Joto hasira wa jay dee

Mkuu mpe heshima yake,huwezi kulinganisha komandoo na konstable/private!...

tatizo lake anawaiga mafikozolo kwa style za nyimbo zao..mwisho wa siku anaimba kwaya!!kwa akina vanessa na akina maua atasubiri saanaaa!!sauti yake ipo flat sanaaa!!
 
Una maana gani huu wimbo? Mi nimeshindwa kupata message nisaidieni na mie niuelewe
WOSIA WANGU KAMA IKITOKEA NIMETANGULIA KUFA KABLA YA RUGE AU JOE KUSAGA Watu wanashtuka mtu akiongelea kifo, Utafikiri hawafahamu fika kuwa kila nafsi itakionja, Kwenye maisha yangu nimepitia mambo mengi, magumu na mepesi Na bado naendelea ku experience mambo magumu zaidi kadri ninavyozidi kuwa mkubwa. Siku za karibuni nimekuwa nikipigwa vita sana na watu wenye uwezo mkubwa kifedha , ki umri na hata wenye ukubwa wa connection katika hii industry ya muziki. Wanaomiliki chombo cha habari. Nasimama na kusema kuwa sitokata tamaa, kwani lengo lao kubwa ni kuona na kuhakikisha nimeanguka kabisa na sipo katika ramani ya muziki. Watu hao ambao vita yao ilikuwa baridi miaka kumi iliopita, sasa inazidi kuwa moto baada ya kutambua kuwa mimi ni mtu mwenye maamuzi yangu na misimamo yangu bila kuburuzwa. Wanapita kila mahali kuhakikisha kila mrija unaoniingizia chochote unakatika, na hiyo ni kutaka kuuthibitishia umma wa Tanzania kuwa hakuna msanii anaeweza ku survive bila wao. Mimi ni msanii tofauti na hao mnaofikiria. Nadhani mnafahamu tangu niachane na Tuzo zenu mnazo influence nani apate nani asipate, na tangu niachane na Fiesta nilipolipwa laki 8 mara ya mwisho na kuamua kuunda Band ili nijiajiri na kupata shows zangu mwenyewe, ikafanikiwa sana jambo ambalo limewauma na kuamua kufanya kitu cha kuiangusha Band yangu. Nita survive kwa njia zozote MUNGU alizonipangia. Wakati bado wote tunapumua na kwakuwa watu hao hawanipendi kabisa, Naamini fika hawataweza kunipenda hata siku nitakapokuwa nimekufa. Na huu ndio wosia wangu kwa watu hao. Natambua wanaweza kutumia redio yao kutangaza sana kifo changu na kusema marehemu alikuwa mtu mzuri na pengine kupiga nyimbo zangu kuanzia asubuhi mpaka jioni. Ila naomba nitamke hivi, siku nikifa CLOUDS FM isipige nyimbo zangu, wala isiongelee lolote kuhusiana na kifo changu. Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga wasihudhurie msiba wangu, na mkiwaona muwapige wame Enyi mtakaokuwa hai baada yangu. Kama wamenifitini, na hawajanipenda nikiwa hai Hakuna haja ya kujifanya kunipenda nikiwa marehemu. Sina haja wanipende pia kwakuwa mimi sio ndugu yao, Ila ubaya wanaoundeleza mioyoni mwao wanaujua na nina hakika nafsi zao zinawasuta pia. Niliamua kujiepusha nao miaka mingi na kufanya biashara zangu, nimekaa kimya watu wanafikiri nabebwa lakini sijabebwa chochote sikutaka ugomvi haya mambo yalianza baada ya Album yangu ya pili ya Binti mwaka 2003 nilipojitoa Smooth Vibes chini ya Ruge. Nilivumilia fitna nikiamini ipo siku yatakwisha lakini naona moto ndio unazidi kuwaka. Na hii ni kwasababu wanaogopa msanii akiwa mkubwa watashindwa kumuamrisha, Hamuwezi kumiliki dunia.. Kama mnasema mlinibeba mbona hamkuwabeba dada zenu wa tumbo moja waimbe ili hela irudi nyumbani??. kama kweli wewe Kusaga unajua kubeba basi beba jiwe liimbe liwe star.. Kwa roho zenu mbaya mnaweza kumbeba mpita njia nyie??. Talent haibebwi, hujibeba kama mnabisha si mna watoto wabebeni basi wawe kama kina Diamond ndio nitaamini kweli nyie mnaweza kubeba watu. Mnawatishia wasanii kuwa yoyote atakaefanya nyimbo na mimi hazitapigwa, vikao vinne mmeshakaa kunijadili. Mnadhani je! nitapungukiwa nini endapo wasanii wengine wakiacha kufanya kazi na mimi?? nyimbo hazitakuwa nzuri. Basi sawa ngoja tuone MUNGU ni nani, Binadamu nani?? Kwahiyo mtaamrisha watu pia wasikae na mimi?? Ilikuwa niseme majina matatu huyo mmoja nimemsamehe baada ya kugundua sio hiyari yake ila yuko under influence ya hawa jamaa wawili. Kila siku mnamsingizia Ruge peke yake Kusaga ni mfitini kuliko hata huyo Ruge, watu hamjui tu. Mtu hela zote hizo bado shillingi mbili ya Jide inakuuma?? Roho gani hiyo?? Naishia hapo na sitabatilisha kauli yangu JIDE
 
Haaah. Eti ana sumbuliwa na ndoto anaziandika kwa ma blogs uyu mdada ugumba/utasa vina mtatiza sana uyu jide.
Haeleweki ana maanagani . Hata mi sija mwelewa.

We mwenye mtt mwanao wankiume anweza ishia kuwa si ridhik na wakike ataish shivaz maaana hujui utu wa mtu n nn!utasa kwani kajiumbia yeye!!?
 
siku nilipomkuta banking hall moja hapa mjinii anavurumisha matusi kwa wafanyakazi wa benki nilimdharau mpaka kesho na sioni kama ni mwanamziki anaejielewa!hana heshima,hafikirii analolisema,yani anaongozwa na hasira zake,ambazo kwa msanii ambaye ni kioo cha jamii,yor not suppose to act in biiig fool!!na sukuhzi nyumbani lounge ni doroo!!
 
siku nilipomkuta banking hall moja hapa mjinii anavurumisha matusi kwa wafanyakazi wa benki nilimdharau mpaka kesho na sioni kama ni mwanamziki anaejielewa!hana heshima,hafikirii analolisema,yani anaongozwa na hasira zake,ambazo kwa msanii ambaye ni kioo cha jamii,yor not suppose to act in biiig fool!!na sukuhzi nyumbani lounge ni doroo!!
Natamani kukajua vizuri haka kastori rafik
 
siku nilipomkuta banking hall moja hapa mjinii anavurumisha matusi kwa wafanyakazi wa benki nilimdharau mpaka kesho na sioni kama ni mwanamziki anaejielewa!hana heshima,hafikirii analolisema,yani anaongozwa na hasira zake,ambazo kwa msanii ambaye ni kioo cha jamii,yor not suppose to act in biiig fool!!na sukuhzi nyumbani lounge ni doroo!!

ukiongezea na jini mahaba basi matatizo juu ya matatizo
 
Haaah. Eti ana sumbuliwa na ndoto anaziandika kwa ma blogs uyu mdada ugumba/utasa vina mtatiza sana uyu jide.
Haeleweki ana maanagani . Hata mi sija mwelewa.

Hivi mtu unapomshambulia mwingine kwa matatizo ya kimaumbile ni kwamba wewe upo kwenye nafasi gani ? wewe ni MUUMBA ama ? Tuwe waungwana kuficha jina usifahamike sio kinga ya adhabu ya Mungu. Sisi hatukufahamu lakini aliyetuumba huwezi kujificha kwake.
 
Jana kapiga wimbo hata hajausindua umekaa vzr sana tid alisaidia kwny chorus watamkomajee redio maji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom