Julius Malema anataka ukahaba uhalalishwe

Julius Malema anataka ukahaba uhalalishwe

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Kiongozi wa EFF Julius Malema ameitaka serikali kuharamisha ukahaba. Akizungumza na wafuasi wa chama katika maandamano ya Siku ya Wanawake huko Mpumalanga, Malema alisema wafanyabiashara ya ngono wanastahili kupata ulinzi na vyombo vya sheria, ikiwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kufungua kesi dhidi ya wabakaji au aina nyingine za unyanyasaji bila kudharauliwa na polisi.
images (49).jpeg

"Serikali lazima ihalalishe ukahaba. Ukahaba ni taaluma kongwe zaidi duniani. Unaweza kuwa Mkristo ama dini nyingine; upende usipende, ukahaba ni kazi na kuna watu wanaofanya kazi humo. Jamii inajengwa na makahaba ndani yake na lazma tukubali kuwaunga mkono."
images (50).jpeg

"Waheshimuni watu hawa na familia zao, wao pia lazima wawe na ulinzi na haki kama wafanyakazi wengine, mwili wake ni haki yake na anapaswa kulindwa dhidi ya unyanyasaji, anaweza kuwa na mume na watoto, kazi yake ndio inampatia kipato na maisha" alisema.
1755372828137.jpg

Kumekuwa na mjadala unaoendelea kuhusu kuhalalisha ukahaba ili kuimarisha afya na usalama kwa wafanyabiashara ya ngono na kulinda haki zao. Mnamo 2022, baraza la mawaziri liliidhinisha kuchapishwa Mswada wa Marekebisho wa Sheria ya Jinai (Makosa ya Kujamiiana na Mambo Yanayohusiana) kuhusu kuharamisha kazi ya ngono kwa maoni ya umma.
images (51).jpeg

Malema alisema wanawake wote wanapaswa kulindwa dhidi ya kuwa wahanga wa unyanyasaji. Hivyo biashara hii iwe sehemu ya watu kujipatia kipato.

JE HOME BOY AMEZINGUA AU YUPO SAHIHI KATIKA HILI SUALA?
 
Amezingua kurombana hakuhtaji siasa tuendelee kula kimya kimya nyama
Anataka tuwape heshima sio ukimromba umtangaze kwa wadau 😃 usione kipochi ukaanza kukisifia kupita kiasi 😃 we fanya kazi yako na kutoa makamasi baaasi
 
Bila uwepo wa machangudoa wanaume vichaa wataongezeka. Ubakaji ikiwa ni pamoja na ubakaji wa ndugu (incest), na ubakaji wa wanyama pia unaweza kuongezeka. Wazungu walishahalalisha wengine kwa uwazi na wengine kwa usiri.
 
Bila uwepo wa machangudoa wanaume vichaa wataongezeka. Ubakaji ikiwa ni pamoja na ubakaji wa ndugu (incest), na ubakaji wa wanyama pia unaweza kuongezeka. Wazungu walishahalalisha wengine kwa uwazi na wengine kwa usiri.
Kuna watu wanasubiria waanze kazi
 
Back
Top Bottom