Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa amesema haoni sababu zozote za msingi za maandamano ya CHADEMA.
"unaposema utaandamana kutoka Arusha hadi Mtwara, unamkomna nani? Ni vema ukatafuta utaratibu mwingine wa kutatua matatizo badala ya kuandamana"
Tendwa alitoa kauli hiyo alipokuwa akifanya interview ktkt kipindi cha DAKIKA 45 cha ITV saa tatu leo usiku.
Tendwa ametishia pia kukifuta chama chochote cha siasa kinachoendeleza kampeni wakati uchaguzi umekwisha.
Akitoa maelezo alisema
"ukishindwa uchaguzi unajipanga kwa ajili ya uchaguzi ujao. Taratibu zinasema unajipanga na sio unafanya kampeni."
Akaongeza,
"sio unatoka bungeni unaenda kuwaambia wananchi, sisi ni wachache kuliko CCM kakini hawatushindi hoja. Sisi tunatoa hoja za kuomba mwongozo kuliko CCM, kwa hiyo uchaguzi ujao mtuchague sisi" aliongeza Tendwa bila kusema wazi anakilenga chama gani.
Ktk kuonesha mamlaka aliyonayo amesema hatasita kukifuta chama chochote kitakachokiuka taratibu.
Alipoulizwa na Mtangazaji wa kipindi hicho Selemani Semunyu kuwa jeuri hiyo ameitoa wapi alijibu,
"mamlaka ninayo, sio jeuri ni mamlaka."
SOURCE:ITV
Tendwa ama anaugua amnesia au ni msanii wa viwango vya kipekee. Mara kadhaa amenukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa maandamano ni haki ya msingi wa vyama vya siasa. Sasa anatishia nini hapa? Nani kamtuma Tendwa kutishia watu? Na ubavu gani huyu babu kama si kujependekeza?
Na kama kweli ni mwanaume afute 'hicho' chama, afute tuone!