GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Jukwaa la Katiba kutangaza Maombolezo ya siku 9
Katika kuonyesha msimamo wao wa kutokubaliana na maridhiano tete kati ya CDM na JK, Jukwaa la katiba lipo katika mchakato utaofanikisha kutolewa kwa tamko rasmi muda wowote kuanzia sasa kuhusu maombolezo ya siku 9 kwa msiba mkubwa wa Katiba.
Tafsiri sahihi ya maombolezo haya ni kuonyesha kwa namna ambavyo mbio za katiba mpya zilivyofikia ukingoni kwa masilahi ya dola na si nini wanachotakiwa kufanyiwa watanzania.
Bado sintofahamu na wingu kuhusu makubaliano ya CDM na JK yanazua maswali mengi kwa makundi shiriki katika kudai uwazi juu ya mchakato wa Katiba Mpya.
Kama muafaka utapatikana maombolezo haya yatadumu kwa siku 9 kuanzia desemba mosi hadi siku ya kumbukumbu ya uhuru.
Technically: Makubaliano ya kuuboresha mswaada yaliyofikiwa na CDM na JK yatatoa nafasi kwa nyongeza hiyo kufanyia marekebisho sheria ya kuundwa katiba mpya na si mswaada kwa maana kwamba marekebisho ya sheria kwa mujibu wa taratibu za Bunge hufanyika baada ya Kipindi cha miezi 6 na si vinginevyo.
Utagundua ndani ya muda huu JK na CCM watakuwa wamefanya mengi ya kutosha katika kupata katiba mpya ikiwa ni pamoja na kuunda tume, kukusanya maoni kwa tume isiyo na meno na hatimaye baada ya miezi sita marekebisho ya sheria yanafanyiaka bungeni huku mchezo ni kama umekwisha hivi.
My Take: sijui hii move ya CDM tuiite bao la kujifunga au bao la offside, Tusubiri tusikie ya Jukwaa la Katiba leo.
ADIOS
Katika kuonyesha msimamo wao wa kutokubaliana na maridhiano tete kati ya CDM na JK, Jukwaa la katiba lipo katika mchakato utaofanikisha kutolewa kwa tamko rasmi muda wowote kuanzia sasa kuhusu maombolezo ya siku 9 kwa msiba mkubwa wa Katiba.
Tafsiri sahihi ya maombolezo haya ni kuonyesha kwa namna ambavyo mbio za katiba mpya zilivyofikia ukingoni kwa masilahi ya dola na si nini wanachotakiwa kufanyiwa watanzania.
Bado sintofahamu na wingu kuhusu makubaliano ya CDM na JK yanazua maswali mengi kwa makundi shiriki katika kudai uwazi juu ya mchakato wa Katiba Mpya.
Kama muafaka utapatikana maombolezo haya yatadumu kwa siku 9 kuanzia desemba mosi hadi siku ya kumbukumbu ya uhuru.
Technically: Makubaliano ya kuuboresha mswaada yaliyofikiwa na CDM na JK yatatoa nafasi kwa nyongeza hiyo kufanyia marekebisho sheria ya kuundwa katiba mpya na si mswaada kwa maana kwamba marekebisho ya sheria kwa mujibu wa taratibu za Bunge hufanyika baada ya Kipindi cha miezi 6 na si vinginevyo.
Utagundua ndani ya muda huu JK na CCM watakuwa wamefanya mengi ya kutosha katika kupata katiba mpya ikiwa ni pamoja na kuunda tume, kukusanya maoni kwa tume isiyo na meno na hatimaye baada ya miezi sita marekebisho ya sheria yanafanyiaka bungeni huku mchezo ni kama umekwisha hivi.
My Take: sijui hii move ya CDM tuiite bao la kujifunga au bao la offside, Tusubiri tusikie ya Jukwaa la Katiba leo.
ADIOS