Jumuiya yetu ya Kanisa Katoliki imevunjika sababu ya michango kuwa mingi

bushland

JF-Expert Member
Mar 6, 2015
7,016
4,961
Wanajamii sijui tunaelekea wapi katika maisha haya?

Kanisa Katoliki tumezoea kuwa na Jumuiya ndogo ndogo kwa ajili ya kusali pamoja na kushirikiana mambo mbali mbali ndani na nje ya kanisa. Zamani tulizoea kutoa sadaka tu kila tunapokutana katika jumuiya hizi zetu na sadaka hizo hupelekwa kanisani.

Lakini siku hizi mambo tofauti michango imekuwa mingi mno tena michango hiyo huanzia elfu kumi kwa kila kichwa.

Mfano, sisi katika jumuiya yetu msalaba ukilala kwako yani siku jumuiya ikisali kwako unatakiwa utoe shilingi elfu kumi, sadaka iliyopangwa kutolewa kila Jumamosi ni shilingi elfu moja na mia tano kila kichwa, pia kuna mchango wa ujenzi wa kanisa kila mtu elfu 30.

Kuna mchango wa familia ya mtoto Yesu kila mmoja anatakiwa kutoa elfu kumi ili tuitimize laki tatu kwa kila jumuiya, mbali na hiyo kunakuwa na bahasha ya zaka zinakuwepo.

Yaani kwa kifupi kila wiki tunaposali kunakuwa na michango karibu 8 na yote inaanzia elfu kumi.

Tatizo linakuja usipolipa hiyo hela jumuiya inakutenga hadi ulipe madeni yote ndIo unaruhusiwa tena kuingia kwenye jumuiya. Kwa sasa jumuiya yetu imevunjika kwa ajili ya michango kuwa mingi ukizingatia hali halisi ya maisha ya sasa.

Kweli wakristo wenzangu hapa ndipo tulipofikia? Tunaelekea wapi kanisa katoliki la leo?!
 
nyumba za ibada za siku hizi zilizo nyingi ni source of income za wajanja, sasa huwa najiuliza kwani hizi nyumba za ibada si ndio zingekuwa zinaongoza kutusitiri na matatizo yetu, yaani leo ndio zingekuwa zinawatunza mayatima wengi na kuwasomesha, lakini thubutu, seminary zenyewe ada yake kama si mtoto wa kigogo huwezi soma, mkuu wacha wakutengetu ila ukweli juu ya Mungu wako uko moyoni mwako, ila wao walipaswa kukupunguzia mzigo
 
Nyingi tu sitakuwa njiani kufa ... hata huku niliko mimi kanisa limekuwa ni pesa, ni pesa ni pesa. Na kibaya kuna parokia zilizo chini ya mashirika ya wahindi, huko ndio hadi kero. Kama kanisa limeacha kazi ya kuhubiri na badala yake wanaanza kuwa money makers basi tunaelekea kujitoa wengi.
 
Hiyo ni Saccos sasa

Habari ya kumtenga mtu kisa hajachangia michango ni kuhamisha huduma za kiroho na kuwa biashara

Kanuni ya Mungu mmepewa bure toeni bure

Ingawa pia kama washirika tunawajibu wa kuitegemeza kazi lakini isiwe kwa kiwango cha kulazimisha watu mpaka kuwatenga kama wamataifa wafanyavyo bali watu watoe kwa moyo wa kupenda
 
wanajamii sijui tunaelekea wapi katika maisha haya,
kanisa katoliki tumezoea kuwa na jumuiya ndogo ndogo kwa ajili ya kusali pamoja na kushirikiana mambo mbali mbali ndani na nje ya kanisa, zamani tulizoea kutoa sadaka tu kila tunapokutana katika jumuiya huzi zetu na sadaka hizo hupelekwa kanisani.

lakini siku hizi mambo tofauti michango imekuwa mingi mno tena michango hiyo huanzia elfu kumi kwa kila kichwa,
mfano sisi katika jumuiya yetu msalaba ukilala kwako yani siku jumuiya ikisali kwako unatakiwa utoe shilingi elfu kumi, sadaka iliyopangwa kutolewa kila jumamosi ni shilingi elfu moja na mia tano kila kichwa, pia kuna mchango wa ujenzi wa kanisa kila mtu elfu 30,

kuna mchango wa familia ya mtoto Yesu kila mmoja anatakiwa kutoa elfu kumi ili tuitimize laki tatu kwa kila jumuiya, mbali na hiyo kunakuwa na bahasha ya zaka zinakuwepo ,
yan kwa kifupi kila wiki tunaposali kunakuwa na michango karibu 8 na yote inaanzia elfu kumi,

tatizo linakuja usipolipa hiyo hela jumuiya inakutenga hadi ulipe madeni yote ndo unaruhusiwa tena kuingia kwenye jumuiya, kwa sasa jumuiya yetu imevunjika kwa ajili ya michango kuiwa mingi ukizingatia hali halisi ya maisha ya sasa

kweli wakristo nwenzangu hapa ndipo tulipofikia?
tunaelekea wapi kanisa katoliki la leo?
Wewe hujasoma Biblia imeandika siku za mwisho watu watapenda pesa?
 
wanajamii sijui tunaelekea wapi katika maisha haya,
kanisa katoliki tumezoea kuwa na jumuiya ndogo ndogo kwa ajili ya kusali pamoja na kushirikiana mambo mbali mbali ndani na nje ya kanisa, zamani tulizoea kutoa sadaka tu kila tunapokutana katika jumuiya huzi zetu na sadaka hizo hupelekwa kanisani.

lakini siku hizi mambo tofauti michango imekuwa mingi mno tena michango hiyo huanzia elfu kumi kwa kila kichwa,
mfano sisi katika jumuiya yetu msalaba ukilala kwako yani siku jumuiya ikisali kwako unatakiwa utoe shilingi elfu kumi, sadaka iliyopangwa kutolewa kila jumamosi ni shilingi elfu moja na mia tano kila kichwa, pia kuna mchango wa ujenzi wa kanisa kila mtu elfu 30,

kuna mchango wa familia ya mtoto Yesu kila mmoja anatakiwa kutoa elfu kumi ili tuitimize laki tatu kwa kila jumuiya, mbali na hiyo kunakuwa na bahasha ya zaka zinakuwepo ,
yan kwa kifupi kila wiki tunaposali kunakuwa na michango karibu 8 na yote inaanzia elfu kumi,

tatizo linakuja usipolipa hiyo hela jumuiya inakutenga hadi ulipe madeni yote ndo unaruhusiwa tena kuingia kwenye jumuiya, kwa sasa jumuiya yetu imevunjika kwa ajili ya michango kuiwa mingi ukizingatia hali halisi ya maisha ya sasa

kweli wakristo nwenzangu hapa ndipo tulipofikia?
tunaelekea wapi kanisa katoliki la leo?
Binafsi nilishaachana na vituko hivi kitambo!
 
wanajamii sijui tunaelekea wapi katika maisha haya,
kanisa katoliki tumezoea kuwa na jumuiya ndogo ndogo kwa ajili ya kusali pamoja na kushirikiana mambo mbali mbali ndani na nje ya kanisa, zamani tulizoea kutoa sadaka tu kila tunapokutana katika jumuiya huzi zetu na sadaka hizo hupelekwa kanisani.

lakini siku hizi mambo tofauti michango imekuwa mingi mno tena michango hiyo huanzia elfu kumi kwa kila kichwa,
mfano sisi katika jumuiya yetu msalaba ukilala kwako yani siku jumuiya ikisali kwako unatakiwa utoe shilingi elfu kumi, sadaka iliyopangwa kutolewa kila jumamosi ni shilingi elfu moja na mia tano kila kichwa, pia kuna mchango wa ujenzi wa kanisa kila mtu elfu 30,

kuna mchango wa familia ya mtoto Yesu kila mmoja anatakiwa kutoa elfu kumi ili tuitimize laki tatu kwa kila jumuiya, mbali na hiyo kunakuwa na bahasha ya zaka zinakuwepo ,
yan kwa kifupi kila wiki tunaposali kunakuwa na michango karibu 8 na yote inaanzia elfu kumi,

tatizo linakuja usipolipa hiyo hela jumuiya inakutenga hadi ulipe madeni yote ndo unaruhusiwa tena kuingia kwenye jumuiya, kwa sasa jumuiya yetu imevunjika kwa ajili ya michango kuiwa mingi ukizingatia hali halisi ya maisha ya sasa

kweli wakristo nwenzangu hapa ndipo tulipofikia?
tunaelekea wapi kanisa katoliki la leo?
Hoji mapato na matumizi ya hiyo michango kwa viongozi wa kanisa lako sio kulalamikia humu.
 
wadhamini hakuna tujenge kanisa wenyewe ila isiwe too much hiyo michango..ninachopendea michango ya katoliki haiendi kwa mtu mmoja (padri)inaenda kwa kamati husika na kila kitu kinachofanyiwa hiyo Pesa waumini mnakiona na kujua.ata iwe kununulia tofali moja.na Mara nyingi parokia nyingi kwenye kamati waumini wanachagua wale watu matajiri sana .maana ukimchagua masikini tamaa ya Pesa nje nje.anachaguliwa tajiri asio na njaa njaa
 
Back
Top Bottom