Kaamua kutokuoa

abdalah Kelenge

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
266
Reaction score
203
Najua mko busy sana kwa shughuli but kuna binamu yangu mmoja kahitimu university mwaka juzi baada ya hapo amepata kazi.

Sasa hutaki kabisa story za wanawake pia tangu asome hana legacy yeyote hata kwa marafiki kuwa na mahusiano na mwanamke yeyote.

Kwa sasa yupo vizuri anapokea mshahara wa laki 9 anamwaga radhi baa akitoka job, hatakagi story na wasichana, wamemkalia hadi kikao cha ukoo Jamaa kagoma, wamemuuliza jogoo hawaki? Anasema hataki kujua.

Anadai ataishi single mpaka mauti sasa sijui anatatizo gani.

Naombeni ushauri wenu wa kitheolojia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maisha murua kabisa hayo, Sasa hivi wanawake ni pasua kichwa tu! Ila mwambieni akumbuke kujenga! Ili asisumbuliwe kodi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Amechagua maisha yake, hata hivyo kuliko kunywa pombe tu fikiria kwamba juhudi zote za utafutaji unamtafutia nani? Acha photocopy yako hapa duniani kwa ukumbusho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Teh teh teh huyo jamaa itakuwa alitenda vibaya sana na hivi viumbe hatari.


Kweli jamaa si wa kisport sport
 
Kwani kabla ya hapo alishawahi kuwa na mwenzio labda?
 
Hivi kuwa na mwanamke ni lazima!? Mwache jamaa afurahie maisha yake!!
 
Jamii inapokulazimisha uishi itakavyo sio upendavyo... Mwacheni, fanyeni yenu, kwani yameisha? Mnadhani kila mmoja anaweza kumudu ubongo wa mwanamke? I hate this
 
Hivi kwani ni lazima kuoa..

Jamii muda mwingine ndio chanzo kikubwa cha ndoa nyingi kuwa kwenye migogoro.. mtu kama huyu hataki kuoa, ni mtu mzima mwenye uhuru wa kufanya maamuzi yake. Eti familia inamkalisha kikao kwa nini haoi..

Akioa halafu akimtesa mke mtamlaumu?

Sio wote waliumbiwa kuoa au kuolewa..
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…