Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wachimbaji Madini Nchini (FEMATA), John Bina, amemwomba mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Samia Suluhu Hassan, kuchukua hatua dhidi ya watu wanaodaiwa kupanga maandamano Oktoba 29, 2025, siku ya Uchaguzi Mkuu.
Bina ametoa kauli hiyo leo, Oktoba 13, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika mkoani Geita, ambako Dk. Samia amehutubia wananchi na kunadi sera na ilani ya chama hicho.
“Wanaandamana ili iweje? Wakati fulani, kwa maslahi ya Watanzania zaidi ya milioni 60, usiwahurumie hawa,” amesema Bina, akisisitiza kuwa vitendo vya aina hiyo vinaweza kuhatarisha amani ya nchi.
Bina amesema kwa sasa kuna baadhi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kupandikiza chuki na kuhamasisha vurugu, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara makubwa kwa taifa.
“Tunaona watu mitandaoni wanavyojitokeza, wengine wanajifungia kwenye magari. Hivi kikinuka hapa tutakwenda wapi? Ningepewa Naibu IGP, ningewavuruga asubuhi,” ameongeza kwa msisitizo.
Kauli hiyo imekuja wakati wanasiasa na viongozi mbalimbali wa kijamii wakiendelea kuhimiza amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, ambapo Watanzania wanatarajiwa kujitokeza kupiga kura kwa amani.
Soma: Rais wa Wachimbaji Madini: Napendekeza moja ya madini tuyabadilishe jina yaitwe 'Samia Suluhu Hassan'
Bina ametoa kauli hiyo leo, Oktoba 13, 2025, katika mkutano wa kampeni uliofanyika mkoani Geita, ambako Dk. Samia amehutubia wananchi na kunadi sera na ilani ya chama hicho.
“Wanaandamana ili iweje? Wakati fulani, kwa maslahi ya Watanzania zaidi ya milioni 60, usiwahurumie hawa,” amesema Bina, akisisitiza kuwa vitendo vya aina hiyo vinaweza kuhatarisha amani ya nchi.
Bina amesema kwa sasa kuna baadhi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kupandikiza chuki na kuhamasisha vurugu, jambo ambalo linaweza kusababisha madhara makubwa kwa taifa.
“Tunaona watu mitandaoni wanavyojitokeza, wengine wanajifungia kwenye magari. Hivi kikinuka hapa tutakwenda wapi? Ningepewa Naibu IGP, ningewavuruga asubuhi,” ameongeza kwa msisitizo.
Kauli hiyo imekuja wakati wanasiasa na viongozi mbalimbali wa kijamii wakiendelea kuhimiza amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, ambapo Watanzania wanatarajiwa kujitokeza kupiga kura kwa amani.
Soma: Rais wa Wachimbaji Madini: Napendekeza moja ya madini tuyabadilishe jina yaitwe 'Samia Suluhu Hassan'