Joseph Kabila kulidhulumu na kulitesa Kanisa Katoliki, anatambua nguvu ya kanisa kweli?

bigmind

JF-Expert Member
Oct 28, 2015
12,457
12,668
Katika hali ya kushangaza mambo yanayoendelea nchini Congo DRC, chini ya rais Joseph Kabila ni kulichezea Kanisa Katoliki na bila kujua ni kwa namna gani linaweza kumuweka au kumwondoa mtu yeyote kwenye utawala.

Ni juzi kati nchi ya Congo DRC ilipatwa msibwa mkubwa wa kiongozi mkuu wa upinzani bwana ETIEN CHISEKEDI huyu alikuwa kinara na mtu mwenye ushawishi mkubwa katika siasa za upinzani na kitaifa nchini DRC.

Kabla ya kifo cha bwana CHISEKED mgogoro wa kisiasa juu ya mhula wa tatu wa rais ambao ni kinyume na katiba ya nchi, mgogoro huu ulikuwa unatafutiwa ufumbuzi wa kusiasa kwa njia ya amani kwa msaada wa kimataifa chini ya uratibu wa KANISA KATOLIKI.

Kufuatia Kanisa Katoliki kuwa mstari katika masuala kupatanisha migogoro ya kisiasa duniani chini ya kamati yake HAKI NA AMANI huwa halina upendeleo na mara nyingi limeonekana kuwa mwiba kwa viongozi wasiopenda Demokrasia duniani.

Rais Joseph Kabila ni miongoni mwa marais wenye utata barani Africa. Kitendo cha rais kabila kukataa kufanyika uchaguzi baada ya mhura wake wa pili ambao alitakiwa aachie madaraka. Kanisa katoliki halikupepesa macho katika kukemea hulka ya rais Joseph Kabila kutaka kukanyaga katiba ya nchi.

Kufuatia msimamo KANISA KATOLIKI kuonekana kumpinga waziwazi
Rais Joseph Kabila sasa naona kaamua kuliandama Kanisa Katoliki kwa kutumia vyombo vya dola hasa jeshi anasahau nguvu ya Kanisa Katoliki ambazo huwa linaushawishi mkubwa wa mataifa yote yenye nguvu duniani kama MAREKANI, UJERUMANI, UFARANSA, ITALIA na URUSI.

Hapa unaweza kuona jinsi kanisa lilivyo na nguvu ata kuwaleta maadui pamoja linapokuja suala la kumuandama adui wake kitendo cha rais J.Kabila kufanya dhuluma kwa Kanisa Katoliki kitamtokea puani.

Hizi ni picha za baadhi ya matendo ya dhuluma kwa Kanisa Katoliki huko nchini Congo DRC...
IMG-20170223-WA0030.jpeg
IMG-20170223-WA0031.jpeg
IMG-20170223-WA0029.jpeg


Kwa Kanisa Katoliki kuchezea YESU WA EKARISTIA ni udhalilishaji wa kiwango cha juu mno. Hakika maombi, sala na dua zitakazopigwa kuunganisha na rasimali ya akili (elimu) na mali (baraka za mikono ifanyayo kazi) zitatumika mpaka huyu kiongozi dhalimu aliyekosa heshima hadi kwa Mungu.

Dunia inatakiwa kumpinga J.Kabila na vibaraka wake na pia viongozi wengine wa kariba yake wanaoibuka hasa katika Afrika. Tukiendelea na upuuzi huu tutakuwa na akina NKRUNZINZA kibao, mifano ni mingi sana, Rwanda, Uganda, Zimbabwe, Gambia tumeshuhudia, hii tabia inaendelea kuota mizizi.

AMERIPOTI RAIA MMOJA WA CONGO
Eklesia is going through pesecutions and humiliation.I Democratic Republic of Congo after the death of one prominent Opposition Leader the Government Troops went and demolish the Catholic Church in which he was congregating because they feel the Church is opposing Kabila's third term bid. Below are some of the scene photos. It's sad for our Church. We need to pray for them and our Church
 
lakini Tanzania pia tumekuwa karakana na kiwanda cha kutengeneza maraisi wahalifu na wanyama,kagame,kabila,museven,nkurunzinza pia...!!nabado serikali imekuwa kimya na kufunikafunika mambo tawala zetu zote zimetumika katika kufanikisha vita za maziwa makuu
 
Kanisa catolic kuwa na nguvu ilikuwa zamani enzi za Roman empire sio siku hizi.

Wana ushawishi baadhi ya nchi kama Tanzania,mexico labda na philiphine,lakini hata huko ushawishi si mkubwa wa kuweza kubadili kiongozi wa nchi
 
Ushawishi wa katoliki umebaki vatican tu, nchi nyingi zina manabii wao na makanisa yao na taratibu ambazo ni tofauti na roman
 
Katika hali ya kushangaza mambo yanayoendelea nchini Congo DRC, chini ya rais Joseph Kabila ni kulichezea Kanisa Katoliki na bila kujua ni kwa namna gani linaweza kumuweka au kumwondoa mtu yeyote kwenye utawala.

Ni juzi kati nchi ya Congo DRC ilipatwa msibwa mkubwa wa kiongozi mkuu wa upinzani bwana ETIEN CHISEKEDI huyu alikuwa kinara na mtu mwenye ushawishi mkubwa katika siasa za upinzani na kitaifa nchini DRC.

Kabla ya kifo cha bwana CHISEKED mgogoro wa kisiasa juu ya mhula wa tatu wa rais ambao ni kinyume na katiba ya nchi, mgogoro huu ulikuwa unatafutiwa ufumbuzi wa kusiasa kwa njia ya amani kwa msaada wa kimataifa chini ya uratibu wa KANISA KATOLIKI. Kufuatia Kanisa Katoliki kuwa mstari katika masuala kupatanisha migogoro ya kisiasa duniani chini ya kamati yake HAKI NA AMANI huwa halina upendeleo na mara nyingi limeonekana kuwa mwiba kwa viongozi wasiopenda Demokrasia duniani.

Rais Joseph Kabila ni miongoni mwa marais wenye utata barani Africa. Kitendo cha rais kabila kukataa kufanyika uchaguzi baada ya mhura wake wa pili ambao alitakiwa aachie madaraka. Kanisa katoliki halikupepesa macho katika kukemea hulka ya rais Joseph Kabila kutaka kukanyaga katiba ya nchi. Kufuatia msimamo KANISA KATOLIKI kuonekana kumpinga waziwazi rais J. Kabila sasa naona kaamua kuliandama Kanisa Katoliki kwa kutumia vyombo vya dola hasa jeshi anasahau nguvu ya Kanisa Katoliki ambazo huwa linaushawishi mkubwa wa mataifa yote yenye nguvu duniani kama MAREKANI, UJERUMANI, UFARANSA, ITALIA na URUSI. Hapa unaweza kuona jinsi kanisa lilivyo na nguvu ata kuwaleta maadui pamoja linapokuja suala la kumuandama adui wake kitendo cha rais J.Kabila kufanya dhuluma kwa Kanisa Katoliki kitamtokea puani.

Hizi ni picha za baadhi ya matendo ya dhuluma kwa Kanisa Katoliki huko nchini Congo DRC...View attachment 473980View attachment 473982View attachment 473983

Kwa Kanisa Katoliki kuchezea YESU WA EKARISTIA ni udhalilishaji wa kiwango cha juu mno. Hakika maombi, sala na dua zitakazopigwa kuunganisha na rasimali ya akili (elimu) na mali (baraka za mikono ifanyayo kazi) zitatumika mpaka huyu kiongozi dhalimu aliyekosa heshima hadi kwa Mungu.

Dunia inatakiwa kumpinga J.Kabila na vibaraka wake na pia viongozi wengine wa kariba yake wanaoibuka hasa katika Afrika. Tukiendelea na upuuzi huu tutakuwa na akina NKRUNZINZA kibao, mifano ni mingi sana, Rwanda, Uganda, Zimbabwe, Gambia tumeshuhudia, hii tabia inaendelea kuota mizizi.

AMERIPOTI RAIA MMOJA WA CONGO
Eklesia is going through pesecutions and humiliation.I Democratic Republic of Congo after the death of one prominent Opposition Leader the Government Troops went and demolish the Catholic Church in which he was congregating because they feel the Church is opposing Kabila's third term bid. Below are some of the scene photos. It's sad for our Church. We need to pray for them and our Church
Pole sana Mkuu, soma vizuri Biblia kitabu cha Waamuzi utagundua kuwa Mungu hatetewi wala hasaidiwi bali hujutetea Yeye Mwenyewe na ikifika hatua hiyo ujue Mungu hujidhihirisha kwa namna ambayo utatamini upenye chini ya ardhi! NASHAURI IFANYIKE TOBA KAMA NI DHAMBI MAANA HUJUI MUNGU ATAFANYA NINI JUU YA TAIFA HILO AMBAPO MADHARA YAKE YAWEZA KUJA MPAKA KWAKO!
 
Kweli tunatii vifungu vya biblia kama vile

"Heri wapatanishi..."
Lakini kwa kanisa kuingia ktk migogoro ya kisiasa sioni kama ni vyema.

Mambo hayo yaachwe ktk jumuia za kimataifa na vyombo mbali mbali vya usuluhidhi ila

Kanisa hapana.!
 
Mkongo yeyote mwenye upeo kidogo kamwe hawezi lipenda kanisa katoliki akikumbuka kina king leopard 11 walivyotumia kanisa kuinyonya kuwadhalilisha kuwadhulumu na kuwavua utu wakongo
 
Kweli tunatii vifungu vya biblia kama vile

"Heri wapatanishi..."
Lakini kwa kanisa kuingia ktk migogoro ya kisiasa sioni kama ni vyema.

Mambo hayo yaachwe ktk jumuia za kimataifa na vyombo mbali mbali vya usuluhidhi ila

Kanisa hapana.!
Wewe sijuu ni mkristo? Utaratibu wa kanisa tangu enzi za petro na mitume wote hadi paul kanisa halijawahi kunyamazia dhuluma yeyote dhidi ya watu wa Mungu! Wasikilize manabii wote hakuna ata mmoja ambaye hakukemea uovu wa watawala hasa wafalme soma kitabu cha wafalme1 na wafalme 2 utaona kazi ya manabii(kanisa) likisimama kupinga dhuluma za kisiasa.

Kitabu cha matendo ya mitume utashuhudia mateso kwa mitume wote 12 wakiuawa na watawala baada ya kupinga dhuluma na kuhubiri haki, upendo na usawa.

Ndugu kanisa katoliki VATICAN kuna tume ya haki na usawa ya kidunia kazi ya kuu ni kusimamia na kutetea haki na usawa kupinga dhuluma dhidi ya watu wote bila kuzingatia imani na dini zao. Kanisa katoliki ni zaidi ya ROMA empire. Watu mnachanganya roma empire ili surrender mamlaka yake kwa Mungu (kanisa katoliki) tangu kipindi cha mfalme Constantine 300 BK tangia hapo hakuna falme inayoitwa Roma duniani, ilibaki nchi ya Italia ambayo ina sehemu ya kanisa katoliki iliyokuwa Roma.
 
Mkuu unataka kuniambia Makanisa mengine ni ya Shetani ???

MSEZA MKULU
Mkuu kanisa ni moja tu mkuu! KANISA KATOLIKI

Haya mengine ni sawa na wewe ulivyomjukuu wa babu na bibi yako. Unaweza kujipata na kuwatusi au kuwafanyia dhihaka ila ujue bila babu zako usingekuwepo kamwe.

Sijui kama umenielewa haijalishi wanalipinga au kuridharau kwa kiasi gani ila bado litasimama kujinadi kama baba wa ukristo duniani. Ata uislam mtume Mohammed kanjanja tuuh.
 
Back
Top Bottom