JWTZ yafanya kufuru Ngara.
Wanajeshi wa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya ya Ngara, kata ya Mrusagamba wamewapiga vibaya wananchi 17 wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa madai kuwa wamekata bomba ya maji yanayopeleka maji Jeshini.
Kipigo hicho kimewakumba wananchi wa vitongoji vya Nyawela na Runyago ambao wako karibu na eneo ambalo bomba hilo limekatwa. Viongozi wa CCM kata ya Mrusagamba walipeleka majina ya wanachama wa Chadema na Viongozi wa kata hiyo kwa maafisa wa jeshi holo na bila uchunguzi wowote wananchi hao walianza kupewa mkongoto ambapo baada ya taarifa kufikia DAS, aliwapigia simu nao kusitisha kipigo na kuwabeba mzobemzobe hadi kituo cha polisi Mrusagamba ambako walifunguliwa mashtaka na kuzuiwa dhamana.
Jana Jumatatu jioni, walisafirishwa mpaka kituo cha polisi Benako ambako waliachwa hapo wala hawakufikishwa kituo kikuu cha polisi Ngara mjini. Pia dhamana zao zimezuiliwa.
Swali: Je bomba moja laweza kukatwa na watu 17? Je Tanzania inaweza kuendeshwa kwa mabavu kiasi hiki? :angry:
Maoni: Vurugu nchi hii zitaletwa na CCM
Ewe mwananchi chukua hatua kulinda amani ya nchi hii.
Wanajeshi wa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) katika wilaya ya Ngara, kata ya Mrusagamba wamewapiga vibaya wananchi 17 wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa madai kuwa wamekata bomba ya maji yanayopeleka maji Jeshini.
Kipigo hicho kimewakumba wananchi wa vitongoji vya Nyawela na Runyago ambao wako karibu na eneo ambalo bomba hilo limekatwa. Viongozi wa CCM kata ya Mrusagamba walipeleka majina ya wanachama wa Chadema na Viongozi wa kata hiyo kwa maafisa wa jeshi holo na bila uchunguzi wowote wananchi hao walianza kupewa mkongoto ambapo baada ya taarifa kufikia DAS, aliwapigia simu nao kusitisha kipigo na kuwabeba mzobemzobe hadi kituo cha polisi Mrusagamba ambako walifunguliwa mashtaka na kuzuiwa dhamana.
Jana Jumatatu jioni, walisafirishwa mpaka kituo cha polisi Benako ambako waliachwa hapo wala hawakufikishwa kituo kikuu cha polisi Ngara mjini. Pia dhamana zao zimezuiliwa.
Swali: Je bomba moja laweza kukatwa na watu 17? Je Tanzania inaweza kuendeshwa kwa mabavu kiasi hiki? :angry:
Maoni: Vurugu nchi hii zitaletwa na CCM
Ewe mwananchi chukua hatua kulinda amani ya nchi hii.