John Nyerere kuagwa leo, Msasani

John Nyerere kuagwa leo, Msasani

Zamani wtt wa viongozi walikuwa wanashiriki ktk ujenzi wa taifa hili,leo wtt wa viongozi wanashiriki ktk kulihujum taifa hili!
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameongoza makumi ya viongozi wa Serikali waliojitokeza jana kumfariji Mama Maria Nyerere, mjane wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere baada ya kifo cha mwanaye, John Nyerere.

Mtoto huyo wa nne wa Mwalimu Nyerere, alifariki dunia juzi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alikokuwa akitibiwa.

Akizungumzia ushiriki wa Serikali katika msiba huo, Pinda alisema hakutakuwa na protokali, bali kila atakayeguswa atashiriki kulingana na muda wake.

"Familia itakuwa imeguswa sana na msiba huu kwa sababu huishi kwa pamoja na hakuna utengano. Si familia ya kujikweza na ndiyo maana inaishi maisha ya kawaida," alisema.

Alieleza kuwa upo uwezekano pia baadhi ya nchi zikatuma wawakilishi kwa kutambua mchango wa Mwalimu katika harakati zao za kupigania uhuru.

"Kuna baadhi ya wapiganaji kama Frelimo wa Msumbiji na ANC wa Afrika Kusini wako wanajali sana kwa kila jambo linalomuhusu Mwalimu ikiwa ni pamoja na familia yake. Wizara ya Mambo ya Nje nadhani watakuwa wanaandaa utaratibu wa kuwakaribisha kama watakuwa tayari," alisema.

Viongozi wengine waliojitokeza jana ni pamoja na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, mawaziri wakuu wastaafu, Salim Ahmed Salim na Jaji Joseph Warioba, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na aliyekuwa wa Waziri wa Ulinzi, Profesa Philemon Sarungi.

Wengine ni aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Balozi Juma Mwapachu, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura.

Wakati viongozi wengine walifika na kuondoka, Jaji Warioba akiwa na mkewe, alikuwapo kwa muda mwingi zaidi katika eneo hilo.

Taarifa zilizopatikana zilieleza kuwa mwili wa kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) umehifadhiwa katika Hospitali ya Lugalo.

Msemaji wa familia, Moringe Magige alisema maziko ya marehemu John yanatarajiwa kufanyika Jumatano huko Butiama mkoani Mara.

"Kesho (leo) kutakuwa na misa ya marehemu na baadaye mwili wake utaagwa. Asubuhi ya keshokutwa utasafirishwa kwa ndege kwenda Butiama kupitia Mwanza," alisema Moringe.

Moringe ambaye pia ni mjukuu wa Mwalimu Nyerere alisema marehemu aliugua kwa muda mrefu kidogo na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa kwa takriban wiki mbili akipatiwa matibabu.

Watoto wengine wa Hayati Baba wa Taifa na Mama Maria Nyerere ni Andrew, Anna, Magige, Makongoro, Madaraka na Rose.

Enzi za uhai wake, marehemu alikuwa rubani wa ndege za kivita za JWTZ hadi alipoamua kustaafu kwa hiari yake.

Chanzo: Mwananchi
 
Hakuwa na mke wala watoto au watoto wa mwalimu walikuwa ni muhimu kutajwa kuliko watoto wake na mke kama wapo??!!!
 
. Wewe unajua ni wanane? Mimi nilikuwa bado sijawahesabu. Lakini hao wanane ni wengi kuliko wa Mwalimu.
Andrew Nyerere naona km unajaribu kuiweka peupe sana familia ya John wakatj labdq yy ktk kipindi chake cha uhai hakupenda kuwa public figure, tumpe uhuru wa kuendelea kuficha mambo yake km yy mwenyewe alivofanya wakati akiwa mzima!
 
Last edited by a moderator:
Andrew Nyerere naona km unajaribu kuiweka peupe sana familia ya John wakatj labdq yy ktk kipindi chake cha uhai hakupenda kuwa public figure, tumpe uhuru wa kuendelea kuficha mambo yake km yy mwenyewe alivofanya wakati akiwa mzima!

Nakubaliana na wewe. Wale watoto wengine wamezaliwa nje ya ndoa. Tukiwataja tunaweza kupata matatizo na Kanisa Katoliki.
 
Last edited by a moderator:
Nakubaliana na wewe. Wale watoto wengine wamezaliwa nje ya ndoa. Tukiwataja tunaweza kupata matatizo na Kanisa Katoliki.

Nashukuru km umenielewa mkuu, athari kubwa itakuwa ni kwa watoto na sifa mbaya kwa marehemu mbele ya jamii na kanisa!
 
Natamani Mwl Nyerere afufuke azabe vibao hao akina mizengo.
 
Rest in peace John nyerere umetangulia nasi tunafata poleni sana familia ya John nyerere kwa msiba huu mzito tunaungana nanyi kwenye kipindi hichi kigumu.
 
Back
Top Bottom