kuna gari zimekuwa modified huko Japs kuna Altezaa cif' zinafika Usd 15,000/= nani za mwaka 2002 uko so ni wazi kodi yako itakua tofauti na huyu mwenye Teza wa cif' ya usd 2,000/=Sawa mkuu nimekuelewa but hiyo calculator si unajaza full description ya hilo gari, sasa iweje bei ibadilke?
Sawa mkuu nimekuelewa but hiyo calculator si unajaza full description ya hilo gari, sasa iweje bei ibadilke?
Hivi Bill of Lading si hua inatumwa kwa couriee i.e DHL etc au inakuja na meliMimi huwa natumia calculator kama base ya ku bargain, maana inanipa makadirio ya bei ya gari husika. Nikiona bei ya gari ni kubwa zaidi ya CIF ya TRA huwa nina assume gari iko over priced. Hivyo nita bargain. Bahati mbaya sana ikiwa underpriced kulingana na calculator ya TRA, wao watatumia CIF ya calculator yao....
Habari za muda huu,
Pamekuwa na thread nyingi sana za watu kuomba ushauri/ elimu hasa kwenye suala zima la budget halisi/ kamili ambayo mtu anahitaji kuwa nayo kuweza kumiliki gari...
Mimi huwa natumia calculator kama base ya ku bargain, maana inanipa makadirio ya bei ya gari husika. Nikiona bei ya gari ni kubwa zaidi ya CIF ya TRA huwa nina assume gari iko over priced. Hivyo nita bargain. Bahati mbaya sana ikiwa underpriced kulingana na calculator ya TRA, wao watatumia CIF ya calculator yao.
Hapa kuna mfano wa magari mawili yanayofanana kila kitu yanayouzwa na watu wawili tofauti (sijasoma miongozo ya TRA mahali popote, ila ni uzoefu niliopata, kama kuna watu wana miongozo wanaweza itoa).
Mfano wa gari ya kwanza
Seller CIF (ambayo itakuja kwenye bill of lading): USD 12,000
TRA CIF (Ipo kwenye calculator): USD 10,000
Status kwa mujibu wa TRA: Overpriced
CIF ipi itatumika kukadiria kodi: ya Seller ambayo ipo kwenye bill of lading
Mfano wa pili gari ileile muuzaji tofauti
Seller CIF (ambayo itakuja kwenye bill of lading): USD 7,000
TRA CIF (Ipo kwenye calculator): USD 10,000
Status kwa mujibu wa TRA: Underpriced
CIF ipi itatumika kukadiria kodi: ya TRA iliyopo kwenye calculator yao kulingana na exchange rate ya dollar siku husika.
Tukumbuke calculator inatoa makadirio, haikupi gharama halisi. Naona calculator inafanya vizuri sana, isipokuwa tunateswa na ukubwa wa ushuru. Halafu kuna magari mengi hayapo kwenye calculator ya TRA, na hata ukijaza fomu kuwataarifu, hawayaongezi.
Mkuu, msaada kwenye tuta kidgo kuhus toyota alphard.Bill of Lading inaweza isiweke thamani ya gari, Invoice ndio inaonyesha thamani ya gari.
Bill of lading hii inaonyesha Nani ni mmliki wa gari na hii ni kama risiti ya kuchukulia mzigo wako melini na kufanya clearing.
TOYOTA VOLTZ
Cif = Tshs 6,891,000
Ushuru = Tshs 7,048,000= 13,039,000
Handling = $7*12.348 = $86.436+ 18% vat = $102
Corridor levy = $0.3*12.348 = 4 + 18% vat = $4.72
Wharfage = 1.6%*2,976 = $47.616
= $155 = Tshs 364,000
Pllus agency fee 200,000
= Tshs 564,000
13,039,000 + 564,000
= Tshs 13,603,000
(Hapo hadi kuitoa bandarini na kuwa mikononi mwako, bima haijajumuishwa)
Na labda kama budget inakua imebana kwa sababu za wingi wa kimajukumu
Unaweza kuiagiza gari hii kupitia Semsella ENTERPRISES
Badala ya kulipia 13,603,000
Unalipia 10,202,250 tu
Gari ikifika, unakabidhiwa
3,400,750 iliyobakia unaimalizia kwa instalment
Ya muda wa miezi 7
Kila mwezi 486,000
Instalment zinaanza mwezi mmoja baada ya kukabidhiwa gari lako.
Semsella Enterprises/ecarstanzania
P.o.box 63178, Dar es salaam
Shekilango, nhc plot number 242
Block number 1,1F
Call/text/Whatsapp text us 24/7
+255745229947
hivi calculator ya TRA haifanyi kazi hadi tuulize kienyeji!?
nilitegemea jamaa aweke link ya hicho kikokotoo
Sent using Jamii Forums mobile app
Mbona inaeleweka mkuuCalculator ya tra majanga
Utaniambiaje cc 2500 and above ....
Nitaendelea..!
Halafu bado mtu anajiuliza kwanini wanawake wanavutiwa na wanaume wenye magari hata kama ni Malaya. Jibu lipo kwenye uthubutu wa kulipia gharama kama hiziT1986MCK,
Habari Mck,
Kwa mujibu wa TRA calculator
Ushuru wa gari yako ni 11,029,645.19
Na bei ya kuifikisha gari hadi bandari ya Da es salaam, kwa sawa sawa na screenshot yako ni 10,742,976.
11,029,645.19 (Ushuru)
10,742,976 (CIF)
Inakuwa : Tshs 21,772,621.19
Handling ni $7 jumlisha VAT (18%) per cbm (cubic meters)
Ile gari ina 14.621 CBM
Kwahiyo unafanya $7*14.621 = $104 plus VAT (18%)
$122.72
Kwahiyo handling inakua $122.72
CORRIDOR LEVY ;
$0.3 plus vat per cbm
$0.3*14.621 = $5 + 18% VAT = $5.9
Kwahiyo Corridor levy inakua $5.9
WHARFAGE :
Hii huwa ni 1.6% ya thamani ya cif
Cif value ya gari yako ni $4,640
$4,640*1.6% = $74.24
Kwahiyo wharfage ni $74.24
TUJUMLISHE
Handling = $122.72
Corridor levy = $ 5.9
Wharfage = $74.24
= $202.86
Ukichange kwa TZS inakua Tshs 476,000
Jumlisha agency fee (200,000)
Inakuwa Tshs 676,000
USHURU NA GHARAMA ZA KULETA HII GARI TULISEMA JUMLA NI
Tshs 21,772,621.19
Kwahiyo Tshs 21,772,621.19 jumlisha 676,000
Inakuwa TSHS 22,449,000 (Hiyo ndiyo budget kamili ya kumiliki hilo gari, yaani hadi kuwa nalo mikononi. Bima haijajumuishwa)
maninaHao ndo TRA. Wameamua.View attachment 1200340View attachment 1200342
Mkuu nakupongeza sana kwa elimu unayoendelea kutoa. Nna maswali mawili:Habari za muda huu,
Pamekuwa na thread nyingi sana za watu kuomba ushauri/ elimu hasa kwenye suala zima la budget halisi/ kamili ambayo mtu anahitaji kuwa nayo kuweza kumiliki gari.
Kwa bahati mbaya, wengi wamekuwa wakipewa gharama kubwa tofauti na uhalisia hiyo yote kwasababu hawajui. Nimeona ni vyema tukafungua huu uzi, Na mimi nimeamua kujitolea kutoa elimu hiyo kwa kadri ya uzoefu wangu.
Naamini si mimi tu ninayefahamu, bali wapo wengine pia, lengo ni kusaidia wote wajue gharama halisi wanazotakiwa kulipia kuweza kumiliki gari.
Nitakuwa hapa kukusaidia mahesabu halisi ya ushuru na gharama zote za bandari unazotakiwa kulipia kwacajili ya kuweza kumiliki gari lako.
NOTE:
Hakikisha unapouliza, unakuwa na mfano halisi wa gari husika ili uweze kupata hesabu halisi ambazo sio za kufikirika. Mfano, unaulizia bei ya Toyota IST, kama gari hiyo labda umeiona mtandao fulani wa kuuza magari (be forward, enhance etc), unanipatia link tu ya gari husika, kisha nakusaidia kuipigia mahesabu halisi.
Kinyume na hapo, yatakuwa ni mahesabu ambayo sio halisi (ya kufikirika)
Ahsante, naamini na wengine wenye uelewa/ufahamu watajumuika hapa kwa ajili ya kusaidia wanaohitaji kujua gharama halisi za ushuru na gharama za bandari wanazohitaji kulipia kwa ajili ya magari yao.
Karibu, tusaidiane!
Inspection-353000Mkuu nakupongeza sana kwa elimu unayoendelea kutoa. Nna maswali mawili:
1. Nimeagiza kagari kadogo Mazda Verisa ya 2006 cc 1500 bei mpaka kanafika dar ni kama USD 2000. Nimecheki kodi TRA ni kama 5.3m. Cha ajabu jamaa wananiambia niandae 1.4m ya clearance, sasa kufuatana na maelezo yako hapa nimebaki nashangaa. Hiyo hela yote itakua ni ya nini?
2. Je, kama nimeshaagiza gari na nimeshachagua agent wa clearing, naweza kumbadilisha?
Asante.