Joseph Msukuma ni nani?

Kipenzi Changu

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
59,115
Reaction score
138,118

Kwa mara ya kwanza nilimuona Bwn.Joseph Kasheku (Msukuma) akiwa kwenye kipindi cha siasa Star TV, akatambulishwa kama Mwenyekiti wa CCM Geita.

Sikumtilia maanani sana kwa kuwa alijaa majigambo kuliko hoja, tofauti na makamanda wa SAUT ambao walijenga hoja nzito. Alionekana bwana mdogo tu hivi!

Ghafla nikasikia Mh. Mwigulu anakata mawimbi na "Chopa la Msukuma". Na leo pale kwenye Safari isiyo na Matumaini kafanya taiz kutua na Chopa.

Sasa wanaomjua vizuri watupe details, huyu ni nani hasa, katoa wapi mapesa haya yote, halafu kama vile kwa umri mdogo!!
 

Attachments

  • msukuma.jpg
    20 KB · Views: 9,892
huyu ni kada wa ccm ambaye anataka kugombea jimbo la geita,ila kwa kweli upstairs ni box tupu,hata ccm wanajuta kumpa nafasi ya uenyekiti wa ccm mkoa,aliwahi kuifuta kazi kamati ya siasa ya mkoa wakati anajua hana uwezo huo,kuna kipindi halmashauri ya geita ilikuwa na ujenzi wa choo katika eneo la umma,yeye akaenda na kundi la mabaunsa wakaenda kukifukia,yaani ni tatizo
 

Huyu ndio anafaa sasa
 
Ni mjinga fulani, ambae amewahi dhalilika vibaya kwenye mjadala mmoja hapo star TV mpaka leo hawajamuita. Nashangaa mwanzoni alikuwa anampiga vita lowassa hadi akakosana na hamisi mgeja, lakini sasa hivi yupo team lowassa! Kitu nina uhakika nacho atakuwa mshirikina wa hali ya juu, maskini albino wa geita!
 
Kila nikitazama marafiki wa Lowassa napata hasira sana
 
OKW BOBAN SUNZU

Yaani nilikuwa mbioni kuanzisha uzi huu umeniwahi... asee kajamaa kanaonyesha kacheshi kweli kanajiita king musukuma. Tunataka tumjue zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Kwa mujibu wa taarifa toka ndani ya kikao cha baraza la madiwani geita ni kuwa ndgu Msukuma, Diwani kata ya Nzera CCM na M/kiti CCM mkoa geita amelazimika kukimbia kikao cha baraza la Madiwani halmashauri geita leo baada ya kupitisha maazimio ya kuchanja ng'ombe wote wilaya za geita na nyang'wale kwa sh 1,500/- kila ng'ombe.

Bwa Msukuma amelazimika kukimbia kikao hicho baada ya kusutwa na madiwani wa CCM ambao ki msingi ndio wengi. Tarehe 9/12/2012 akihutubia mkutano wa hadhara geita mjini aliwaambia wananchi kuwa yeye ndiye Boss wa Mkoa wote wa geita, hakuna cha mkuu wa mkoa ,mkurugenzi wala mkuu wa wilaya , hivyo hakuna kuchangia pesa yoyote kwenye mpango huo wa chanjo kitu ambacho ki mantiki ni kazi ya wataalamu na wala si kazi ya M/kiti CCM mkoa.

Katika kikao cha baraza la madiwani leo, hoja ya Mganga Mkuu wa mifugo imekubaliwa na kupitishwa na Madiwani wote wa CCM na CDM, hivyo ika onekana Boss wa mkoa amedhalilishwa sana licha ya M/kiti huyo kuwatangazia wananchi kwamba Mganga huyo alitaka kumuhonga rushwa sh 30,000,000/- . Kwa wasio mfahamu huyu bw Msukuma ni kuwa ndo aina ya watu kama akina Matata-mwza ambao kimsingi hawapaswi kuongoza jamii kwa maslahi mapana wananchi lakini leo ndiye kapewa kuongoza ccm mkoa wa geita sijui kwa sifa zipi ! Tangu amekuwa M/kiti CCM amekuwa akitoa matamko mbalimbali ambayo kimsingi hayana tija kwa wananchi kama si matatizo,

Kwa mfano :- alipiga marufuku sheria ya kufanya usafi kila siku ya alhamis kwa kuwatishia na kuwadhalilisha viongozi waandamizi wa wilaya lakini hadi jana sheria hii ilitekelezwa kama kawaida. Pia aliwaagiza wananchi kijiji Katoma walio hamishwa kupisha mgodi wa GGM warudi kwenye mashamba yao kitu ambacho yeye ni sehemu ya tatizo , wananchi walipo rudi walikamatwa na FFU ambapo wengine tayari wamesha hukumiwa vifungo.

Kwa kifupi huyo ndiye bw Msukuma a.k.a Nyundo. Mwanafalsafa Albert alipata kusema "HAKUNA KITU HATARI SANA DUNIANI KAMA MAMLAKA IKIWA KWENYE MIKONO YA MTU AMBAE ANA AKILI NDOGO ."


 



Wakati Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikiwa hakijaruhusu kampeni, Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, ambaye amesema ameombwa na wazee na wasomi kuwania urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu, sasa atazunguka nchi nzima kwa kutumia helikopta kufanya mikutano ya hadhara kuzungumza na wananchi.

Hatua hiyo ya Mwigulu, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Tanzania Bara, ilitangazwa na Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Geita, Joseph Msukuma jana.

Msukuma alisema ameamua kumpa Mwigulu helikopta yake ili aitumie kuzunguka nchini kote kutokana na kuwa mtetezi wa wananchi na maslahi ya taifa kwa jumla.

Alitangaza hatua hiyo katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na CCM Wilaya ya Morogoro mjini kwa ajili ya kuwashukuru wakazi wake kwa kuwachagua wagombea wa chama hicho katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliomalizika hivi karibuni.

Mgeni rasmi alikuwa Mwigulu aliyeambata na Msukuma kwa kutumia helikopta hiyo.

“Tulianza ziara zetu Mkoa wa Tanga katika wilaya zote. Leo tumezunguka wilaya zote za Mkoa wa Morogoro na kumalizia hapa kwa chopa. Lakini tayari kumejitokeza majungu katika mitandao kuwa Mwigulu kanunua chopa ya kufanyia kampeni. Sasa nataka kuwaambia chopa ni mali yangu mimi Msukuma na ninampa Mwigulu atazunguka nayo Tanzania nzima kwa kuwa namuunga mkono kwa kutetea wanyonge na maslahi ya taifa hili,” alisema Msukuma.

Aliongeza: “Kama kuna PCCB, polisi wanataka kumchunguza Mwigulu kapata wapi chopa ya kutembelea wasihangaike, waje kwangu mimi kuniuliza au waulize huko Geita Msukuma ni nani? Hii ni mali yangu halali na nimeamua mwenyewe kumpa kwa hiari yangu kutokana na kumuunga mkono kwa kuwa ni msema ukweli. Lakini siyo kumfanyia majungu Mwigulu katika mitandao ya kijamii tuliyoanza kuiona tayari.”

Alisema Mwigulu ni mmoja wa viongozi wazalendo nchini kwa kutetea maslahi ya taifa na kupingana na viongozi wanaokandamiza wanyonge na matokeo yake kuifanya CCM ichukiwe na wananchi.

Kuhusu vigogo waliohusishwa na kashfa ya uchotwaji zaidi ya Sh. bilioni 300 katika akaunti ya Tegeta Escrow, iliyokuwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Msukuma alisema wote waliohusika na kashfa hiyo wanapaswa kukamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria bila kujali anatoka CCM.

Alisema watu hao wanapswa kuchukulia hatua hizo kwa kuwa wao ndiyo chanzo cha Watanzania kuendelea kuishi katika hali ya umaskini na kusababisha kukichukia chama hicho.

“Wote waliochota fedha za akaunti ya Escrow awe waziri au nani, tunataka wakamatwe na kushtakiwa ili kuwa mfano wa viongozi wengine. Wananchi hawawezi kuchukia chama chetu kwa sababu ya watu wachache waliokula fedha kwa manufaa yao,” alisema Msukuma.

Kwa upande wake, Mwigulu alimshukuru Msukuma kwa kumpa helikopta hiyo ili kuzunguka nchini kuzungumza na wana CCM na Watanzania kwa jumla kuhusiana na mustakabali wa nchi pamoja na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na serikali dhidi ya malalamiko ya wananchi.

Kauli ya Msukuma kuhusiana na helkopta hiyo imefuatia mjadala katika mitandao mbalimbali huku baadhi ya watu wakidai kuwa Mwigulu ameinunua na wengine wakihoji hatua hiyo.

Kuhusu sakata la akaunti ya Tegeta Escrow, Mwigulu alisema wote waliochota fedha za umma hawatabaki salama.

Mwigulu alisema wote watafikishwa mahakamani pamoja na wale waliokwepa kulipa kodi na kwamba, mchakato wa kukatwa kodi hiyo umekwishaanza.

Alisema CCM haiwezi kumvumlia mtu yeyote aliyekula fedha za umma na na kuwataka wajiandae kuanzia sasa kwa kuwa hawatabaki salama, watafikishwa mikononi mwa vyombo vya sheria.

Kuhusu wanafunzi wa programu maalumu stashahada ya ualimu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) kufikishwa mahakamani kutokana na kufanya maandamano bila kibali, alisema haikuwa busara kufanya hivyo kwa kuwa suala hilo lilipaswa kumalizwa ndani ya uongozi wa chuo, kwani walikuwa wakidai haki yao.

Alisema katika kila vyuo kuna taratibu za kinidhamu, migomo na maandamano, hivyo badala ya kuwafikisha mahakamani wanafunzi hao, walipaswa kulimaliza tatizo hilo chuoni.

Hata hivyo, Mwigulu aliwakikishia wanafunzi hao kuwa serikali imeshaanza kufanyia kazi madai yao na kwamba, kinachosubiriwa hivi sasa ni fedha, ambazo zikipatikana suala hilo litamalizika.

Aliwataka wananchi wa Mkoa wa Morogoro kujitokeza kujiandikisha katika daftari la wapigakura ili kupiga kura katika uchaguzi ujao kuchagua viongozi, ambao wana uchungu na nchi.

Alisema suala la kujindikisha katika daftari hilo ni muhimu kwa kuwa litawafanya wananchi kuchagua viongozi watakaowataka na kuacha kulalamika baada ya uchaguzi kuisha.

Kuhusu kukosekana dawa katika hospitali za mkoa wa Morogoro, alisema inashangaza kuona serikali imekuwa ikizinunua na kuzifikisha katika hospitali na vituo vya afya.

Lakini akasema zimekuwa zikiibwa au kuuzwa katika maduka ya dawa ya watu binafsi, huku viongozi wa serikali wakiwapo pasipo kuwachukulia hatua wahusika na hivyo wananchi kulalamikia serikali.

Alimuagiza Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Said Amanzi, kuhakikisha anasimamia tatizo la watumishi wasio waaminifu, ambao wanauza dawa za serikali kwa kuwachukulia hatua kali na kuwatataka pia wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwataja wahusika pale wanapowaona.

Mwigulu akihojiwa na kituo kimoja cha televisheni nchini hivi karibuni, alisema amekuwa akipokea ujumbe mwingi kutoka kwa wazee wa Kijiji cha Butiama, mkoani Mara na kutoka kwa vijana wa vyuo vikuu, wakimuomba awanie urais mwaka huu, lakini suala hilo haliwekei umuhimu.

Badala yake, alisema anatekeleza jukumu kubwa alilopewa na Rais Jakaya Kikwete la Naibu Waziri wa Fedha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…