mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Habari wakuu,
Tokea nimeanza kufuatilia Siasa nimekuwa nikimsikia Joyce Mukya. Nimemsikia kwa mengi kuanzia bungeni akitajwa na mpaka uraiani, bahati mbaya au nzuri sijawahi kumuona sehemu yoyote hata bungeni.
Nasikia ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA kwa zaidi ya miaka 10. Sijawahi kumuona/kumsikia akichangia hoja yoyote bungeni, Sijawahi kumuona akijenga chama kwa namna yoyote tofauti na wabunge wengine wanawake wa chadema na wanachama wengine wanawake, kifupi sio mbunge active.
Kama hafanyi haya yote amewezaje kupeta na kuwa mbunge huku wanachama wengine active ambao wanakipigania chama wakiachwa solemba kwenye ubunge na sehemu nyeti chamani.
Juzi nikamsikiliza Jerry Muro ndio nikagundua kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na ni mama wa watoto wa Mwenyekiti Mbowe.
Katika fukunyua fukunyua ndio nikakutana na habari mbalimbali zinazohusu huyu mama na Mbowe nikakutana hizi baadhi na zenye ushahidi usioacha shaka...
1. Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Hilal Aeshi katika vita ya kimapenzi wakimgombania Mhe. Joyce Mukya
2. Mwigulu amlipua Mbowe bungeni, ni kuhusu kutumia vibaya madaraka yake na hawara
3. Freeman Mbowe na Joyce Mukya wamtumia Mjomba wa Mtoto kupata cheti cha kuzaliwa
Nikasema sawa, anapewa ubunge kwasababu ni mzazi mwenza wa Mwenyekiti wa chama, ila mbona hata waliopendelewa kwa kupewa ubunge wa vitu maalum kutokana na uhusiano wa kindugu au kingono na viongozi waandamizi wa CHADEMA wako active kwenye siasa za nchi, kulikoni huyu Joyce Mukya!?
Chama kinachojinasibu kuwa chama kikuu cha upinzani ni wakati sasa kuachana na kasumba yao ya upendeleo wa kugawa vyeo kwa undugu,kingono na kikanda. Wabadilishe mfumo wao wa uteuzi ili waweze kuwapa nafasi wengine wanaokipigania chama.
Asanteni sana.
Tokea nimeanza kufuatilia Siasa nimekuwa nikimsikia Joyce Mukya. Nimemsikia kwa mengi kuanzia bungeni akitajwa na mpaka uraiani, bahati mbaya au nzuri sijawahi kumuona sehemu yoyote hata bungeni.
Nasikia ni mbunge wa viti maalum kupitia CHADEMA kwa zaidi ya miaka 10. Sijawahi kumuona/kumsikia akichangia hoja yoyote bungeni, Sijawahi kumuona akijenga chama kwa namna yoyote tofauti na wabunge wengine wanawake wa chadema na wanachama wengine wanawake, kifupi sio mbunge active.
Kama hafanyi haya yote amewezaje kupeta na kuwa mbunge huku wanachama wengine active ambao wanakipigania chama wakiachwa solemba kwenye ubunge na sehemu nyeti chamani.
Juzi nikamsikiliza Jerry Muro ndio nikagundua kuwa ana uhusiano wa kimapenzi na ni mama wa watoto wa Mwenyekiti Mbowe.
Katika fukunyua fukunyua ndio nikakutana na habari mbalimbali zinazohusu huyu mama na Mbowe nikakutana hizi baadhi na zenye ushahidi usioacha shaka...
1. Mhe. Freeman Mbowe na Mhe. Hilal Aeshi katika vita ya kimapenzi wakimgombania Mhe. Joyce Mukya
2. Mwigulu amlipua Mbowe bungeni, ni kuhusu kutumia vibaya madaraka yake na hawara
3. Freeman Mbowe na Joyce Mukya wamtumia Mjomba wa Mtoto kupata cheti cha kuzaliwa
Nikasema sawa, anapewa ubunge kwasababu ni mzazi mwenza wa Mwenyekiti wa chama, ila mbona hata waliopendelewa kwa kupewa ubunge wa vitu maalum kutokana na uhusiano wa kindugu au kingono na viongozi waandamizi wa CHADEMA wako active kwenye siasa za nchi, kulikoni huyu Joyce Mukya!?
Chama kinachojinasibu kuwa chama kikuu cha upinzani ni wakati sasa kuachana na kasumba yao ya upendeleo wa kugawa vyeo kwa undugu,kingono na kikanda. Wabadilishe mfumo wao wa uteuzi ili waweze kuwapa nafasi wengine wanaokipigania chama.
Asanteni sana.