PreGE2025 Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania yampongeza Rais Samia kwa kuonesha ukomavu wa kisiasa

PreGE2025 Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania yampongeza Rais Samia kwa kuonesha ukomavu wa kisiasa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,436
Reaction score
5,233
Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania imempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuonesha ukomavu wa kisiasa, huku ikimuomba kwa heshima asamehe kauli za matusi na udhalilishaji zinazotolewa na baadhi ya vijana kutoka nchini Kenya kupitia mitandao ya kijamii.

Akizungumza jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Taifa, Sheikh Alhad Mussa Salum, amesema licha ya lugha zisizofaa zinazomlenga Rais Dkt. Samia, bado wanaamini msamaha ndio msingi wa kudumisha undugu na ujirani mwema kati ya mataifa hayo mawili.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Sheikh Alhad ametoa wito kwa viongozi wa dini nchini Kenya kushirikiana na Jumuiya hiyo katika kuwaelimisha na kuwaongoza vijana wa mataifa yao kuheshimiana, kuepuka lugha chafu, na kudumisha uhusiano mwema uliojengwa kwa misingi ya ujirani na undugu kwa muda mrefu.

 
Halafu haya mambo yanayohusu uhusiano wa nchi na nchi nafikiri ni vyema wawepo watu rasmi wa kuyazungumzia sio tu kila limtu linaropoka na matakataka yanaisemea nchi
 
Pongezi ufanya aliyepongezwa kufurahia

Habari nzuri 👏🏽👏🏽👏🏽


Kazi iendeleeee
 
km vile ambavyo nabii tito hawakilishi ukirisho, bas huyu pia hawakilishi uislam.
 
Wasakatonge on air.
Kazi ni kipimo cha utu
 
Watu wanatekwa na kuuawa nchini, hawajawahi kutoa kauli yoyote kwa Rais, ila wakenya wasamehewa kwa kuwa Rais hana ubavu wa kuwateka wala kuwabambikiza kesi ya uhaini.
 
Shehe njaa kali sijui anakadi namba ngp ya ccm.
Ndg zetu wakenya tunawasihi waendelee kukazia hapohapo, wasiachie!!.
 
Ushauri wangu huyu mwamba tusimparamie wala kumrarua, muoneeni huruma, angalieni hata rangi yake na mwili wake, ni wazi kwamba ipo shida inamtafuna. Na kama kwenye kikao hicho chai haikuandaliwa ujue ndio siku imepita
 
Back
Top Bottom