John Magale Shibuda: Kilio cha samaki

John Magale Shibuda: Kilio cha samaki

Mleta mada umepote na umevurugwa sana, hasa wakati huu wa vuguvugu la mabadiliko. It is too late kwa wewe kujisahihisha, ila kikubwa ni kuwa JIANDAE KISAIKOLOJIA ​October 2015 imekaribia.
 
.... hawa jamaa zetu ni sikio la kufa...kaburi tu ndio dawa.
Du! unampango wa kuwapeleka kaburini? naona wenye ualbino jumuia ya kimataifa imewakataza kuua, vikongwe mmekatazwa kuua, sasa mmegeukia wapinzani mnatangaza kabisa kaburi ndo dawa yao. Nasikia mmetoa sadaka kwa njia ya ajali lkn mganga wenu kawaambia haitawasaidia hivyo mmechagua wapinzani. YAWEZEKANA MKAFANIKIWA YETU MACHO TUSUBIRI.
 
Hawa ndio vijana wa nchi hii ...... tena mwanamke mwenye elimu ya chuo kikuu .....laana ...
 
Ni kweli kabisa kwamba;mwanamke uliyeachana naye then akiwa anakutajataja ujue kuwa bado anakupenda.Yes..shonza alikwisha achana na chadema na sasa yupo ccm,ya nini unaitaja sana cdm?...Inaonekana cdm walikuwa wanakufikisha kwenyewe mpaka.....!!!???,Lakini baada ya kuachika na kuolewa na ccm,Inaonekana hawezi kazi hasa ikizingatiwa kuwa wewe bado ni kijana na unahitaji mara kwa mara na ccm kazeeka..so kimoja chali mpaka asubuhi..TULIA KWENYE NDOA YAKO MPYA,MICHEPUKO NI HATARI SHONZA!!!!
 
Nayajua usiyoyajua...ni heri ukakaa kimya.

wewe dada hujui kitu, acha kujifanya eti unayajua ya sirini, wewe hujui kitu, kaa kimya jenga ccm yako kama unao uwezo ingawa najua hata huko nako tayari umeshajizaraulisha.
 
Kwa umahiri wake katika siasa Mheshimiwa John Magale Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanasiasa wenzake walimpatia jina la DROGBA (Mshambuliaji hatari wa timu ya Chelsea wakati huo)

Mnamo Mwaka 2009 - 10, wakati wa kupanda kwa "joto la kisiasa" ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Shibuda akiwa ni mwanachama wa chama hicho na Mbunge pia, alipatwa na joto hilo, pale ambapo alipishana lugha na wenzie ndani ya Chama na baadae kufanya maamuzi ya hasira na kuhamia CHADEMA ambako alipokelewa kama LULU na kutangazwa nchi nzima na viongozi waandamizi wa Chama hicho.

Kwa namna ya mapokezi yake yalivyokuwa hakuna aliyeweza kuamini wala kutegemea kuwa huo ulikuwa ndio mwanzo wa kifo cha kisiasa cha mkongwe, nguli na mbabe huyo wa kisiasa hapa nchini.

Hakuna kilichomponza zaidi ya rekodi ya mafanikio yake, uwezo wake na utashi mkubwa alionao katika siasa za ndani na nje ya nchi, MAARIFA ya JOHN MAGALE SHIBUDA yaliwatia hofu Viongozi wa CHADEMA juu ya nafasi zao, vyeo vyao na hatma yao ndani ya Chama hicho.

Zengwe likaundwa, watu wakaandaliwa na vihunzi vikatengwa kuhakikisha kuwa SHIBUDA ananasa, anadhibitiwa na anapotezwa, ndivyo ilivyokuwa kwani muda mfupi tu, tuhuma zikaanza, malalamiko yakasikika na mishale ikarushwa kwa Shibuda, alikwepa mingi lakini hakuweza kukwepa yote, alitandikwa, akapewa jina MSALITI, akachafuka hatimae kupotezwa..

Kwangu mimi huyu bwana ni Mwalimu wa siasa, ni hazina na njia ya kuifuata katika mapito ya kisiasa. Namtafuta- DROGBA, nataka kuona umahiri wake, ufundi wake na maarifa yake hivi sasa akiwa na wakati mgumu kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.
Mwanzo wa thread mpaka mwisho ni UPUUZI...
Haya nenda kachukue ujira wako kwa Shibuda.
 
Hivi Shibuda nae ni mtu wa kuongelea,, yule si ana kauchiz flani
Kwa anayemfahamu huyu baba hawezi kumzungumzia hata chembe
 
Ni msaliti kabisa huyu Shibuda wala tusidanganyane NI NANI ALIYE KUWA AKITOA VIJEMBE PALE BUNGENI NA KWENDA KUFUNDA WATU WA CCM, Hicho kikombe hawezi kikwepa Shibuda!
 
Kaburi linawasubiri ccm na sio ukawa wala chadema hata matokeo ya chaguzi zilizopita na mikutano yao yanadhirisha kasi ya ukawa kwenda Tanzania kuzaliwa upya na ccm kuelekea kaburini haitaji degree kuliona hilo bali utashi na kuwa natathimini thabiti thats why wewe uko busy kuwakashifu na kuwasema ukawa na si chama kingine kama ACT na vinginevyo na kama ukawa ingekuwa inakufa wala msingehangaika navyo. Vip mmepostpone kufa kwa CHADEMA tena maana mlisema 2014 nashanga hadi sasa marehemu mliyemtabiria anazidi kuwapiga mabao na refa wa kwenu Je angekuwa refa wa kimataifa hali ingekuwaje Shoste Juliana
 
Kama ni mwalimu wa siasa mlilitoaje jina lake kwenye kura za maoni na kumuweka mwingine. Zengwe alimuhundia nani kama sio yeye mwenyewe labda nikukumbushe inawezekana umesahau maana uko ccm sio mahala salama unaweza kukuta washakupiga juju. Wabunge wa CHADEMA wanajipanga kutoa hoja za kumchallenge JK na kutoa msimamo wa kutokubaliana na utaratibu waliotumia kushinda kura za Urais na kudai tume huru ya uchaguzi, katiba mpya yeye kaende kuhudhuria sherehe za kuzindua bunge na kufakamia wali kinyume na msimamo wa cdm. Alipinga sera za CHADEMA bungeni za kukataa posho na kumkashifu Mh.KUB Mbowe (wakati ndio alitumia sera hizo kuomba kura na kupitishwa kuwa mbunge kwa tiketi yaCDM si angepinga toka anaomba ubunge) na kuhudhuria vikao vya ccm live
 
Aisee michango yako huwa inanifurahisha sana,pamoja na kuisema CHADEMA vibaya ukifikiri kuwa unaichafua ili watanzania waichukie ndiyo watanzania wanazidi kuipenda zaidi.

Unapo iombea kifo CHADEMA ndiyo Mungu ana zidi kuisitawisha na kuiongezea uhai zaidi na kuifanya watanzania waendelee kuiona kuwa hakuna chama kinachoweza kuwakomboa kutoka kwenye utumwa wa CCM zaidi ya CHADEMA.

Ndiyo maana tangu ulipoanza kuishambulia na kuiombea kifo CHADEMA kwa kushirikiana na wenzako mliotimliwa kwa pamoja, hakuna aliyeweza kuleta tathimini ya hasara iliyopata CHADEMA baada ya wewe na wenzako kutimliwa CHADEMA.
Chadema mpango wa Mungu, uongo babu..??
 
Kama ni mwalimu wa siasa mlilitoaje jina lake kwenye kura za maoni na kumuweka mwingine. Zengwe alimuhundia nani kama sio yeye mwenyewe labda nikukumbushe inawezekana umesahau maana uko ccm sio mahala salama unaweza kukuta washakupiga juju. Wabunge wa CHADEMA wanajipanga kutoa hoja za kumchallenge JK na kutoa msimamo wa kutokubaliana na utaratibu waliotumia kushinda kura za Urais na kudai tume huru ya uchaguzi, katiba mpya yeye kaende kuhudhuria sherehe za kuzindua bunge na kufakamia wali kinyume na msimamo wa cdm. Alipinga sera za CHADEMA bungeni za kukataa posho na kumkashifu Mh.KUB Mbowe (wakati ndio alitumia sera hizo kuomba kura na kupitishwa kuwa mbunge kwa tiketi yaCDM si angepinga toka anaomba ubunge) na kuhudhuria vikao vya ccm live
Nadhan haujamuelewa juliana, ebu soma tena bandiko lake, yeye anasema Akili kubwa haiwezi kuongozwa na akili ndogo..Anasema Shibuda ni fundi wa siasa Mbowe na timu yake wakaogopa uwezo wake...na ndio maana Shibuda alikuwa akikataa amri zao za kiboya..
 
Ni msaliti kabisa huyu Shibuda wala tusidanganyane NI NANI ALIYE KUWA AKITOA VIJEMBE PALE BUNGENI NA KWENDA KUFUNDA WATU WA CCM, Hicho kikombe hawezi kikwepa Shibuda!

Siasa sio vita na hakuna adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu kwenye siasa.
 
Ukawa ni mkombozi wa kweli na ndiye mwenye jehanumu ya kuunguza ufisadi wa Yeyote aliyekula vya watanzania Juliana una Jina la mama yangu lakini unaandika post za kipumbavu wewe ushapewa taraka kauze kimboka dizaini yako cdm haina mteja
 
Nadhan haujamuelewa juliana, ebu soma tena bandiko lake, yeye anasema Akili kubwa haiwezi kuongozwa na akili ndogo..Anasema Shibuda ni fundi wa siasa Mbowe na timu yake wakaogopa uwezo wake...na ndio maana Shibuda alikuwa akikataa amri zao za kiboya..

Kwa hiyo hata CCM alikimbia kwa kuwa alikuwa hakubaliani na amri za kiboya zilizokuwa zinatolewa na CCM?.
 
Hivi nyie vijana wa siku hizi huwa mna muda wa kutafakari maslahi mapana ya nchi kweli? Au nyie kazi yenu ni kuwa wapambe wa viongozi waliopo pekee?
 
Back
Top Bottom