Zing
JF-Expert Member
- Jun 24, 2009
- 1,767
- 470
Ni upungufu lakini labda mapungufu hayo ndo yanachangia maendeleo waliyonayo.
hapa naongelea uelewa wa mambo ya kawaida, mambo ya kimataifa na kitafifa. elimu zetu tanzania ni ukweli kuwa zinatuwezesha kuwa na uelewa mkubwa wa jiografia, lugha, sayansi, historia . n.k. Labda hili ndilo linafanya tuwe wanasiasa, wanasayansi na wataalamu wa wenye longo longo.
nadhani elimu za wenzetu kama USA wanawai kuspecialize mapema na hivyo wengi wanakuwa wana uelewa wa mambo fulani kwa sana na wanakuwa hawana uelewa hata chembe wa mambo mengine yanayohusu jamii. Utaona mfano wa yule mgombea mwenza wa chama cha republican marekani aliyedhani afrika ni nchi.
Je kuna haja ya kubadilisha mitaala na kuanza kuspecialize mapma kwenye taaluma zetu badala ya kuwa na general education kwa muda mrefu?
Last edited by a moderator: