Kabla hujafungua mdomo wako shirikisha akili yako

Galacha Maestro

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
1,353
2,216
KABLA HUJAFUNGUA MDOMO WAKO , SHIRIKISHA AKILI YAKO

Kabla hujafungua mdomo wako, kwanza shirikisha akili yako.
Kufungua mdomo kabla ya kushirikisha akili ni chanzo kikubwa cha matatizo yako na watu wengine.
Kabla ya kufungua mdomo ni vizuri ukafikiri kwa kina, ili kile unachokwenda kuzungumza kiwe bora.
Baadhi ya maswali unayoweza kujiuliza kabla ya kufungua mdomo wako;
1. Je hiki ninachokwenda kusema ni muhimu?
2. Je kinaweza kumsaidia mtu ambaye atakisikia?
3. Je kina mchango chanya kwa kila atakayekisikia?
Kama majibu ni ndio kwenye maswali yote, basi unaweza kusema kitu hiko, na hakika kitakuwa msaada kwa wengine.
Ila kama utaongea tu bila ya kufikiri, utajikuta unaongea vitu ambavyo sio muhimu, au visivyo na msaada wowote kwa wengine na mbaya zaidi vinakuwa na mchango hasi.
Na pia unapoongea bila ya kufikiri utajikuta unaongea sana, na ukishakuwa muongeaji sana, jua wewe ndiye utakayepoteza. Wanaopata zaidi ni wale wanaosikiliza na kuangalia zaidi ya wanavyoongea.
Na kumbuka neno likishatoka kwenye mdomo wako huwezi kulirudisha tena. Ni vyema ukaongea kile ambacho unaweza kukisimamia.
Kabla hujafungua mdomo wako kuongea, shirikisha akili yako na hakikisha unaongea kitu chenye mchango mkubwa. Hii ni muhimu sana kwa kupata na kuendelea kuwa na mafanikio makubwA.
 
Maskini NAPE ana wakati mgumu mwaka huu...hii ni trela tu.
 
Mkuu Galacha Maestro nakubaliana na wewe kwa ulichokisema japo neno 'fikiri' linaweza kuonekana gumu kutegemea na mazingira.

Kwa mfano inawezekana kufikiri vizuri pale unapowasiliana na mtu kwa njia ya ujumbe wa simu, mtu unapata muda wa kufikiri hata dakika tano, kumi au hata mbili sio mbaya, sasa tatizo ni kuwa thinker kwenye mazungumzo ya barabarani/njiani au popote pale ulipokutana na mtu bila kupanga au kubadilisha mazungumzo. Vyovyote vile iwavyo kufikiri kabla ya kusema ni muhimu ila pia inategemea na hitimisho lako kama fikra yenyewe na uwezo wako wa kufikiri ulivyo, maana unaweza ukapata muda wa kufikiri ila mwisho inakuwa ni yale yale ya "the way you see a problem is the problem".
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Galacha Maestro nakubaliana na wewe kwa ulichokisema japo neno 'fikiri' linaweza kuonekana gumu kutegemea na mazingira.

Kwa mfano inawezekana kufikiri vizuri pale unapowasiliana na mtu kwa njia ya ujumbe wa simu, mtu unapata muda wa kufikiri hata dakika tano, kumi au hata mbili sio mbaya, sasa tatizo ni kuwa thinker kwenye mazungumzo ya barabarani/njiani au popote pale ulipokutana na mtu bila kupanga au kubadilisha mazungumzo. Vyovyote vile iwavyo kufikiri kabla ya kusema ni muhimu ila pia inategemea na hitimisho lako kama fikra yenyewe na uwezo wako wa kufikiri ulivyo, maana unaweza ukapata muda wa kufikiri ila mwisho inakuwa ni yale yale ya "the way you see a problem is the problem".
Asante kwa.maoni yako mazuri.
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom