JWTZ wavamia kituo cha FFU na kukisambaratisha

JWTZ wavamia kituo cha FFU na kukisambaratisha

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,764
29th April 2014

Kundi la wanajeshi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanadaiwa wamevamia kituo cha Polisi wa Kutuliza Ghasia (FFU) kilichopo Kwa Mrombo na wanadaiwa kutembeza mkong'oto kwa askari kadhaa.

Baadhi ya wanajeshi wanadaiwa kukamatwa, ingawa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, alipotakiwa na NIPASHE kuzungumzia tukio hilo alikanusha.

"Hakuna tukio kama hilo, wewe uliona wapi watu wa serikali wanapigana," alihoji Kamanda Sabas na kuongeza: "Sisi tulikuwa kwenye vikao vyetu vya kawaida.

Hata hivyo, msemaji wa JWTZ, Luteni Kanali Eric Komba, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo wakati akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana jioni.

Hata hivyo, alisema polisi na JWTZ wanafanya uchunguzi wa tukio hilo na taarifa zikishawasilishwa makao makuu watatoa taarifa.

Lakini baadhi ya watu walioshuhudia tukio hilo walisema tukio hilo lilitokea majira ya saa tano au sita asubuhi jana, baada ya wanajeshi kuvamia kituo hicho kwa nyakati tofauti.

Inadaiwa wanajeshi hao walikuwa kati ya 50 hadi 60 hivi na haikufahamika mara moja walikuwa wametokea kambi gani ingawa baadhi ya watu walidai walitokea Monduli.

Shuhuda mwingine alisema aliwaona wanajeshi wanne wakiingia kwenye lango kuu la kuingilia kituo hapo na kutembeza kichapo kwa askari aliyekuwapo.

Hata hivyo, habari zingine zinasema hakuna polisi aliyepigwa na hakuna mwanajeshi aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Baadhi ya wakazi jirani na eneo hilo walisema waliwaona kundi la wanajeshi wakiwa katika eneo hilo na wengine wakikimbilia kwenye mashamba.
 
"Wapigwe tu...na mimi nasema wapigwe tu Tumechoka"!... Long Live Mugabe broda from another mother...
 
Hao ffu wapigwe tu maana wameoea kuwapiga wananchi bila kosa lolote nao lazima waonje radha ya kipondo nasema WAPIGWE TU maana tumechoka.

BACK TANGANYIKA
 
Acha FFU wapewe mambo! Eeeh wamezoea kupiga kama bosi wao alivyo watania nao wakaachia masikio, sasa bosi wa pinda naye katoa amri kwa wale waliko juu ya askari wa pinda!

Haya yote yanaweza kuhusishwa na maneno ya viongozi wa serikali wanayotoa bila kufikiria madhara ya maneno yao kwa umma! Sasa ni Mwamunyange Vs IGP ......!

Siasa hizi.... eeh mola wangu!
 
Ile dhambi ya wapigwe tu haitaishia hapo, itaingia hadi kwa hawa watawala wetu ndiyo watajua madhara ya kauli zao.
 
Hao ffu wapigwe tu maana wameoea kuwapiga wananchi bila kosa lolote nao lazima waonje radha ya kipondo nasema WAPIGWE TU maana tumechoka.

BACK TANGANYIKA

Wananchi tujiandae kujihami, maana baada ya kichapo kutoka kwa wajeda hao, watakuja kumalizia hasira kwetu raia. Mtaona ama kusikia muda si mrefu.
 
Viongozi wanafikiria kwa ma------... Tumia kichwa kufikiri siyo kutumia miguu! Miguu kazi yake ni kudance....!
 
duh! kumbe neon ma-sa-buri JF moderator inayafahamu!
 
Hayo ni mazoezi ya kudhibiti watu wa s3
Wamefanyia kwa wenzao
Hatuogopi wala kutishwa hata wauwane wenyewe kwa wenyewe
 
Hizi ni athari za kukaa bila active combat matokeo yake mizuka ya shari inapanda hovyo, wapeleke hicho kikosi South Sudan ama CAR huko.
 
Yale yale usichopenda kutendewa ,usimtendee mwenzako,maana siku ya kutendwa huijui.Poleni FFU mjifunze kutokana na makosa yenu.Inawezekama walijua ni raia wa kawaida kumbe matatizo.
 
Hao ffu wapigwe tu maana wameoea kuwapiga wananchi bila kosa lolote nao lazima waonje radha ya kipondo nasema WAPIGWE TU maana tumechoka.

BACK TANGANYIKA
nami nasema waendelee kupigwa tu,wakiwamaliza ffu wawaanzie kazi matrafiki.
 
Hiiii habari haiwezi kuwa Kweli unaposema wanajeshi 50 kuvamia kambi ya FFU si kitu cha kawaida ingekuwa big news leo .

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
1. Kituo cha polisi FFU sijawahi kukiona Tanzania hii.

2. Tukio kama hilo lingetokea kama linavyotanabaishwa kwa hakika kusingehitajika kumpigia kamanda simu. Ingekuwa ni vita

3. Askari wa FFU wanaishi kambini...WOTE...or tuseme wanatakiwa wote waishi kambini (hivyo kiuhalisia zaidi ya 80% yao wanaishi kambini)...sasa hao JWTZ wa kwenda kuanzisha vita kambi ya FFU aisee. sijui...labda waende battalion na silaha za nguvu tena si hivi hivi.

4. Sipendi vita kati ya vyombo vya ulinzi na usalama. Natumai hii habari ni rumor tu. au ni ugomvi wa maaskari wawili tu na sio chuki baina ya wengi.
 
Back
Top Bottom