View attachment 2975932
Ni Joe Kusaga tena…
Waswahili husema mwenye nacho huongezewa, sio sahihi. Mwenye nacho hujiongeza ndipo huongezewa.
Mfanyabiashara na mwekezaji mkubwa nchini aliyejikitika zaidi kwenye tasnia ya burudani, Joseph Kusaga yuko mbioni kuja na App itakayokuwa katika mtindo unaoshabihiana na App maarufu ulimwenguni Netflix.
Ni App ya burudani…
Maudhui makubwa yatakayopatikana ndani ya App hiyo ni burudani. Zikiwemo series na movies za kibongo, habari za michezo na kutakuwemo pia na vipindi vya matukio ya wanamuziki wa Bongo Flava kama vile matukio wakati wa kuchukua video za nyimbo zao (behind the scenes)
Ni uwekezaji mkubwa!
Taarifa zinasema Joe Kusaga amefanya uwekezaji mkubwa sana katika App hiyo, kuanzia ununuzi wa vifaa vya kisasa vinavyosemekana kuwa na uwezo sawa na App nyingine kubwa za kimataifa kama Prime Video, Hulu, Netflix n.k
Pia itakuwa inapatikana kwenye TV za Smart na Android kama zilivyo hizo App nyingine.
Ni mradi wake binafsi.
Huu ni mradi binafsi wa Joe Kusaga nje ya miradi ya familia yake ambayo wanamiliki miradi mingi kwa pamoja ukiwemo Clouds media.
Pia ni mradi wake bila ya ushirika kama ilivyo Wasafi n.k
Kuzinduliwa June mwaka huu
Mpango wa awali wa uzinduzi ulikuwa tarehe 9 June ambayo ni siku ya kuzaliwa ya Jose Kusaga, lakini kuna mambo yalitokea yakapelekea uzinduzi kusogezwa mbele.
Licha ya changamoto hizo zilizojitokeza, bado uzinduzi utafanyika tarehe yoyote ndani ya mwezi huohuo (June).
Kupitia chanzo cheti,
Nifah.