JWTZ ni kwamba mnafanya maigizo ama?

JWTZ ni kwamba mnafanya maigizo ama?

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Wakati dunia inazungumza kuhusu vita vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu, jeshi la Tanzania bado limebaki nyuma likifanya mazoezi yasiyo na tija.

Badala ya kuwekeza kwenye zana za kivita za kisasa na mbinu za kijeshi zinazolingana na zama hizi, mara nyingi wanajeshi huonekana wakitumia muda katika nyimbo za hamasa, gwaride, na mazoezi ya heshima.
=============
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kupitia Brigedi ya Faru, limehitimisha zoezi la medani Pima Uwezo 2025 lililofanyika mkoani Shinyanga.

Akimwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda, katika kilele cha kuhitimisha zoezi hilo, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, Meja Jenerali Fadhili Nondo, amewataka maafisa na askari kuwa tayari nyakati zote kulinda mipaka ya nchi kwa njia ya ardhi, anga na maji dhidi ya uvamizi wa adui.

"Mazoezi ni sehemu ya kutufanya wanajeshi tuwe tayari nyakati zote katika kutekeleza majukumu ya ulinzi wa taifa. Hivyo, wakati wa amani tunapaswa kuvuja jasho jingi ili wakati wa vita tutekeleze majukumu yetu kwa ufanisi mkubwa," amesema Meja Jenerali Nondo.

Aidha, amesema mazoezi hayo yataendelea kufanyika kwa nyakati na maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa na askari wa JWTZ.

Kwa upande wake, Kamanda wa Brigedi ya Faru, Brigedia Jenerali Gabriel Kwiligwa, amesema zoezi hilo limefanyika kwa siku 12 likiwa na lengo la kupima utayari wa vikundi katika kukabiliana na matishio mbalimbali ikiwemo ugaidi, uvamizi kutoka ndani na nje ya nchi, pamoja na kuzuia uhamiaji haramu.

Zoezi la medani Pima Uwezo 2025, lenye kaulimbiu isemayo “Pima Uwezo, Kaa Tayari Tuilinde Tanzania”, pia limeshirikisha askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo)

 
Wakati dunia inazungumza kuhusu vita vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu, jeshi la Tanzania bado limebaki nyuma likifanya mazoezi yasiyo na tija. Badala ya kuwekeza kwenye zana za kivita za kisasa na mbinu za kijeshi zinazolingana na zama hizi, mara nyingi wanajeshi huonekana wakitumia muda katika nyimbo za hamasa, gwaride, na mazoezi ya heshima.


View: https://www.facebook.com/share/v/1CQPNDrvaG/

Hali hii inawafanya Watanzania wengi kuhoji kama kweli jeshi linaweza kulinda taifa endapo tishio kubwa kama Vita lingetokea.

😂wewe unaota au ?
 
Kwa nn msisubiri kampeni zipite, au fanyeni kimya kimya mana hizo ni kazi zenu za kila siku. Sasa Kipindi hiki cha kampeni, hayo ni kuleta siasa jeshini kutangaza majukumu yenu
 
Jeshi halina Kitengo cha kulinda uchumi wa nchi lenyewe linalinda mipaka tu jeshi inatakiwa kua na Kitengo cha kulinda uchumi wa nchi na rasilmali maslahi ya icho Kitengo inabidi kiwe cha kificho ni kwa maslahi Rasi wa nchi akiingia mikataba mikataba mibovu icho Kitengo kikangudua kinamweka pembeni Rais kwa maslahi ya nchi mambo ya kulinda mipaka tu wakati rasilmali za nchi zinaisha hiyo mipaka itakua haina maana
 
mkuu umewahi kupita ata depo la mujibu wa sheria
Ndio tatizo la waafrika! Mkishikwa pabaya mnaanza kuuliza maswali off topic!? Ukienda Depo ni wapi wanapozungumza kuhusu utii wa chama!? Ndio maana nikakwambia ni Jeshi la Wananchi sio Jeshi la Mwenyenchi
 
Watakuja kukuambia jwtz ni hatari na silaha za kisasa wanazo na mafunzo wanayo ila hawaweki hadharani...😎
 
Jeshi halina Kitengo cha kulinda uchumi wa nchi lenyewe linalinda mipaka tu jeshi inatakiwa kua na Kitengo cha kulinda uchumi wa nchi na rasilmali maslahi ya icho Kitengo inabidi kiwe cha kificho ni kwa maslahi Rasi wa nchi akiingia mikataba mikataba mibovu icho Kitengo kikangudua kinamweka pembeni Rais kwa maslahi ya nchi mambo ya kulinda mipaka tu wakati rasilmali za nchi zinaisha hiyo mipaka itakua haina maana
Ninaafiki jeshi letu lifanye paradigm shift kwa kulinda mipaka ambayo dhana pana ni pamoja na raslimali za nchi dhidi ya maadui wa ndani na nje ya nchi. Mipaka ni uchumi,watu,ardhi na teknolojia ndani, vilindwe kwa wivu mkubwa.
 
Nenda pale Lugalo ukawape haya maoni yako. Jeshi ni waungwana watakusikiliza.
 
Hawa mpaka karne hii ya 21 eti bado wanajisifu kwa kuzindua mtambo wa kuponda kokoto.
 
Hili jeshi ingekuwa vita vina ligi nchi yetu ingekuwa daraja la tatu.
 
Wakati dunia inazungumza kuhusu vita vya kisasa vinavyotumia teknolojia ya hali ya juu, jeshi la Tanzania bado limebaki nyuma likifanya mazoezi yasiyo na tija.

Badala ya kuwekeza kwenye zana za kivita za kisasa na mbinu za kijeshi zinazolingana na zama hizi, mara nyingi wanajeshi huonekana wakitumia muda katika nyimbo za hamasa, gwaride, na mazoezi ya heshima.
=============
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kupitia Brigedi ya Faru, limehitimisha zoezi la medani Pima Uwezo 2025 lililofanyika mkoani Shinyanga.

Akimwakilisha Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob Mkunda, katika kilele cha kuhitimisha zoezi hilo, Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Nchi Kavu, Meja Jenerali Fadhili Nondo, amewataka maafisa na askari kuwa tayari nyakati zote kulinda mipaka ya nchi kwa njia ya ardhi, anga na maji dhidi ya uvamizi wa adui.

"Mazoezi ni sehemu ya kutufanya wanajeshi tuwe tayari nyakati zote katika kutekeleza majukumu ya ulinzi wa taifa. Hivyo, wakati wa amani tunapaswa kuvuja jasho jingi ili wakati wa vita tutekeleze majukumu yetu kwa ufanisi mkubwa," amesema Meja Jenerali Nondo.

Aidha, amesema mazoezi hayo yataendelea kufanyika kwa nyakati na maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo maafisa na askari wa JWTZ.

Kwa upande wake, Kamanda wa Brigedi ya Faru, Brigedia Jenerali Gabriel Kwiligwa, amesema zoezi hilo limefanyika kwa siku 12 likiwa na lengo la kupima utayari wa vikundi katika kukabiliana na matishio mbalimbali ikiwemo ugaidi, uvamizi kutoka ndani na nje ya nchi, pamoja na kuzuia uhamiaji haramu.

Zoezi la medani Pima Uwezo 2025, lenye kaulimbiu isemayo “Pima Uwezo, Kaa Tayari Tuilinde Tanzania”, pia limeshirikisha askari wa Jeshi la Akiba (Mgambo)

Jeshi letu lina hadhi ya mgambo ukilinganisha na majeshi ya Duniani
 
Back
Top Bottom