Developer IOS
JF-Expert Member
- Jun 20, 2017
- 1,457
- 1,409
Habari wakuu,swala la kuongoza nchi na kuiletea nchi maendeleo ni swala gumu sana linahitaji chama na kiongozi makini,swala hili linahitaji chama na kiongozi aliyejitoa kupigania ukweli na haki kiongozi mwenye msimamo wa kweli kwenye mambo yenye manufaa na taifa sio kiongozi wa matukio na mwenye kuongelea mambo mengi kihisia ili kutafuta huruma ya wananchi.
Uzuri watanzania wa leo wanajielewa sio wa kuyumbishwa yumbishwa despite wamebaki wachache ambao wapo kama misukule kumradhi lakini kwa kugha hii niliyotumia.Nimetumia lugha hii kumaanisha watu wasio weza kuhoji uhalali wa kitu zaidi ya kupelekwa pelekwa kama misukule.
Cdm wamekuwa kama misukule ya mbowe ambao wanafata kila kitu mbowe anachosema bila kuhoji uhalali wake.Leo wanachama wa cdm wameshindwa kuhoji mambo machache tu ya msingi kama
Uzuri watanzania wa leo wanajielewa sio wa kuyumbishwa yumbishwa despite wamebaki wachache ambao wapo kama misukule kumradhi lakini kwa kugha hii niliyotumia.Nimetumia lugha hii kumaanisha watu wasio weza kuhoji uhalali wa kitu zaidi ya kupelekwa pelekwa kama misukule.
Cdm wamekuwa kama misukule ya mbowe ambao wanafata kila kitu mbowe anachosema bila kuhoji uhalali wake.Leo wanachama wa cdm wameshindwa kuhoji mambo machache tu ya msingi kama
- Kwa miaka zaidi ya saba wafuasi na wapenzi wa cdm waliaminishwa kuwa bw mamvi aka rais wa mioyo ya watu kama wanavyompamba leo ni adui mkubwa wa maendeleo ya taifa hili.Nishawahi kunukuu baadhi ya maneno ya kamanda lema akithibitisha umma kuwa anaushahidi wote kuwa lowassa ni fisadi.Tujikumbushe maneno ya Lema kuhusu fisadi Lowassa.Je wafuasi wa chadema mmeshindwa kuhoji juu ya usafi wa edward lowassa?.je mmeshindwa kuuliza kati ya ufisadi wa lowassa na ushahidi kipi ni halali?kama ushahidi si halali je kwa kutokuwa makini huku mnaweza kweli kutawala nchi?.kama ushahidi ni halali je kweli ni sahihi kumpa ikulu mlanguzi?
- Kwanini watu wote wanaompinga mbowe wanapotezwa? tukianza kwenye kifo chenye utata cha chacha wangwe kuvuliwa unanachama zitto kabwe na kuitwa msaliti pia kufukuzwa kwa juliana shonza.vyote vilitokana na kupinga na kumkosoa mbowe.wanachama wa chadema mnashindwa kudai demokrasia ndani ya chama na uhuru wa kuhoji inasikitisha sana.
- Kwanini hakuna anaejitokeza kupingana na mbowe kwenye nafasi ya uenyekiti wakati wa uchaguzi mkuu?Mara zote mbowe hupita bila kupingwa je hii inamaanisha ndani ya cdm hakuna mtu mwingine mwenye uwezo wa kuwa mwenyekiti zaidi ya mbowe?kama ni hivyo je mbowe akifariki ghafla ndo chadema imekufa?
- Mapato na matumizi ya pesa za ruzuku?kwa miaka zaidi ya ishirini cdm kimeongoza kuwa chama masikini kila siku kinapitisha bakuli licha ya kupokea pesa nyingi ya ruzuku kutoka serikali inasikitisha sana leo chama hakimiliki asset yoyote nembo ya chama inatumika kwa manufaa ya mbowe huku misukule yake inashindwa kuhoji kwanini kwa zaidi ya miaka 25 chama hakina hata jengo la chumba kimoja cha makao makuu?
- iko wapi agenda ya kupinga rushwa na ufisadi?leo hata humu jamiiforums hakuna tena zile thread zenye muktadha wa kupinga rushwa na ufisadi since misukule ya mbowe ilivyobadilishiwa gia angani.Dr slaa ameondoka na agenda yake leo kadhi kubwa ya cdm kutetea wale waliowaita wezi.mfano mzuri kwa nyalanduLazaro Nyalandu, Miss Tanzania na 40,000 za Ujenzi wa Shule!.leo kawa mwema na ukimgusa utashambuliwa hadi bhasi