JKT na migomo vyuoni

JKT na migomo vyuoni

Dr Aluta

Senior Member
Joined
Apr 16, 2015
Posts
121
Reaction score
39
Poleni na majukumu wanaJF,

Mwaka jana nikiwa miongoni wa wahitimu wa kidato cha sita nilifanikiwa kwenda jeshin JKT. Wakati tupo jeshini, kauli mbiu ya maafande ilitutaka tuache migomo tukiwa chuoni. Walikemea kila kukicha wakijua ndo mwarobaini wa kuzima migomo chuoni.

Ilifikia kipindi nikajiuliza kilichotuleta huku ni migomo? Maana kila kuruta mkosefu alibashiriwa kuwa mgomaji chuoni. Haya, hebu tazama leo hali iliyopo vyuoni. Migomo ipo palepale!

Na sehemu kubwa ya wagomaj wamepitia JKT. Niseme tu, serikal ijikite katika utatuzi wa tatizo na sio vitisho jeshini. Wakumbuke kiumbe chenye uhai na mauti huongozwa na tamaa.

Nawasilisha.
 
CCM wanawaza kutumia masabuli, hata mtoto anaelewa kufuga mbwa hakuzuii wezi kuja, niliwahi mwambia mtu kuwa hichi wanachokifanya ccm kitawatokea puani siku moja, haiwezekani umpeleke mtu JKT alafu umyime haki zake na utegeemee atakuwa mtii na mtulivu eti kisa alipita JKT.

CCM na washirika wake watambue hayo ni mawazo mgando, mawazo hayo yalifaa sana karne ya 20 siyo kwa karne hii yenye utandawazi kila pahala, karne ambayo teknolojia imekua na inaendelea kukua na kuchangia watu kuwa na uelewa mpana siku hadi siku.

Wanachopaswa ni kutatua tu kero za wanafunzi hao basi. Vinginevyo hali itakuwa mbaya tena na hivi wakihitimu hawapati ajira ni hatari zaidi, imefika wakati tuelezane ukweli mambo ya zidumu fikra za mwenyekiti na ndiyoo mkuu yalikuwa hukoooo zamani za kale, zama hizi ni ndiyo au hapana kwisha.
 
Utawala ukifika mwisho mungu huwatia watawala upofu wasijue wanalotenda.mwisho ni 'menemene,tekeli na pereshi'
 
kwel kabsa mkuu yaan hata mm walikua wananshangaza sana migomo migomo.... mi naona ndo wameongeza ujuz kwa kifup hyo n trailer movie bado. haki haiwez pokonywa kwa vitisho
 
Mimi nimepata kusema mara nyingi,katika nchii kama hii ya kwetu,viongozi wetu hawajui kitu priority,,.mambo yenye umuhimu kidogo yanakuwa ya kwanza na yale yenye umuhimu mkubwa na impact kubwa kwa watu wengi yanakuwa ya mwisho

Kupeleka vijana National Service katika kipindi kama hiki ambacho taifa linakabiliwa na mambo mengi sana ya kufanya ni upotofu..Impact ya wao kwenda kule haionekani,leo wala kesho.Hakuna cha uzalendo,hakuna kujituma,kufanya kazi kwa bidii na uvumilivu hakuna,Migomo kama kawaida,yani tumepoteza pesa na muda na kuwafaidisha maafande tu kusimaisha minazi na dada zetu

Sidhani kama huwa wanafanya evaluation kuona ni kiasi gani lengo la kupeleka watu NS limefanikiwa,au wanaendekeza tu ushabiki wa kisiasa hapa..Sasa sisi tutaendelea kugoma kuikumbusha serikali kuwa hii nchi sio yao peke yao,hatuwezi kusoma tukiwa na njaa,,pesa za kuiba zipo kwa nini za kufanya mambo muhimu kama haya ya elimu hazipo

Inatia hasira
 
Hapo bado sasa, ngoma itanoga zaidi pale watakapo maliza vyuo na kuja mtaani kusugua viatu bila ajira tutegemee magenge ya wahalifu mara dufu coz mbinu zote za kijeshi wanazo na tusipo angalia soon makundi ya uasi (Mungu atuepushie hili) yataanza kuibuka Tanzania.
 
JKT kwa mujibu uje utie kelele hapa hata aibu huna we ungepitia jkt kwa kujitolea uujue uzalendo kwanza kwa nchi yako alafu tungeona kama utafanya ujinga huu wa migomo. Kwa mujibu nyinyi ndio ile mnapiga funika kombe mwanaharam apite kozi mtiemaji mtienaji miezi mitatu afu useme umepita jkt. Wewe pamoja na wenzio rudini tena jakata mkajifunze uzalendo kwa nchi yenu kwanza.
 
Chinga One
Kwa kozi hiyo ya kwa mujibu usifikiri ina impact mbaya kwa nchi serikali yenyewe inaakili kuliko wewe akuna mafunzo ya maana wanayoyapata yakusema eti utapata waasi wa maana laiti kama wakikaziwa kwenye kozi wahakikishe wanatoa makamanda wa vita hakuna atakae goma hata mmoja askari hagomi hao ni raia tu.
 
Last edited by a moderator:
JKT kwa mujibu uje utie kelele hapa hata aibu huna we ungepitia jkt kwa kujitolea uujue uzalendo kwanza kwa nchi yako alafu tungeona kama utafanya ujinga huu wa migomo. Kwa mujibu nyinyi ndio ile mnapiga funika kombe mwanaharam apite kozi mtiemaji mtienaji miezi mitatu afu useme umepita jkt. Wewe pamoja na wenzio rudini tena jakata mkajifunze uzalendo kwa nchi yenu kwanza.


Sina uhakika kama unajua kinachozungumziwa hapa..Juzi vijana wa kujitolea waliomaliza mkataba wao waliandamana kutaka kuajiriwa,unataka sema hawajaiva kijeshi?

Uzalendo unaouzungumzia hapa ni kulima mpunga Ruvu na Migazi ya Bulombora au ni uzalendo gani

Sisi hapa tunazungumzia haki..kama jeshini hazipo basi uraiani zipo..Pesa ya kujikimu ni haki yangu(nitailipa ujue) hivyo inatakiwa itolewe kwa wakati na kama ikichelewa ziwepo sababu genuine

Isipotolewa kwa muda,the simplest and immediate solution kuilazimisha serikali itoe ni kugoma.
 
Hamna namna ambavyo unaweza kutumia mtutu kumnyamazisha mtu mwenye 'uchungu at climax' kulia, akijitahadi atalia ila siyo kwa sauti!
 
Ze Heby
Sikiliza kijana, katika watu ambao wamepitia jakata na kukosa ajira mimi mmoja wapo lakini sifikirii hata siku moja eti nidai ajira kwa kuandamana kwani mkataba wangu ulionyesha ajira ukimuona mtu kapitia JKT na anaandamana jibu ahaiva kijeshi askari akiandamana maana yake ni uasi je waujua uasi unaathari gani kwa taifa?

Pili kaa ukijua JKT unafundishwa uvumilivu je uvumilivu wao upo wapi? Kama ni haki kuna namna ya kudai haki na sio kuandamana kitu ambacho kitaleta matatizo zaidi ya yale yaliyokuwa wanadai. JKT ni jando la taifa pale ndio unaenda kupata miiko ya nchi na uzalendo kwa nchi yako.

Mzalendo wa kweli ni yule anayeheshimu sheria za nchi na serikali iliopo sasa kama serikali imekuambia tunashughulikia tatizo kuna haja ya maandamano? Unavyosema haki yako sawa ni haki yako lakini serikali imekataa kukupa kabisa au utaratibu ulikua unafanyika wa kupewa na kwa nini usiwe na subira?
 
Last edited by a moderator:
Chinga One
Mimi nilibahatika kupitia JKT kwa kujitolea na nilimaliza mkataba wangu vizuri tu wa miaka miwili hivyo sikubahatika kuajiriwa ila nashukuru nimekua mzalendo safi wa nchi yangu na naendelea na shughuli zingine kama raia mwema.
 
Last edited by a moderator:
JKT kwa mujibu uje utie kelele hapa hata aibu huna we ungepitia jkt kwa kujitolea uujue uzalendo kwanza kwa nchi yako alafu tungeona kama utafanya ujinga huu wa migomo. Kwa mujibu nyinyi ndio ile mnapiga funika kombe mwanaharam apite kozi mtiemaji mtienaji miezi mitatu afu useme umepita jkt. Wewe pamoja na wenzio rudini tena jakata mkajifunze uzalendo kwa nchi yenu kwanza.

Uzalendo gani unaongelea? Hao wanaosababisha hawa vijana kugoma wana uzalendo gani? Uzalendo si kuwa zuzu bali ni kujua kuitetea nchi yako.

Sasa hawa wasiotimiza wajibu wao na kuwafanya watu kughafirika ni wazalendo? Tena wengi wao walipitia JKT au wamesahau hayo maadili ili tuwapeleke tena?
 
Sikiliza kijana katika watu ambao wamepitia jakata na kukosa ajira mimi mmoja wapo lakini sifikirii hata siku moja eti nidai ajira kwa kuandamana kwani mkataba wangu ulionyesha ajira ukimuona mtu kaoitia jkt na anaandamana jibu ahaiva kijeshi askari akiandamana maana yake ni uasi je waujua uasi unaathari gani kwa taifa? Pili kaa ukijua jkt unafundishwa uvumilivu je
uvumilivu wao upo wapi? Kama ni haki kuna namna ya kudai haki na sio kuandamana kitu ambacho kitaleta matatizo zaidi ya yale yaliyokuwa wanadai. Jkt ni jando la taifa pale ndio unaenda kupata miiko ya nchi na uzalendo kwa nchi yako. Mzalendo wa kweli ni yule anae heshimu sheria za nchi na serikali iliopo sasa kama serikali
imekuambia tunashughulikia tatizo kuna haja ya maandamano? Unavyosema haki yako sawa ni haki yako lakini serikali imekataa kukupa kabisa au utaratibu ulikua unafanyika wa kupewa na kwa nini usiwe na subira?

Napenda nikuulize swali dogo. Wanaoshindwa kutimiza wajibu wao kwa taifa ni wazalendo? Mie pia nimepitia JKT, operesheni Kambarage lakini natofautiana na wewe kwamba watu waende JKT ili wawe wavumilivu katika kudhulumiwa. Kila mtu akitimiza wajibu wake, hakuna migomo.
 
Napenda nikuulize swali dogo. Wanaoshindwa kutimiza wajibu wao kwa taifa ni wazalendo? Mie pia nimepitia JKT, operesheni Kambarage lakini natofautiana na wewe kwamba watu waende JKT ili wawe wavumilivu katika kudhulumiwa. Kila mtu akitimiza wajibu wake, hakuna migomo.

Kwa hiyo pindi serikali itapokuambia tatizo linashughulikiwa hiyo ni dhulma? Au hao vijana waliambiwa hawatapewa kabisa hiyo mikopo? Je serikali haijatimiza wajibu wake kwako na kwa mwingine? Mbona haitokei kipindi mnapolipwa kwa wakati hamgomi? Tatizo wanasiasa uchwara ndio wanaoangamiza taifa hili kila kitu kinajadiliwa kisiasa.
 
Kwa hiyo pindi serikali itapokuambia tatizo linashughulikiwa hiyo ni dhulma? Au hao vijana waliambiwa hawatapewa kabisa hiyo mikopo? Je serikali haijatimiza wajibu wake kwako na kwa mwingine? Mbona haitokei kipindi mnapolipwa kwa wakati hamgomi? Tatizo wanasiasa uchwara ndio wanaoangamiza taifa hili kila kitu kinajadiliwa kisiasa.

mwanafunzi huwa hagomi ujinga, anacho gomea ni haki yake, labda tu akosee staili ya kugoma..
 
Ze Heby
Sikiliza kijana, katika watu ambao wamepitia jakata na kukosa ajira mimi mmoja wapo lakini sifikirii hata siku moja eti nidai ajira kwa kuandamana kwani mkataba wangu ulionyesha ajira ukimuona mtu kapitia JKT na anaandamana jibu ahaiva kijeshi askari akiandamana maana yake ni uasi je waujua uasi unaathari gani kwa taifa?

Pili kaa ukijua JKT unafundishwa uvumilivu je uvumilivu wao upo wapi? Kama ni haki kuna namna ya kudai haki na sio kuandamana kitu ambacho kitaleta matatizo zaidi ya yale yaliyokuwa wanadai. JKT ni jando la taifa pale ndio unaenda kupata miiko ya nchi na uzalendo kwa nchi yako.

Mzalendo wa kweli ni yule anayeheshimu sheria za nchi na serikali iliopo sasa kama serikali imekuambia tunashughulikia tatizo kuna haja ya maandamano? Unavyosema haki yako sawa ni haki yako lakini serikali imekataa kukupa kabisa au utaratibu ulikua unafanyika wa kupewa na kwa nini usiwe na subira?

unaandika utafikiri ni raia wa marekani au Japan! nani asiyejua usanii wa serikali ya ccm! bila maandamano,migomo serikali hii haitimizi wajibu wake!! kwako wewe uzalendo ni kukaa kimya hata haki zako za msingi zinapoporwa! hujielewi unachozungumza!!
 
Last edited by a moderator:
unaandika utafikiri ni raia wa marekani au Japan! nani asiyejua usanii wa serikali ya ccm! bila maandamano,migomo serikali hii haitimizi wajibu wake!! kwako wewe uzalendo ni kukaa kimya hata haki zako za msingi zinapoporwa! hujielewi unachozungumza!!

Kaishi kongo kama hapa unadhulumiwa
 
siwezi kukimbia matatizo coz anaeyasababisha nimeshamjua ni kupambana nae kwa njia zote. watanzania wa leo wameamka unapoandika pumba zako jipime sana! Hao mafisadi walioifilisi nchi ndio wazalendo kwa upeo wako haba! rudi darasa la saba!
 
Back
Top Bottom