John Magale Shibuda: Kilio cha samaki

John Magale Shibuda: Kilio cha samaki

Juliana Shonza

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2012
Posts
2,009
Reaction score
1,607
Kwa umahiri wake katika siasa Mheshimiwa John Magale Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wanasiasa wenzake walimpatia jina la DROGBA (Mshambuliaji hatari wa timu ya Chelsea wakati huo)

Mnamo Mwaka 2009 - 10, wakati wa kupanda kwa "joto la kisiasa" ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Shibuda akiwa ni mwanachama wa chama hicho na Mbunge pia, alipatwa na joto hilo, pale ambapo alipishana lugha na wenzie ndani ya Chama na baadae kufanya maamuzi ya hasira na kuhamia CHADEMA ambako alipokelewa kama LULU na kutangazwa nchi nzima na viongozi waandamizi wa Chama hicho.

Kwa namna ya mapokezi yake yalivyokuwa hakuna aliyeweza kuamini wala kutegemea kuwa huo ulikuwa ndio mwanzo wa kifo cha kisiasa cha mkongwe, nguli na mbabe huyo wa kisiasa hapa nchini.

Hakuna kilichomponza zaidi ya rekodi ya mafanikio yake, uwezo wake na utashi mkubwa alionao katika siasa za ndani na nje ya nchi, MAARIFA ya JOHN MAGALE SHIBUDA yaliwatia hofu Viongozi wa CHADEMA juu ya nafasi zao, vyeo vyao na hatma yao ndani ya Chama hicho.

Zengwe likaundwa, watu wakaandaliwa na vihunzi vikatengwa kuhakikisha kuwa SHIBUDA ananasa, anadhibitiwa na anapotezwa, ndivyo ilivyokuwa kwani muda mfupi tu, tuhuma zikaanza, malalamiko yakasikika na mishale ikarushwa kwa Shibuda, alikwepa mingi lakini hakuweza kukwepa yote, alitandikwa, akapewa jina MSALITI, akachafuka hatimae kupotezwa..

Kwangu mimi huyu bwana ni Mwalimu wa siasa, ni hazina na njia ya kuifuata katika mapito ya kisiasa. Namtafuta- DROGBA, nataka kuona umahiri wake, ufundi wake na maarifa yake hivi sasa akiwa na wakati mgumu kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba 2015.
 
Nchi hii ina watu wa ajabu sana.. hii umeandika kwa utashi wako au kwa shinikizo la M-pesa za Lumumba!!

Kama umeandika kwa utashi wako kuna mawili.. unaweza kua umelewa viroba original au una mihemko iliyopitiliza, tafuta vijana wakusaidie kutoa hiyo mihemko!!

Its a pity kwa vijana kua na upuuzi wa kiwango hichi... hatuwezi kuendelea kwa style hii aisee!!

Pathetic!
 
Mleta mada na Shibuda si wote mlikuwa mnalipwa na Zitto Zuberi Kabwe kuiua Chadema? +255714669850/75635903 na 0754465597 kuanzia 2011 hadi 2012 mlikuwa mnapokea kila mwezi siyo chini ya 200,000/=. Shibuda arudi CCM mkutane mpange mambo yenu kabla ya 25 Octoba 2015
 
Kwa sababu alitoka CCM na alipotea kwenda kwa CHADEMA bado anayohaki ya msingi kabisa kurudi kwenye chama chake cha zamani.............Sioni sababu za Juliana Shonza kila wakati kulaumu CHADEMA,hebu tuache kwanza tukijenge chama chetu..........Nadhani Shibuda ndiyo aliyoikataa kwanza CHADEMA............Ni vyema ukamshauri either arudi CCM au aanzishe chama chake kitakacho kubali matakwa yake.............

Pole Juliana kwa sasa tuko busy na KAMPENI ya SHAHADA YAKO TALAKA KWA CCM byeeeeeeeeeeeeee
 
huwa simuelewi shonz.uliishatoka chadema lakini kila kukicha ni chadema tu. juzi umesena dr slaa yuko nje ya nchi na ukapata mabango ya kutisha.kwanini usimpeleke ccn ili nyota ing'ae? nakubali intelejensia ya chadema ilifanya kaxi kubwa kuwafilter nyie virusi ndani ya chama. ukimuona xzk, mchange, kaijage yani nyote ni empty magazine. heko lwakatale kubaini mpango hovu na kufukuxia mbali virusi hvi
 
Juliana shoza, unakumbuka ulikua unacheo gan cdm 2010, naamini na ww ulishiriki kumpokea shibuda. Kwa sasa achana na cdm jenga chama chako au kama bado unaipenda cdm bas omba msamaha rud uwe mwanachama wa kawaida na ujipange zaid.
 
Mleta maada ni aina ya wanasiasa kama Shibuda. Hawana msimamo. Wanadhani kuhama vyama watapata kile wakitakacho kumbe ni kujidhaurisha mbele ya jamii.
 
uliana Shonza

Dadangu Juliana Shonza jitahidi kuwa mkweli. Shibuda hajapotezwa na Chadema bali kajipoteza mwenyewe. Pia kama ni kupotezwa na chama basi ccm ndiyo walioanza kumpoteza. Ukirejea kauli ya Hamis Mgeja (mwenyekiti wa ccm Shinyanga) aliwahi kunukuliwa akisema Shibuda amegundua kwamba hapendwi ndani ya ccm ndiyo maana akahamia upinzani. Sasa kwa kuwa ccm ndo chama chake kilichomlea basi mrudisheni na muwekeni kwenye ulingo wa siasa
 
Last edited by a moderator:
hahahahaha!! Like Shonza; Like Shibuda; two of a kind!! haha; Shibuda angekuwa Nguli wa siasa asingejichimbia kaburi akajizika mwenyewe kisiasa! Shibuda, ZZK na mleta mada hawana tofauti; when need is too high; logic suffers.; Nyota zilizozimika; Good riddance Shonza; Good riddance Shibuda, Good riddance ZZK, the modern day Judeas Iskariots!
 
Ukawa wanapenda kusifiwa tu kama wanawakeee oooh ww mzr sijui macho yako kama gololi nk

Ukiwaponda tu ujue matusi, kashfa na kujiona kama miungu watu hawakosei

Pumbafu kabisa mbona wezenu wasisiem wanakosolewa na husikii wakilalamika
 
Miongoni mwa watu ambao hua nina wasiwasi na utashi wao ni huyu Binti, naomba niishie hapa kwanza

Kama isingelikuwa "chuki binafsi" dhidi yangu basi ungeweza kuchangia kwa kiasi cha ufahamu ulichonacho, maana nafahamu uwezo wako hauishii kwenye kumjudge mtoa mada tu, inaendelea zaidi ya hapo.
 
Ukawa wanapenda kusifiwa tu kama wanawakeee oooh ww mzr sijui macho yako kama gololi nk

Ukiwaponda tu ujue matusi, kashfa na kujiona kama miungu watu hawakosei

Pumbafu kabisa mbona wezenu wasisiem wanakosolewa na husikii wakilalamika
Inahitaji akili na ufahamu kujua kuwa umekosea, na inahitaji hekima kukiri makosa, na inahitaji maarifa ya hali ya juu "kujisahihisha" kimsingi hawa jamaa zetu ni sikio la kufa...kaburi tu ndio dawa.
 
Back
Top Bottom