Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Profesa Palamagamba Kabudi amesema Tanzania imepiga hatua kubwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwani kwenye Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Serikali yake imeridhia mabadiliko katika ule utaratibu wa kupita bila kupingwa.
Akizungumza Jijini Arusha wakati wa mdahalo katika kongamano la kupongeza miaka minne ya mafanikio ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Waziri Kabudi amesema viongozi hao wote hivi sasa ikiwa akisalia mwenyewe kwenye mchakato wa uchaguzi atapigiwa kura ya ndiyo au hapana jambo linaloifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza duniani ambayo imeruhusu utaratibu huo ili kuimarisha zaidi demokrasia.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
"Tanzania ndio nchi ya kwanza Duniani ambayo sasa mwenyekiti wa kijiji, kitongoji, diwani, mbunge na Rais akiwa peke yake kwenye uchaguzi anapigiwa kura ya ndiyo au hapana. Uingereza hadi sasa anapita moja kwa moja, sasa watu wanasahau kule kupita bila kupingwa tuliletewa na waingereza lakini sisi tumekwenda mbele ya waingereza kwamba sasa wewe ukibaki peke yako lazima upigiwe kura. Kwa mabadiliko hayo, Je! reform hiyo ni ndogo au kubwa?", amehoji Profesa Kabudi
"Na uchaguzi huu wa viongozi wa vijiji kuna ambao kura za hapana zilikuwa nyingi kuliko ndiyo, Naibu Katibu Mkuu hayo watu waelezwe kuna ambao hapana zilikuwa nyingi na uchaguzi ulirudiwa…Je!, hiyo ni reform au sio reform?". ameendelea kuhoji Profesa Kabudi
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
"Tanzania ndio nchi ya kwanza Duniani ambayo sasa mwenyekiti wa kijiji, kitongoji, diwani, mbunge na Rais akiwa peke yake kwenye uchaguzi anapigiwa kura ya ndiyo au hapana. Uingereza hadi sasa anapita moja kwa moja, sasa watu wanasahau kule kupita bila kupingwa tuliletewa na waingereza lakini sisi tumekwenda mbele ya waingereza kwamba sasa wewe ukibaki peke yako lazima upigiwe kura. Kwa mabadiliko hayo, Je! reform hiyo ni ndogo au kubwa?", amehoji Profesa Kabudi
"Na uchaguzi huu wa viongozi wa vijiji kuna ambao kura za hapana zilikuwa nyingi kuliko ndiyo, Naibu Katibu Mkuu hayo watu waelezwe kuna ambao hapana zilikuwa nyingi na uchaguzi ulirudiwa…Je!, hiyo ni reform au sio reform?". ameendelea kuhoji Profesa Kabudi