GE2025 John Mnyika: Hotuba ya kwanza ya Rais Haramu haijaonesha matumaini kwa watanzania, yeye na Serikali yake dhalimu wafanye toba

GE2025 John Mnyika: Hotuba ya kwanza ya Rais Haramu haijaonesha matumaini kwa watanzania, yeye na Serikali yake dhalimu wafanye toba

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Msolo

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2008
Posts
3,829
Reaction score
5,269
Kutoka account ya X ya CHADEMA

WARAKA NAMBA 03 WA 2025

Ujumbe wa Katibu Mkuu Na. 3 wa 2025: Juu ya Hotuba ya Rais Haramu ya 3/11/2025 na maombolezo ya wafia demokrasia, uhuru na haki ya tarehe 5 mpaka 11 Novemba 2025.

Makamanda, wapendwa na ndugu nawasalimu kwa salamu zote za Chama na salamu za imani zenu kwa Mungu.

Naomba mrejee taarifa kwa umma niliyotoa tarehe 2 Novemba 2025, hotuba ya Rais Haramu ya tarehe 3 Novemba 2025 na tangazo la Mkurugenzi wa Mawasiliano Chadema la tarehe 4 Novemba 2025.

Kwa mara nyingine nitoe pole kwa familia za marehemu wafia haki, uhuru na demokrasia kutokana na uchafuzi wa mwaka 2025 kabla, wakati na baada ya uchafuzi huo.

Nakuomba wewe unayesoma ujumbe huu uungane nami kusimama dakika moja kwa heshima ya marehemu wetu na tumwombe Mwenyezi Mungu azilaze roho zao katika haki, amani na furaha ya milele.

Kwa wagonjwa nawatakia heri katika matibabu na ni sala yangu kuwa Mwenyezi Mungu awajalie neema ya uponaji.

Kimsingi hakukuwa na uchaguzi 2025. Na tunawashukuru Watanzania kwa kutekeleza kwa namna mbalimbali maamuzi ya No Reforms No Election. Mwenyezi Mungu awajaze rehema na baraka kwa majitoleo yenu.

Natambua kwa Chadema tuko kwenye kipindi cha maombolezo ya wiki moja kuanzia tarehe 5 mpaka 11 Novemba 2025 ambapo bendera za Chama zinapepea nusu mlingoti. Nashukuru wote walioungana nasi kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Naiasa Serikali dhalimu nayo kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Na nawaomba wadau wote wa haki, demokrasia na uhuru nanyi kutangaza maombolezo kila mmoja kwa namna yake. Nawaomba viongozi wa dini, kiroho na wote mnaothamini uhai na utu nanyi kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Taifa letu linahitaji toba na uponyaji na hatua mojawapo muhimu katika mchakato huo ni maombolezo ya marehemu wa maafa ya kinachoitwa na watawala haramu na vyombo vyao "Uchaguzi Mkuu 2025".

Pamoja na kuwa katika kipindi cha maombolezo nimelazimika kuandika ujumbe huu kutokana na upotoshaji unaoendelea kufuatia hotuba ya Rais Haramu ya tarehe 3 Novemba 2025 kabla haijaleta taathira na madhara zaidi.

Ni udhalimu na udhaifu kwa Rais Haramu kuanza hotuba yake ya mara baada ya kuapa kwa kushika Quran kuanza kwa kusema uongo kwa kuipongeza Tume ya Uchaguzi isiyokuwa huru kwa "kuendesha uchaguzi kwa ufanisi usiotiliwa shaka". Toba na tiba kwa Taifa inaanza kwa kuwa wakweli mbele ya Mungu na watu ambao ni Sauti ya Mungu. Rais Haramu anapaswa kujirudi kwa kukiri ukweli hadharani kwa kuwa uongo wake umefanya vyombo vyake na wafuasi wake kuchukua mwelekeo wa kuwa hakuna tatizo kwenye taifa letu lenye kuhitaji suluhisho la haraka.

Rais Haramu amehamisha lawama ya mgawanyiko wa uchafuzi mkuu 2025 bila kujitazama ndani na kujikumbusha ukweli kuwa mgawanyiko huo ni matokeo ya kiburi chake, cha Serikali yake na Chama chake CCM kukataa kusikiliza sauti ya watu, sauti ya vyama vya kweli vya upinzani na sauti za wadau wengine muhimu waliotaka reforms kabla ya uchaguzi mkuu 2025 kwa kufanya marekebisho ya kikatiba, kisheria na kitaasisi kuweka mazingira ya kuwa na chaguzi huru na haki. Sauti ambazo zimepazwa kwa nyakati na njia mbalimbali toka aliporithi urais Machi 2021.

Mwito wa kutaka maisha yaendelee kama kawaida ni mwito wenye nia ovu ya kufunika kombe mwanaharamu apite. Maisha hayapaswi kuendelea kama yalivyokuwa kwa kiwango cha mauaji kilichofanyika na uwepo wa Viongozi Haramu madarakani wasiotokana na kura za kweli za wananchi wengi na walioapishwa kwa matokeo ya uongo bila hatua za haraka za toba na tiba kwa Taifa.

Amri yake ya vyombo vya dola kuchunguza ina nia ovu ya kuficha ukweli na kuhamisha mzigo wa tuhuma za mauaji na kukwepa uwajibikaji. Tayari matokeo ya amri hiyo ni kamata kamata inayoendelea ya viongozi wa Chadema na hatari ya kupika ushahidi. Tayari Makamu Mwenyekiti wa Chadema John Heche aliyekuwa mahabusu kabla hata ya uchaguzi kwa tuhuma za makosa ya Uhamiaji yenye dhamana amebadilishiwa makosa na sasa anatuhumiwa kwa ugaidi. Amri hiyo imekuwa na itakuwa na athari mbaya zaidi kwa walioko mahabusu za polisi kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025.

Vyombo vya dola havipaswi kuachiwa kujichunguza kwa kuwa ni watuhumiwa wakuu wa vitendo vya utekaji vya kabla ya uchaguzi na mauaji ya wakati na baada ya uchaguzi. Hivyo, Wananchi na wadau tuungane kutaka hatua tatu za pamoja na sambamba:
1. Kuundwa kwa Tume ya Ukweli, Haki na Upatanishi kwa mapendekezo kutoka Taasisi za kitaifa za dini, za kiraia na kisiasa zenye kuaminika.
2. Tume ya Kijaji ya Uchunguzi na 3. Kuja kwa Vyombo vya Kimataifa vya Uchunguzi vya Umoja wa Mataifa (UN) na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kama nilivyotoa mwito kupitia taarifa kwa umma ya tarehe 2 Novemba 2025.

Rais Haramu hana uhalali kutoa onyo kwa wanaotuhumiwa kufanya vurugu bila yeye mwenyewe kwanza kujipa onyo kwa mipango yake na ya vyombo vyake kabla, wakati na baada ya uchaguzi iliyosababisha vurugu za vyombo vya dola na vikundi vingine haramu dhidi ya wananchi waliopanga kufurahia haki na uhuru wao wa kuandamana kwa amani na raia wengine waliouwawa ambao hawakuwa wanashiriki maandamano. Adhabu ya kutuhumiwa kuvunja sheria haikupaswa kuwa kuuliwa kwa risasi: hizi ni vurugu za dola zinazohitaji wahusika katika vyombo vya dola kuchukuliwa hatua. Ni nani wa kumuonya na kumchukulia hatua yeye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo hivyo wakati wote wa vurugu hizo na mauaji hayo?

Juu ya kauli tupu ya Rais Haramu ya kutaka mazungumzo ni vyema akakumbuka na umma ukakumbuka kuwa Chadema wakati wote imekuwa tayari kwa mazungumzo. Ndio maana tuliomba mazungumzo 2019 na aliyekuwa Rais Magufuli baada ya uporaji wa uchaguzi wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji 2019 tukapuuzwa. Tuliomba tena mazungumzo na Rais Samia 2021 mara baada ya Mwenyezi Mungu kufungua Ukurasa Mpya kwa Nchi yetu na tukakubali kushiriki mazungumzo 2022 na 2023. Hata hivyo ni Rais Samia, na Serikali yake na Chama chake ndio walikwamisha mazungumzo wakati huo kwa kukataa mapendekezo yote ya kukwamua na kukamilisha mchakato wa katiba mpya na pia kukataa mapendekezo yote ya marekebisho ya katiba na marekebisho ya maana ya sheria na kitaasisi kuwezesha chaguzi za 2024 na 2025 kuwa huru na haki.

Iwapo kauli ya sasa ya Rais Haramu sio ya kinafiki basi itanguliwe na na toba na tiba ya sasa ya mazungumzo ihusishe pia wasuluhishi na usuluhishi wa haraka kwa kuwa Taifa liko katika mgogoro mkubwa. Mazungumzo ya sasa yatengeneze mazingira ya dharura ya pamoja na mambo mengine kuwezesha kufanyika kwa uchaguzi huru na haki. Chadema tuko tayari kwa mazungumzo ya kweli, huru na ya haki kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Chadema ibara ya 3.2 katika itikadi yake ya mrengo wa kati Chadema inaamini katika siasa zilizo juu ya Vyama zenye kuzingatia zaidi maslahi ya Taifa. Katika mazungumzo hayo uhusika wa umma ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi wenye kuaminika na kukubalika upewe kipaumbele tukirejea falsafa yetu ya people's power (Nguvu ya Umma).

Kitendo cha Rais Haramu kunukuu kipande cha hotuba ya Hayati Rais Mkapa ya mwaka 2000 ya kukataa kutekeleza maagizo ya waangalizi wa kimataifa wa Uchaguzi haramu uliosababisha mauaji Zanzibar 2001 kunaashiria kuwa hayuko tayari kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na waangalizi wa kimataifa ambao wamekwisha tangaza kupitia taarifa zao za awali kuwa unaoitwa uchaguzi mkuu wa 2025 Tanzania haukuwa huru wala wa haki.

Rais Haramu alipaswa kuzingatia kuwa Rais Mkapa katika kitabu cha maisha yake alichoandika kabla ya kufariki kwake alijutia matendo yake na ya Serikali yake mintaarafu uchaguzi wa Zanzibar wa 2000 hivyo hakupaswa kuitumia hotuba yake kama rejea kuhalalisha udhalimu wa mwaka 2025.

Hotuba yake hii ya kwanza haijaonyesha majuto wala unyenyekevu wa kustahili kujiita kuwa ni "Mtumishi Mkuu wa Maendeleo Endelevu" bali inamfanya apate tuhuma mbele ya umma ya kuwa "Mhusika Mkuu wa ama Mauaji Endelevu au Matendo Maovu Endelevu". Kazi na utu haipaswi kuwa kazi ya uuaji. Hotuba yake haijazingatia misingi aliyoitaja ya kutaka tuwe na taifa lenye umoja, upendo na amani. Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kwamba hakutaja kabisa msingi mkuu wa haki ambao ni wa lazima kwa taifa kuwa na upendo, utu, umoja, matumaini, furaha na amani.

Rais Haramu ametoa tafsiri potofu kuwa Demokrasia sio uchaguzi bali matendo ya baada ya uchaguzi. Umma ni vyema uzingatie kuwa Demokrasia ikiwa ni utawala unaoundwa na watu kwa ajili ya watu ni vyote viwili- nani wamechaguliwa na wanatawala namna gani. Hivyo jaribio lolote la kuwaghilibu na kuwarubuni Wananchi kusahau uwepo wa utawala Haramu madarakani linapawa kupuuzwa na wapenda haki, demokrasia, mabadiliko, uhuru, ukweli na uadilifu ndani ya nchi yetu na katika Jumuiya ya Kimataifa. Hatua ya kuponya inapaswa kutanguliwa na kutambua kuwa kuna ugonjwa.

Nakubaliana naye kuwa Tanzania ni kubwa kuliko mtu. Hivyo, Serikali iliyopo (kwa maana ya utumishi halali na wa haki wa umma wenye ueledi na Maadili) , Viongozi wa Dini wenye Roho ya Ucha Mungu, vyama vya siasa vyenye kuheshimu sauti za watu, Jumuiya Huru zisiingie kwenye mtego na kumtetea Rais Haramu na Viongozi wengine haramu kwa kuwafanya kuwa wakubwa kuliko Tanzania.

Badala yake waendelee kuheshimu sauti za watu na nguvu ya umma inayotaka Reforms, Reconciliation na Rebuilding kupitia Katiba Mpya na uwepo madarakani viongozi wa kuchaguliwa na Wananchi kupitia kufanyika kwa uchaguzi huru na haki kwa haraka.

Ni udhalimu na kinyume na utu kwa Rais Haramu kuanzia hotuba yake bila walau kutaka watu kusimama dakika moja kwa heshima kwa maafa ya Mauaji yaliyotokana na uchafuzi wake; lakini ni udhalimu zaidi na uovu kumaliza hotuba yake bila kutangaza maombolezo ya Kitaifa na kuagiza bendera kupepea nusu mlingoti sanjari na kuagiza misaada ya mazishi kutolewa kwa familia za waliouwawa kuwawezesha kusitiriwa kwa haraka.

Narejea kuwaomba tuendelee na maombolezo tukiweka kumbukumbu za wafia haki, uhuru na demokrasia wote wa matukio na matokeo ya tarehe 29 Oktoba mpaka sasa.

Katika kipindi hiki ambacho bado pia Chadema tunazuiwa kukusanyika na kufanya vikao kutokana na zuio ovu la tarehe 10 Juni 2025.

Nihitimishe ujumbe huu kuendelea kutaka na kusisitiza:

Mosi, Waliouwawa wapewe mazishi yenye heshima, kumbukumbu zao zihifadhiwe na familia zao zilipwe fidia.

Pili, Vyombo huru vya Uchunguzi vya Kimataifa vije kuchunguza udhalimu iliofanyika kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

Tatu, hakuna uchaguzi halali iliofanyika Tanzania tarehe 29 Oktoba 2025 hivyo matokeo yaliyotangazwa tarehe 1 Novemba 2025 ni batili na haramu.

Nne, Mwenyekiti Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti John Heche, viongozi wengine na wananchi waliofanywa mahabusu na wafungwa wa kisiasa kufuatia msimamo wa Chadema na wa umma wa No Reforms No Election waachiwe huru bila masharti yoyote.

Tano, Taasisi ya Chadema iliyo kwenye kifungo cha kisiasa kwa kuzuiwa kutumia rasilimali zake na kufanya shughuli za kisiasa tangu tarehe 10 Juni 2025 iachiliwe huru kwa maombi yenye nia ovu kufutwa ili kutuwezesha kutumia haki zake na zetu za kikatiba na kutimiza majukumu yake na yetu kwa taifa kwa Taifa katika wakati huu muhimu kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Haki huinua Taifa (Mithali 14:34) na haki na amani vinabusiana (Zaburi 85:10) wenye kutoa hukumu dhidi yetu na dhidi ya wengine watoe hukumu kwa haki (Quran 4:58) na Haki ifanywe kipaumbele (Quran 16:90) tudumishe Tanzania ya uhuru na umoja na zaidi tujenge Tanzania mpya yenye haki na furaha ambavyo ni vilele vya amani ya kweli.

John Mnyika
Katibu Mkuu
06/11/2025

1762433263512.png
 
Mnyika atangaze mwaka mmoja wa maombolezo na siyo siku saba tu. Ndani ya mwaka mmoja bendera zote za CHADEMA zipepee nusu mlingoti. Na chama kiwatafute wafiwa na kiwafariji..

Hii itasiaidia kupunguza jitihada za CCM kujaribu kubuy time ili wakiamini umma utasahau.
 
Kutoka account ya X ya CHADEMA

WARAKA NAMBA 03 WA 2025

Ujumbe wa Katibu Mkuu Na. 3 wa 2025: Juu ya Hotuba ya Rais Haramu ya 3/11/2025 na maombolezo ya wafia demokrasia, uhuru na haki ya tarehe 5 mpaka 11 Novemba 2025.

Makamanda, wapendwa na ndugu nawasalimu kwa salamu zote za Chama na salamu za imani zenu kwa Mungu.

Naomba mrejee taarifa kwa umma niliyotoa tarehe 2 Novemba 2025, hotuba ya Rais Haramu ya tarehe 3 Novemba 2025 na tangazo la Mkurugenzi wa Mawasiliano Chadema la tarehe 4 Novemba 2025.

Kwa mara nyingine nitoe pole kwa familia za marehemu wafia haki, uhuru na demokrasia kutokana na uchafuzi wa mwaka 2025 kabla, wakati na baada ya uchafuzi huo.

Nakuomba wewe unayesoma ujumbe huu uungane nami kusimama dakika moja kwa heshima ya marehemu wetu na tumwombe Mwenyezi Mungu azilaze roho zao katika haki, amani na furaha ya milele.

Kwa wagonjwa nawatakia heri katika matibabu na ni sala yangu kuwa Mwenyezi Mungu awajalie neema ya uponaji.

Kimsingi hakukuwa na uchaguzi 2025. Na tunawashukuru Watanzania kwa kutekeleza kwa namna mbalimbali maamuzi ya No Reforms No Election. Mwenyezi Mungu awajaze rehema na baraka kwa majitoleo yenu.

Natambua kwa Chadema tuko kwenye kipindi cha maombolezo ya wiki moja kuanzia tarehe 5 mpaka 11 Novemba 2025 ambapo bendera za Chama zinapepea nusu mlingoti. Nashukuru wote walioungana nasi kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Naiasa Serikali dhalimu nayo kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Na nawaomba wadau wote wa haki, demokrasia na uhuru nanyi kutangaza maombolezo kila mmoja kwa namna yake. Nawaomba viongozi wa dini, kiroho na wote mnaothamini uhai na utu nanyi kutangaza maombolezo ya Kitaifa. Taifa letu linahitaji toba na uponyaji na hatua mojawapo muhimu katika mchakato huo ni maombolezo ya marehemu wa maafa ya kinachoitwa na watawala haramu na vyombo vyao "Uchaguzi Mkuu 2025".

Pamoja na kuwa katika kipindi cha maombolezo nimelazimika kuandika ujumbe huu kutokana na upotoshaji unaoendelea kufuatia hotuba ya Rais Haramu ya tarehe 3 Novemba 2025 kabla haijaleta taathira na madhara zaidi.

Ni udhalimu na udhaifu kwa Rais Haramu kuanza hotuba yake ya mara baada ya kuapa kwa kushika Quran kuanza kwa kusema uongo kwa kuipongeza Tume ya Uchaguzi isiyokuwa huru kwa "kuendesha uchaguzi kwa ufanisi usiotiliwa shaka". Toba na tiba kwa Taifa inaanza kwa kuwa wakweli mbele ya Mungu na watu ambao ni Sauti ya Mungu. Rais Haramu anapaswa kujirudi kwa kukiri ukweli hadharani kwa kuwa uongo wake umefanya vyombo vyake na wafuasi wake kuchukua mwelekeo wa kuwa hakuna tatizo kwenye taifa letu lenye kuhitaji suluhisho la haraka.

Rais Haramu amehamisha lawama ya mgawanyiko wa uchafuzi mkuu 2025 bila kujitazama ndani na kujikumbusha ukweli kuwa mgawanyiko huo ni matokeo ya kiburi chake, cha Serikali yake na Chama chake CCM kukataa kusikiliza sauti ya watu, sauti ya vyama vya kweli vya upinzani na sauti za wadau wengine muhimu waliotaka reforms kabla ya uchaguzi mkuu 2025 kwa kufanya marekebisho ya kikatiba, kisheria na kitaasisi kuweka mazingira ya kuwa na chaguzi huru na haki. Sauti ambazo zimepazwa kwa nyakati na njia mbalimbali toka aliporithi urais Machi 2021.

Mwito wa kutaka maisha yaendelee kama kawaida ni mwito wenye nia ovu ya kufunika kombe mwanaharamu apite. Maisha hayapaswi kuendelea kama yalivyokuwa kwa kiwango cha mauaji kilichofanyika na uwepo wa Viongozi Haramu madarakani wasiotokana na kura za kweli za wananchi wengi na walioapishwa kwa matokeo ya uongo bila hatua za haraka za toba na tiba kwa Taifa.

Amri yake ya vyombo vya dola kuchunguza ina nia ovu ya kuficha ukweli na kuhamisha mzigo wa tuhuma za mauaji na kukwepa uwajibikaji. Tayari matokeo ya amri hiyo ni kamata kamata inayoendelea ya viongozi wa Chadema na hatari ya kupika ushahidi. Tayari Makamu Mwenyekiti wa Chadema John Heche aliyekuwa mahabusu kabla hata ya uchaguzi kwa tuhuma za makosa ya Uhamiaji yenye dhamana amebadilishiwa makosa na sasa anatuhumiwa kwa ugaidi. Amri hiyo imekuwa na itakuwa na athari mbaya zaidi kwa walioko mahabusu za polisi kabla, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025.

Vyombo vya dola havipaswi kuachiwa kujichunguza kwa kuwa ni watuhumiwa wakuu wa vitendo vya utekaji vya kabla ya uchaguzi na mauaji ya wakati na baada ya uchaguzi. Hivyo, Wananchi na wadau tuungane kutaka hatua tatu za pamoja na sambamba:
1. Kuundwa kwa Tume ya Ukweli, Haki na Upatanishi kwa mapendekezo kutoka Taasisi za kitaifa za dini, za kiraia na kisiasa zenye kuaminika.
2. Tume ya Kijaji ya Uchunguzi na 3. Kuja kwa Vyombo vya Kimataifa vya Uchunguzi vya Umoja wa Mataifa (UN) na Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) kama nilivyotoa mwito kupitia taarifa kwa umma ya tarehe 2 Novemba 2025.

Rais Haramu hana uhalali kutoa onyo kwa wanaotuhumiwa kufanya vurugu bila yeye mwenyewe kwanza kujipa onyo kwa mipango yake na ya vyombo vyake kabla, wakati na baada ya uchaguzi iliyosababisha vurugu za vyombo vya dola na vikundi vingine haramu dhidi ya wananchi waliopanga kufurahia haki na uhuru wao wa kuandamana kwa amani na raia wengine waliouwawa ambao hawakuwa wanashiriki maandamano. Adhabu ya kutuhumiwa kuvunja sheria haikupaswa kuwa kuuliwa kwa risasi: hizi ni vurugu za dola zinazohitaji wahusika katika vyombo vya dola kuchukuliwa hatua. Ni nani wa kumuonya na kumchukulia hatua yeye aliyekuwa Amiri Jeshi Mkuu wa vyombo hivyo wakati wote wa vurugu hizo na mauaji hayo?

Juu ya kauli tupu ya Rais Haramu ya kutaka mazungumzo ni vyema akakumbuka na umma ukakumbuka kuwa Chadema wakati wote imekuwa tayari kwa mazungumzo. Ndio maana tuliomba mazungumzo 2019 na aliyekuwa Rais Magufuli baada ya uporaji wa uchaguzi wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji 2019 tukapuuzwa. Tuliomba tena mazungumzo na Rais Samia 2021 mara baada ya Mwenyezi Mungu kufungua Ukurasa Mpya kwa Nchi yetu na tukakubali kushiriki mazungumzo 2022 na 2023. Hata hivyo ni Rais Samia, na Serikali yake na Chama chake ndio walikwamisha mazungumzo wakati huo kwa kukataa mapendekezo yote ya kukwamua na kukamilisha mchakato wa katiba mpya na pia kukataa mapendekezo yote ya marekebisho ya katiba na marekebisho ya maana ya sheria na kitaasisi kuwezesha chaguzi za 2024 na 2025 kuwa huru na haki.

Iwapo kauli ya sasa ya Rais Haramu sio ya kinafiki basi itanguliwe na na toba na tiba ya sasa ya mazungumzo ihusishe pia wasuluhishi na usuluhishi wa haraka kwa kuwa Taifa liko katika mgogoro mkubwa. Mazungumzo ya sasa yatengeneze mazingira ya dharura ya pamoja na mambo mengine kuwezesha kufanyika kwa uchaguzi huru na haki. Chadema tuko tayari kwa mazungumzo ya kweli, huru na ya haki kwa kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Chadema ibara ya 3.2 katika itikadi yake ya mrengo wa kati Chadema inaamini katika siasa zilizo juu ya Vyama zenye kuzingatia zaidi maslahi ya Taifa. Katika mazungumzo hayo uhusika wa umma ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi wenye kuaminika na kukubalika upewe kipaumbele tukirejea falsafa yetu ya people's power (Nguvu ya Umma).

Kitendo cha Rais Haramu kunukuu kipande cha hotuba ya Hayati Rais Mkapa ya mwaka 2000 ya kukataa kutekeleza maagizo ya waangalizi wa kimataifa wa Uchaguzi haramu uliosababisha mauaji Zanzibar 2001 kunaashiria kuwa hayuko tayari kutekeleza mapendekezo yaliyotolewa na waangalizi wa kimataifa ambao wamekwisha tangaza kupitia taarifa zao za awali kuwa unaoitwa uchaguzi mkuu wa 2025 Tanzania haukuwa huru wala wa haki.

Rais Haramu alipaswa kuzingatia kuwa Rais Mkapa katika kitabu cha maisha yake alichoandika kabla ya kufariki kwake alijutia matendo yake na ya Serikali yake mintaarafu uchaguzi wa Zanzibar wa 2000 hivyo hakupaswa kuitumia hotuba yake kama rejea kuhalalisha udhalimu wa mwaka 2025.

Hotuba yake hii ya kwanza haijaonyesha majuto wala unyenyekevu wa kustahili kujiita kuwa ni "Mtumishi Mkuu wa Maendeleo Endelevu" bali inamfanya apate tuhuma mbele ya umma ya kuwa "Mhusika Mkuu wa ama Mauaji Endelevu au Matendo Maovu Endelevu". Kazi na utu haipaswi kuwa kazi ya uuaji. Hotuba yake haijazingatia misingi aliyoitaja ya kutaka tuwe na taifa lenye umoja, upendo na amani. Ni jambo la kushangaza na kusikitisha kwamba hakutaja kabisa msingi mkuu wa haki ambao ni wa lazima kwa taifa kuwa na upendo, utu, umoja, matumaini, furaha na amani.

Rais Haramu ametoa tafsiri potofu kuwa Demokrasia sio uchaguzi bali matendo ya baada ya uchaguzi. Umma ni vyema uzingatie kuwa Demokrasia ikiwa ni utawala unaoundwa na watu kwa ajili ya watu ni vyote viwili- nani wamechaguliwa na wanatawala namna gani. Hivyo jaribio lolote la kuwaghilibu na kuwarubuni Wananchi kusahau uwepo wa utawala Haramu madarakani linapawa kupuuzwa na wapenda haki, demokrasia, mabadiliko, uhuru, ukweli na uadilifu ndani ya nchi yetu na katika Jumuiya ya Kimataifa. Hatua ya kuponya inapaswa kutanguliwa na kutambua kuwa kuna ugonjwa.

Nakubaliana naye kuwa Tanzania ni kubwa kuliko mtu. Hivyo, Serikali iliyopo (kwa maana ya utumishi halali na wa haki wa umma wenye ueledi na Maadili) , Viongozi wa Dini wenye Roho ya Ucha Mungu, vyama vya siasa vyenye kuheshimu sauti za watu, Jumuiya Huru zisiingie kwenye mtego na kumtetea Rais Haramu na Viongozi wengine haramu kwa kuwafanya kuwa wakubwa kuliko Tanzania.

Badala yake waendelee kuheshimu sauti za watu na nguvu ya umma inayotaka Reforms, Reconciliation na Rebuilding kupitia Katiba Mpya na uwepo madarakani viongozi wa kuchaguliwa na Wananchi kupitia kufanyika kwa uchaguzi huru na haki kwa haraka.

Ni udhalimu na kinyume na utu kwa Rais Haramu kuanzia hotuba yake bila walau kutaka watu kusimama dakika moja kwa heshima kwa maafa ya Mauaji yaliyotokana na uchafuzi wake; lakini ni udhalimu zaidi na uovu kumaliza hotuba yake bila kutangaza maombolezo ya Kitaifa na kuagiza bendera kupepea nusu mlingoti sanjari na kuagiza misaada ya mazishi kutolewa kwa familia za waliouwawa kuwawezesha kusitiriwa kwa haraka.

Narejea kuwaomba tuendelee na maombolezo tukiweka kumbukumbu za wafia haki, uhuru na demokrasia wote wa matukio na matokeo ya tarehe 29 Oktoba mpaka sasa.

Katika kipindi hiki ambacho bado pia Chadema tunazuiwa kukusanyika na kufanya vikao kutokana na zuio ovu la tarehe 10 Juni 2025.

Nihitimishe ujumbe huu kuendelea kutaka na kusisitiza:

Mosi, Waliouwawa wapewe mazishi yenye heshima, kumbukumbu zao zihifadhiwe na familia zao zilipwe fidia.

Pili, Vyombo huru vya Uchunguzi vya Kimataifa vije kuchunguza udhalimu iliofanyika kabla, wakati na baada ya uchaguzi.

Tatu, hakuna uchaguzi halali iliofanyika Tanzania tarehe 29 Oktoba 2025 hivyo matokeo yaliyotangazwa tarehe 1 Novemba 2025 ni batili na haramu.

Nne, Mwenyekiti Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti John Heche, viongozi wengine na wananchi waliofanywa mahabusu na wafungwa wa kisiasa kufuatia msimamo wa Chadema na wa umma wa No Reforms No Election waachiwe huru bila masharti yoyote.

Tano, Taasisi ya Chadema iliyo kwenye kifungo cha kisiasa kwa kuzuiwa kutumia rasilimali zake na kufanya shughuli za kisiasa tangu tarehe 10 Juni 2025 iachiliwe huru kwa maombi yenye nia ovu kufutwa ili kutuwezesha kutumia haki zake na zetu za kikatiba na kutimiza majukumu yake na yetu kwa taifa kwa Taifa katika wakati huu muhimu kwa mustakabali mwema wa nchi yetu.

Haki huinua Taifa (Mithali 14:34) na haki na amani vinabusiana (Zaburi 85:10) wenye kutoa hukumu dhidi yetu na dhidi ya wengine watoe hukumu kwa haki (Quran 4:58) na Haki ifanywe kipaumbele (Quran 16:90) tudumishe Tanzania ya uhuru na umoja na zaidi tujenge Tanzania mpya yenye haki na furaha ambavyo ni vilele vya amani ya kweli.

John Mnyika
Katibu Mkuu
06/11/2025

View attachment 3498137
May the wrath of God Lord be upon that wicked woman and her demons-possessed agents and sycophants!
 
Mnyika atangaze mwaka mmoja wa maombolezo na siyo siku saba tu. Ndani ya mwaka mmoja bendera zote za CHADEMA zipepee nusu mlingoti. Na chama kiwatafute wafiwa na kiwafariji..

Hii itasiaidia kupunguza jitihada za CCM kujaribu kubuy time ili wakiamini umma utasahau.
Hii muhimu sana, tena wao wakiwa wahanga wa siasa kandamizi wafanye hivyo.
 
Hiyo hotuba ya Mnyika utafikiri imeandaliwa na jopo la wataalam kama 100 hivi kudadek
Hebu linganisha na ile ya Rais Haramu
 
Back
Top Bottom