albuluushiy
JF-Expert Member
- Oct 2, 2013
- 1,404
- 687
HONGERENI ACT - WAZALENDO......
Mwanademokrasia yeyote hapaswi kukasirika pale ambapo chama kipya kinaanza kazi zake huku kikionesha mambo kadha wa kadha mazuri na ya kuigwa na vyama vilivyopo.
Japokuwa chama hiki kipya pia kina mambo lukuki ya kuiga na kujifunza kutoka kwa vyama vikongwe. Kwa uzoefu wangu wa siasa, huwezi kukilinganisha chama hiki kipya na vyama utitiri ambavyo hata ofisi zao hazijulikani ziko wapi na lini wanafanya mkutano mkuu au vikao vya maamuzi.
Ifikie wakati tuwe na sheria ambayo inavilazimu vyama fulani kujifuta moja kwa moja vikishindwa kupata ushindi kiasi fulani kwenye uchaguzi. Nchi inahitaji kuwa na vyama vichache vyenye malengo ya kuleta ushindani wa kweli, Mimi ni muumini wa ushindani na nawakaribisha ACT kwenye ushindani wa kidemokrasia.
Njooni mjenge hoja na tushindanishe sera. Naamini kuwa chama chenu ni platform ya kisiasa kama zilivyo zingine.
J. Mtatiro,
DSM.
Mwanademokrasia yeyote hapaswi kukasirika pale ambapo chama kipya kinaanza kazi zake huku kikionesha mambo kadha wa kadha mazuri na ya kuigwa na vyama vilivyopo.
Japokuwa chama hiki kipya pia kina mambo lukuki ya kuiga na kujifunza kutoka kwa vyama vikongwe. Kwa uzoefu wangu wa siasa, huwezi kukilinganisha chama hiki kipya na vyama utitiri ambavyo hata ofisi zao hazijulikani ziko wapi na lini wanafanya mkutano mkuu au vikao vya maamuzi.
Ifikie wakati tuwe na sheria ambayo inavilazimu vyama fulani kujifuta moja kwa moja vikishindwa kupata ushindi kiasi fulani kwenye uchaguzi. Nchi inahitaji kuwa na vyama vichache vyenye malengo ya kuleta ushindani wa kweli, Mimi ni muumini wa ushindani na nawakaribisha ACT kwenye ushindani wa kidemokrasia.
Njooni mjenge hoja na tushindanishe sera. Naamini kuwa chama chenu ni platform ya kisiasa kama zilivyo zingine.
J. Mtatiro,
DSM.