Juu ya tuhuma kwa Zitto na kundi lake kutoka kwa Mamuya...

Status
Not open for further replies.
Wapenda haki wameshamjua ben, he is full of hates.

ZZK, tulikushauri hukushaurika, nadhani now utaijua vyema CDM
 
This is hard to believe.....


Ila ipo siku ukweli wote utamwagwa hadharani.....

Wengine tulishaonya ila tukabezwa...!!
 
Peleka agenda ya kumfukuza muone kivumbi! Zitto ni CDM na CDM ni Zitto. Vita vya panzi hivi ......
Huyu ikidhibitika kakisaliti chama hana chake hakuna aliye juu ya chama maandishi yaani kanuni ndio na taratibu zilizopo kwenye katiba ndizo zinazoendesha chama hapa sio magambani huko kwenu ambapo umaarufu na fedha za watu ndivyo vinavyoendesha chama cha magamba kibaraka wenu kajulikana kazi mnayo.
 
Ben saanane we ni jasiri kama Godbless Lema na mwenye msimamo kama Julius Malema.

Long live my hero Ben na vizazi vitakukumbuka kwa ujasiri wako huu na hakika wewe Ben ndiye THE BEST YOUNG POLITICIAN OF 2012.

bravo kamanda.
 
Nakuomba sana Mh Zitto usijibu hii hoja endelea na ukimya hivo hvo ili kulinda heshima yako na viongozi wezio. Hivi ni kwa nini vijana wa Chadema waliowengi wako so harsh? Lazima mkubali kuwa Mh Zitto pamoja na mapungufu kama binadamu ambayo kila mtu anayo anamchango na heshima kubwa katika nchi hii, Sidhani kama anatakiwa kubezwa, kuzarauliwa,kutukanwa kama mnavyofanya baadhi ya wanajamvi.
Tatizo la vijana wengi wliomo humu na wenye siasa za kuchafuana,kwanza wanaonekana hawana kazi, kazi zao nikupost humu asubuhi mpaka jioni. Hawataki kukosolewa na kujifunza kutoka kwa wangine, wanataka uwasapoti katika misimamo yao na kama utakuwa tofauti nao basi wewe ni mpinzani wao. na utatukanwa na kuzarauliwa na maneno tofauti tofauti machafu.

Rai kwa Viongozi wa chama, Hawa vijana wengi wanafanya hivi kwa maslahi yao binafsi,hakuna ukombozi wala ukamanda hapa ndio maana wanarubunika kirahisi. Sipati picha itakuwaje 2015 kwa wale watakao taka uongozi na wakakosa watafanyaje. Chadema andaeni vijana waadilifu, walipeni vizuri wawasaidie katika kujenga chama. Na hili swala la Usaliti and the like mkalimalize huko kwenye vikao vyenu.

kama tuhuma hizi zilizotolewa zitakuwa za kweli kupitia ushahidi walionao kina ben, huyu ni lazima aombe radhi, no way...tena aombe radhi kwa wenye chama yaan umma, kwenye kikao tu haitoshi, aanze kwenye kikao, akishasameheka ndo arudi kwa umma. usaliti wa ukubwa huu hauwezi kusahaulika hiv hiv..wewe hujui tu huyu zito ndo alitu-inspire weingine hadi tukajiunga kwenye movement halaf leo anataka kusaliti uwekezaji woooooooote wa hali na mali tuliofanya eti tumwangalie tu.....no way, msaliti ni msaliti tu hata kama angekuwa na mchango gan...
 
.
Sisi wapenzi na wafurukutwa wa wanamageuzi wa kweli hatutapepesa hata ukupe wa jicho letu kumwita msaliti yeyote jina lake la usaliti. Hata kama ni malaika kutoka mbinguni atakaesaliti harakati za kumkomboa mnyonge tutamlaani mbele ya watu wote. Chadema sio TLP au NCCR ya zama za mrema. Hii ni taasisi iliyojengwa kisomi na inayogusa maisha ya watu kutoka ngazi ya kaya mpaka taifa.
.

Haya ndiyo matatizo ya kuvaa magwanda wakati wa kiangazi. Hapo kwenye malaika nenda ukatubu kwa muumba wako. Ni msomi gani huyo unayemtaja hapo? Mbowe au 'DR' wa 'ukweli'?
 
na sisi wa zenji tunasema ulipoingilia msumari ndipo hapo hapo utakapotokea...daadake!! mnatuletea mambo ya ughalula karne hizi??!! waone kwanza!! nyie viiiiip!??

Watu Lamu wasema kuzipa tundu la msumari shurti paingie kitu!!!

Chama
Gongo la mboto DSM
 
.
Sisi wapenzi na wafurukutwa wa wanamageuzi wa kweli hatutapepesa hata ukupe wa jicho letu kumwita msaliti yeyote jina lake la usaliti. Hata kama ni malaika kutoka mbinguni atakaesaliti harakati za kumkomboa mnyonge tutamlaani mbele ya watu wote. Chadema sio tlp au nccr ya zama za mrema. Hii ni taasisi iliyojengwa kisomi na inayogusa maisha ya watu kutoka ngazi ya kaya mpaka taifa. Tutakilinda chama na viongozi wote waandamizi kwa nguvu zote na yeyote aliyejiunga upande wa mafisadi wachache wanaoitafuna nchi kwa kueneza propaganda za kuwanusuru wachawi wote na mkono wa umma, tutamshughulikia kulingana na usaliti wake. Mungu ibariki chadema na wapambanaji wote wanaoitetea haki ya mnyonge iliyodhulumiwa.
.

aaaaaaaamen...
 
Baada ya ZZK,Dr Kitilla Mkumbo atakaefuata ni Prof Safari na Tundu Lissu ili wenye chama wabaki wenyewe na wafanye ya kwao.
 
Zitto Kabwe
Kabila; MUHA
Dini; Islam
Kosa ; KUTANGAZA KUGOMBEA URAIS
Hapo kaka kweli unategemea vijana hawa wa hapa JF watakuachia uwe kiongozi wao ndani ya chadema.
Kaka mie sio mnafiki, hivyo ningependa nikupe ushauri mmoja tu kwa faida ya wapenda maendeleo ya Tasifa letu.
Nakuomba ndugu yangu uachane na chadema kwa sababu watakuumiza kichwa bure.
Tanzania inahitaji wanasiasa hodari na wapiganaji kama wewe, hivyo ningekushauri ujiunge na CCM upambane kutoka ndani ya CCM kama vile wenzako akina Deo filikunjombe wanavyofanya na utafanikiwa.
Mimi nimetoka Chadema na ninayajua mengi mazito ambayo kama nikiyaongea hapa nazani itakuwa balaa zaidi.
Kuna wengi viongozi wa chadema hawakutaki na mimi binafsi niliwahi kuambiwa nisije kupoteza muda kuwasiliana na wewe kwa sabau ni nyoka. Hilo vumbi linalotimka huko Chadema ukiendelea kubaki nalo litakusababishia kifua kikuu ndugu yangu.

Jina: Kubenea

Kabila: La Mafia

Dini: Muislamu

Madai- 1. Zitto anatumiwa na unasalama wa taifa: Usalama wa Taifa wavamia CHADEMA | Gazeti la MwanaHalisi

2. Zitto na Rostam Aziz:Zitto ahusishwa na Rostam | Gazeti la MwanaHalisi

3. Zitto kuhujumu wagombea wa CHADEMA kusaidia vyama vingine: Siri za Zitto nje | Gazeti la MwanaHalisi

4. Zitto na vijana wake kutoa rushwa BAVICHA:Masalia ya Zitto yapukutishwa CHADEMA | Gazeti la MwanaHalisi

5. Zitto na NCCR dhidi ya CHADEMA kwa mara nyingine: NCCR kutumika kuvuruga CHADEMA | Gazeti la MwanaHalisi

Kubenea mwislamu mwenzake ambaye anatoka pwani naye anamuonea? Au CCM mnataka kuleta udini, ukabila na ukanda? Ndio maana umerudi kwa magamba wenzio.

Serayamajimbo
 
Aina hii ya watu wapo tangia enzi za Yesu .Yuda Iskarioti alimsaliti Yesu kwa tamaa ya hela,ila kusalitiwa kwa Yesu haikuwa mwisho wa maisha yake bali ni mwanzo wa maisha mapya ya ukombozi,Nandiyo maana kila baada ya ijumaa kuu huja pasaka.
 
Haya ndiyo matatizo ya kuvaa magwanda wakati wa kiangazi. Hapo kwenye malaika nenda ukatubu kwa muumba wako. Ni msomi gani huyo unayemtaja hapo? Mbowe au 'DR' wa 'ukweli'?

Ha ha haaa, mkuu nilikuwa nina stress at least zimepungua...'kweli kuvaa magwanda wakati wa joto ni shida' tupu!
 
Acha kupoteza mda ndugu, narudia tena kusema HUNA jipya la kuiyumbisha chadema,

Tumia hata akili ya kitoto tu mkuu, hivi Zitto aliyekiongozi wa juu Uzandiki wake kwa chama umedhibitiwa na amejitahidi kukigawa chama ameshindwa, je wewe usiye na hata anwani ya kisiasa ndani ya Chadema unaweza kuwa na jipya au pumba tu?

Usipoteze mda hapa, kitengo cha ujasusi cha chadema kinamjua kila mwanachama kuanzia utosi hadi unyayo!

Na wewe ukiwemo, kitengo kinajkujua kuanzia nywele hadi nyayo!

Kaa kimya endelea kufurahia maisha huko CCM,

Ukiendelea kuropoka hapa, na huko ccm watakufukuza bure mkuu!

Intelijensia yetu ni pana haiishii Kinondoni manyanya tu!

I like this confidence Yericko! Tafadhali hakikisheni hivyo ndivyo ilivyo na ndivyo ibakie for our beloved country.
God Bless you guys!
 
Huyu ikidhibitika kakisaliti chama hana chake hakuna aliye juu ya chama maandishi yaani kanuni ndio na taratibu zilizopo kwenye katiba ndizo zinazoendesha chama hapa sio magambani huko kwenu ambapo umaarufu na fedha za watu ndivyo vinavyoendesha chama cha magamba kibaraka wenu kajulikana kazi mnayo.

Hivi hiyo message ya Ben Saanane hamuisomi vizuri, mnaangalia kwenye neno ZITTO tu? Kwa mujibu wa data kutoka ndani ya CDM na Ben pamoja na Yericko, safu yote ya CDM ni vibaraka wa chama tawal:

1) DR Slaa amegoma kurudisha kadi ya CCM kwa vile anataka kutumia kadi yake ile ile akirudi.

2) Zitto ndio hivyo tena mnasema ni Pandikizi pamoja na Dr Kitilla

3) Ben na Bavicha mnasema vibaraka

Sasa nani amebaki hapo? CDM basi itakuwa ni CCM B, Youth wing ambako wanaandalia viongozi wake 'Yosso' kwa ajili ya kujiunga na CCM A when they attain maturity.
 
kinachomzingua bwa'mdogo cha kwanza ndo hicho hapo kwenye red...eti yy ni zaid ya chama, ghalula bana!! kwa sababu anapaa na ungo basi adhani eti yeye ni sana!! nyungo zenu ni huko huko.

cha pili kinchomzingua kijana ni kutaka kuwa juu ya kila mtu, iwe iwavyo...superiority complex kibao. eti nimechangia damu cdm, kwa hiyo kama umechangia damu ndo unataka upae mawinguni au? mzee mtei asemeje sasa? ungejua wewe watu tumetulia tu lakini ukioneshwa kiasi cha damu zetu tulizowekeza ungeshangaa.. kama yako ni glass ya kwangu ni pipa nzima, halafu nimetulia tuliiiiii, wala sijulikani hata ndani ya nyumba kumikumi za magamba. waliochangia damu wanasemega wewe?! cheza kwel wewe zitto.

Kweli mkuu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom