John Nyerere kuagwa leo, Msasani

John Nyerere kuagwa leo, Msasani

Wapo wengine wanajulikana sana, na hapa jukwaani tuna wawili, Andrew Nyerere na Yericko Nyerere . Kaka yao Makongoro ni maarufu pia na anatajwa kurithi viatu vya Jakaya.

Atavirithi hukohuko ccm na kukiweka pale makumbusho labda apewe kazi ya kutunza majina ya mafisadi khuku kwa wananchi makabwela tumaini letu ni UKAWA.
 
Last edited by a moderator:
Watanzania mbalimbali wanaendelea kufika nyumbani kwa Mwalimu Msasani kwa ajili ya kutoa pole na kujianda kuaga mwli wa marehemu John Nyerere.
John-Nyerere-115x85.jpg
Marehemu John Nyerere enzi za Uhai wake akiwa Mwanajeshi wa Kikosi cha Anga cha Jeshi La Wananchi Tanzania [JWTZ]
jon.jpg
Kitabu cha Rambirambi kilichoko Msasani Dar es Salaam
 
Ni ndo mwanajeshi wa kwanza kufariki kwenye hili Taifa ?? au mwana wa Jullius ?? wengine ndo tunatua hii ardhi sasa hivi...... mods hebu sogezeni hizi habari kwenye jukwaa la mambo mengine
 
Mwanadamu ye yote aliyezaliwa na mwanamke afahamu siku zake za kuishi siyo nyingi. Ni miaka 70 na kama ana nguvu ni miaka 80 na tena imejaa taabu. Mwili huyarudia mavumbi ambamo ulitoka lakini roho huenda hukumuni. Kwa aliyekuwa anamwamini Yesu anakwenda mbinguni na kwa wale waliomkataa motoni. Hakuna cha toharani. (Waebrani 9:27) . Fanya uamuzi sasa kwa kuwa hakuna mwingine mwenye mbingu isipokuwa Yesu Kristo.
 
Huyu hata sijawahi kumsikia....Angetufaa kweli kama kiongozi ila ndio kapendwa zaidi... RIP John Nyerere; dad, broo
 
Wewe ndio hujui, hao waliokuambia wanaitwa akina nani nyerere? Huyu ni mtoto wa mwalimu na jina lithibitisha.
Kuwa na jina linalofanana la Nyerere, hakumaanishi ni mtoto wa mwalimu, mbona watu wengi tu wanafanana majina na hawana uhusiano wowote??Acheni ujuha mmeshupalia huyu jamaa huku mmeshaambiwa hana uhusiano wowote na familia ya mwalimu hilo ni jina tu kama majina mengine..RIP kamanda John Guido Nyerere.
 
Ni ndo mwanajeshi wa kwanza kufariki kwenye hili Taifa ?? au mwana wa Jullius ?? wengine ndo tunatua hii ardhi sasa hivi...... mods hebu sogezeni hizi habari kwenye jukwaa la mambo mengine

Kuwa na utu kidogo ndugu, huyu ni kaka wa mwana JF mwenzetu Yericko Nyerere
 
Last edited by a moderator:
Ni ndo mwanajeshi wa kwanza kufariki kwenye hili Taifa ?? au mwana wa Jullius ?? wengine ndo tunatua hii ardhi sasa hivi...... mods hebu sogezeni hizi habari kwenye jukwaa la mambo mengine
Mbona kama una jazba???? Kama umekerwa si ufungue sehemu nyingine.... Au nawe una shida na jina Nyerere?????????????
 
Kuwa na jina linalofanana la Nyerere, hakumaanishi ni mtoto wa mwalimu, mbona watu wengi tu wanafanana majina na hawana uhusiano wowote??Acheni ujuha mmeshupalia huyu jamaa huku mmeshaambiwa hana uhusiano wowote na familia ya mwalimu hilo ni jina tu kama majina mengine..RIP kamanda John Guido Nyerere.
Huyu Yericko Nyerere ni mtoto wa mwalimu, kama unashida na hilo nenda RITA au andamana.
 
Last edited by a moderator:
nasikiaaa huyu marehemu alikuwa chini ya uangalizi maalumu zaidi ya miaka 30??
 
Poleni wafiwa kwa kuondokewa na mpendwa wenu,Bwana awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu!
 
haya kaka...na Stive Nyerere ni bandugu yao?

Steve Nyerere yule ni muigizaji na lile ni jina lake la uigizaji kama alivyo Masanja, Joti na Mpoki. Yericko Nyerere ni jina lake amefuata jina la ukoo wa baba yake. Nashangaa vile mmemkomalia mtoto wa mwalimu kwani yeye anatofauti gani na Makongoro na Madaraka?
 
Last edited by a moderator:
Nawe acha umalaya kwenye mambo ya msingi.
Uelezwe mara ngapi kuwa Yericko hana mahusiano yoyote na ukoo wa Burito?
Unahaha huku kote kwa faida ya nani?
Naona unatafuta nikutukane ili nifungiwe, sasa nakuambia tukana unavyoweza ila Yericko Nyerere ni mtoto wa mwalimu kama inakukera na wewe jiite kipuyo Nyerere
 
Last edited by a moderator:
Mwanadamu ye yote aliyezaliwa na mwanamke afahamu siku zake za kuishi siyo nyingi. Ni miaka 70 na kama ana nguvu ni miaka 80 na tena imejaa taabu. Mwili huyarudia mavumbi ambamo ulitoka lakini roho huenda hukumuni. Kwa aliyekuwa anamwamini Yesu anakwenda mbinguni na kwa wale waliomkataa motoni. Hakuna cha toharani. (Waebrani 9:27) . Fanya uamuzi sasa kwa kuwa hakuna mwingine mwenye mbingu isipokuwa Yesu Kristo.

Mbona mzee mwinyi anadunda tu na miaka yake tisini?
 
Back
Top Bottom