Cha harakati za ukombozi. Ila Cha ajabu hv Sasa watu wa pwani wamekuwa wakibezwa sana Kama si lolote.

Hivi ukiachia ile barabara iliyopewa jina lake , huyu Malkia ana kumbukumbu gani nyingine hapa nchini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ulitaka apewe nini?
 
Bibi Titi hata ajulikani saana kivile.ila alikua mama shupavu na mwenye uthubutu tena wala haogopi. Makamo wa Rais Muheshimiwa Samia Suluhu Hassan mambo yake makini na jinsi haiba yake ilivyo nahisi kama bibi titi alikua hivyo.na ule wanja wa makamo wa rais mashallah kama bibi titi vile vile bwana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wa pwani hasa Dar es salaam wana mchango mkubwa sana katika kuzaliwa kwa taifa hili (Tanzania), na inasemekana Nyerere alipewa msaada mkubwa Sana na wenyeji wake wa Dar kipindi Cha harakati za ukombozi. Ila Cha ajabu hv Sasa watu wa pwani wamekuwa wakibezwa sana Kama si lolote.

Hivi ukiachia ile barabara iliyopewa jina lake , huyu Malkia ana kumbukumbu gani nyingine hapa nchini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Natamani hata Chuo Kikuu Kimoja kipewe jina la huyu Shujaa.
 
Nyerere hoyeeee!

Julius K. Nyerere, Roman Catholic, Zanaki, anti-colonial activist, politician, and political theorist.

In October 1942, Nyerere completed his secondary education and decided to study at Makerere College in the Ugandan city of Kampala. He secured a bursary to fund a teacher training course there, arriving in Uganda in January 1943. At Makerere, he studied alongside many of East Africa's most talented students, although spent little time socializing with others, instead focusing on his reading.

He took courses in chemistry, biology, Latin, and Greek. Deepening his Catholicism, he studied the Papal Encyclicals and read the work of Catholic philosophers like Jacques Maritain; most influential however were the writings of the liberal British philosopher John Stuart Mill. He won a literary competition with an essay on the subjugation of women, for which he had applied Mill's ideas to Zanaki society. Nyerere was also an active member of the Makere Debating Society, and established a branch of Catholic Action at the university.
 
tunasubiri taazia ya Salum Shamte
Laki...

Hujapata kuona mtu karim kama Salum Shamte.

Mlango wa nyumba yake ulikuwa wazi kwa kila muhitaji.

Kwa kipindi karibia miaka 10 tuko sote Tanga kila mwezi bila kukosa wala kumkumbusha akinipa fedha nimlipe mwalimu wa madrasa Muheza.

Siwezi kuhadithia yote.

Akipenda mambo ya kheri na mfuko wake ulikuwa wazi muda wote. Slim kawasomesha watoto wa nduguze katika imani udaktari chuo kikuu na leo watoto hawa wanatibu watu katika hospitali kubwa na wanawafaa wazee wao na watu wengine.

Hakuna watu watakaoelemewa na msiba huu kama ndugu zetu wa Tanga.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hvy ndivyo waislam tunavyozikwa tena ukienda sehem zingine makaburi hayajengewi kabisaaaa, kikubwa sie tunamdhaifu khery tu huko alipo inatosha

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtu mwenye wadhifa hapaswi kuzikwa hivyo ni aibu. Usipojengea kaburi ni rahisi kupotea watu hawayajengei kama fashion ila ni kutunza kumbukumbu kwamba fulani alizikwa hapa.
.
Dini yenu haiendani na nyakati kiasi kwamba mambo ya karne ya 7 mnayafanya karne ya 21.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom